EPA billionaires shocked banker

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
EPA billionaires shocked banker
FAUSTINE KAPAMA
Daily News; Wednesday,January 28, 2009 @21:15​

A prosecution witness told a court in Dar es Salaam yesterday, how he was shocked after his clients became billionaires shortly after opening an account at the bank in 2005.

Ronald Manongi, Head of Operations and Administration with Commercial Bank of Africa (CBA), two businessmen, Rajab Shaban Maranda and Farijala Shaban Hussein, opened a joint current account number 0101305008 on August 31, 2005 in the name of Kiloloma and Brothers after depositing 500,000/-.

"But, two days later (on September 2, 2005), the Central Bank credited the account with 921,178.83 Pounds, equivalent to 1,864,949,294/45 for M/S B.C. Cars Exports Limited," he told principal resident magistrates Cypriana William, Saul Kinemela and Phocus Bampikya, who were presiding over the case.


Mr Manongi was testifying in a case in which Maranda and Hussein are charged with forgery and stealing 1.86bn/- from the Bank of Tanzania (BoT) through the External Payment Arrears (EPA). Led by Principal State Attorney Stanislaus Boniface, Mr Manongi, who is the second prosecution witness (PW2), told the court that he was suspicious of the transaction and expressed his concern in writing to BoT.

"I expressed to the supervisor of banks my concern and doubts on the way the bank account was opened and hurriedly credited with such a colossal amount of money," he said. He told the court that the BoT answered his queries later.

Referring to a letter signed by Deputy Governor Juma Reli, Mr Manongi testified that the Central Bank informed him that funds credited to Rashhaz Tanzania Limited and Kiloloma and Brothers were genuine payments originating from BoT in respect of national external debt obligations. Rashhaz Company owned by Maranda is also named to have been used in theft transactions from EPA account.


The witness told the court further that he also wrote a letter to partners of Kiloloma and Brothers, seeking to know the source of such huge amount of money and who would be the beneficiaries. He testified that Maranda replied to him that the money was payment of debt on behalf of their principal, M/S B.C.

Cars Exports Limited of Mumbai India and that they had authority to use part of such amount as per agreement they had entered with the company. After getting such information from both the Central Bank and Kiloloma and Brothers, the witness testified, he allowed the bank account to be operated.

The businessmen withdrew at least all the money within two months, as at December 6, 2005 the account had only 41,920/-. Mr Manongi testified that out of 1,864,949,294/45, only 350,000 Sterling Pounds, equivalent to 714,700,000/- was transferred through telegraphic transfer to B.C.

Cars Export Limited at HSBC in Britain and 41,920/- was deposited in another bank account operated by the accused. He told the court further that since the account was opened at his bank no any other deposit was made by the accused and had not operated it since they withdrew the entire amount. As of now, he testified, the accused have overdrawn 115,394/96. Hearing of the case continues today.
 
Kwa hiyo na huyo Juma Reli ni fisadi????, du kweli bongo kazi ipo????
 
Kwa hiyo na huyo Juma Reli ni fisadi????, du kweli bongo kazi ipo????

Unategemea nini wakati hii hela ya EPA ilikuwa imekaa hapo BOT haina mwenyewe na mwizi aliyemo ndani ya BOT ili aiibibe lazima ashirikiane na mwizi toka nje. Tanzania WIZI mtupu, mkubwa anaibia nchi, mdogo anamwibia mdogo mwenzake, wizi mtindo mmoja!!!
 
‘Akaunti ya akina Maranda iliaminiwa BoT'
Neema Mgonja
Daily News; Wednesday,January 29, 2009

Shahidi wa pili Ronald Manongi (49), katika kesi ya wizi wa mabilioni ya fedha za Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kutoka Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), inayowakabili watuhumiwa Farjala Hussein na Rajab Maranda amedai kuwa BoT ilimwondoa shaka juu ya akaunti iliyofunguliwa na washitakiwa.

Manongi ambaye alikuwa Mkuu wa Kitengo cha Utendaji na Huduma za Benki katika Benki ya Umoja wa Afrika (UBA), alidai katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana, kuwa wakati akiwa ofisa katika benki hiyo, wakurugenzi wa Kiloloma and Brothers, walifungua akaunti Agosti 31, 2005 namba 0101305008 na aliitilia shaka baada ya kuona imeingiziwa na BoT fedha ambazo ni zaidi ya Sh bilioni 1.8.

Mbele ya jopo la mahakimu wakazi chini ya Crypiana William ambaye ni Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Kazi, shahidi huyo alidai kuwa baada ya kuona akaunti hiyo imepata kiasi hicho cha fedha, alimwandikia Naibu Gavana wa BoT, barua iliyoelezea shaka yake kuhusu akaunti hiyo na kuituma kwa Kurugenzi ya Usimamizi wa Mabenki katika ofisi za BoT.

Kwa mujibu wa shahidi huyo, BoT ilimwandikia barua ya kumjibu ikiwa imeandikwa na Naibu Gavana Juma Reli, ambaye akimtaka aondoe shaka juu ya kampuni hiyo, kwa sababu BoT imeridhia akaunti hiyo kupata fedha hizo.

Baada ya kuandikiwa barua hiyo na BoT, shahidi huyo alidai kuwa aliwaandikia barua wamiliki wa akaunti hiyo, ambao ni washitakiwa katika kesi hiyo, akiwataka wamweleze zaidi kuhusu akaunti hiyo na kudai kuwa Septemba 26, 2005 alipokea barua kutoka kwa mmoja wa wamiliki wa akaunti hiyo, Maranda, aliyemweleza kwamba wana kibali cha kulipwa deni na BoT kwa niaba ya kampuni ya B.C. Cars Export na kwamba kazi ya kukusanya madeni kwa niaba ya kampuni za nje ni biashara yao mpya. Aliongeza kuwa Maranda alimwandikia kwamba kampuni yao ya Kiloloma and Brothers, ina kibali maalumu cha kutumia kiasi cha fedha ambazo zimelipwa na BoT kupitia akaunti yao na kwamba hayo ni moja ya makubaliano yao na B.C. Cars Export.

Manongi alidai kuwa baada ya kupata barua hizo kutoka BoT na kwa wamiliki wa akaunti ya Kiloloma and Brothers, aliiruhusu akaunti hiyo kuendelea na alimwandikia mkuu wake wa kazi, akimweleza kuwa amepata maelezo ya kutosha BoT na kwa wamiliki wa akaunti hiyo.

Akieleza jinsi fedha hizo zilivyoanza kutolewa katika akaunti hiyo, shahidi alidai kuwa baada ya akaunti kuingiziwa fedha, wamiliki hao walianza kuzitoa kwa nyakati tofauti na kwa mara ya kwanza walitoa Sh milioni 30. Shahidi alidai kuwa Septemba 5, 2005 wamiliki hao walichukua tena Sh milioni 150 na Septemba 13, mwaka huo walitoa Sh milioni 100 wakitumia hundi namba 062352.

Alidai kuwa Septemba 15, mwaka huo walitoa Sh milioni 300 kwa hundi namba 062354. Na kwa hundi namba 062355 walitoa Sh milioni 100. Alidai kuwa walitoa fedha tena Oktoba 7, 2005 kwa hundi namba 062356 zikiwa Sh milioni 20. Manongi alidai kuwa kwa mara ya kwanza kupitia akaunti hiyo Oktoba 19, mwaka huo walihamisha Sh milioni 100 kwenda nje ya nchi katika akaunti ya B. C.

Cars Export Uingereza. Pamoja na kutuma fedha hizo walichukua Sh milioni 100 kwa hundi namba 062357. Oktoba 21, mwaka huo, shahidi alidai kuwa walichukua Sh milioni 45 kwa hundi namba 062358 na baada ya kuchukua fedha hizo, Oktoba 24 walihamishia Sh milioni 308.7 katika akaunti ya B. C. Cars Export.

Baada ya kuhamisha fedha hizo wamiliki hao siku hiyohiyo walinunua dola 10,000 za Marekani kwa Sh milioni 11.5 kutoka UBA, wakiwa na lengo la kubadili fedha hizo kutoka kwenye shilingi kwenda dola. Alidai kuwa Novemba 6, mwaka huo kwa kutumia hundi namba 062360 walichukua Sh milioni 5.2. Shahidi aliiambia Mahakama kuwa baada ya hapo wamiliki hao hawakufanya malipo tena bali Novemba 8, 2006 walihamisha Sh 41,000 kwenda katika akaunti yao ya dola namba 0101305019.

Aliongeza kuwa tangu BoT ilipoingiza fedha katika akaunti hiyo, hakuna fedha yoyote iliyoingia zaidi ya kutolewa na kwamba mpaka sasa akaunti hiyo imebakiwa na Sh 115,000. Shahidi alidai kuwa fedha zilizolipwa nje ni Sh milioni 714.7. Baada ya kumaliza kutoa ushahidi upande wa utetezi uliokuwa na Wakili Majura Magafu uliomba upewe muda wa kupitia hundi zote zilizotumika mahakamani ili uweze kuuliza maswali kwa shahidi. Kesi hiyo ya wizi wa zaidi ya Sh bilioni moja iliahirishwa hadi leo itakapoendelea kusikilizwa.
 
Kesi ya EPA: Shahidi azidi kuibua mapya

na Happiness Katabazi
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MKUU wa kitengo cha uendeshaji wa huduma kwa wateja katika Commercial Bank of Africa, Ronald Manongi, ambaye ni shahidi wa pili katika kesi ya wizi wa sh bilioni 1.8 za EPA inayomkakili Farijala Hussein na Mweka Hazina wa CCM Mkoa wa Kigoma, Rajabu Maranda, jana alimaliza kutoa ushahidi wake kwa kuieleza mahakama kuwa hajawahi kupokea malalamiko toka Kampuni ya BC Cars Export Ltd ya Mumbai, India kwamba imedhulumiwa fedha na Kampuni ya Kiloloma & Brothers ya Tanzania.

Shahidi huyo, alieleza hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, alipokuwa akijibu maswali ya wakili wa utetezi, Majura Magafu.

Alidai BC Cars Export Ltd yenye akaunti UK iliingiziwa fedha hizo kwa njia ya Telegraph Transfer (TT) na kampuni ya Kiloloma & Brothers ambayo ilikuwa na akaunti Commercial Bank of Africa.

Hata hivyo, alidai BoT haijawahi kuitaarifu benki yake kwamba sh bilioni 1.8 walizoiingizia Kiloloma & Brothers si malipo halali.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili Magafu na Shahidi Manongi:

Wakili:Jana (Juzi) wakati unaongozwa na msomi mwenzangu, Stanslaus Boniface, kutoa ushahidi, uliiambia mahakama kwamba baada ya kuona kiasi hicho cha fedha kimeingia kwenye akaunti ya washtakiwa ulipatwa na wasiwasi, eh ulimpigia simu Ofisa wa BoT? Tutajie jina lake tafadhali?

Shahidi: Iman Mwakosya ambaye pia anakabiliwa na kesi za EPA katika mahakama hii.

Wakili: Eeeh.. Mwakosya alikujibu nini kwenye mazungumzo yenu katika simu?

Shahidi: Aliniambia fedha hizo ni halali na BoT imezituma kwa Kiloloma & Brothers.

Wakili: Ulimuuliza Mwakosya ni kwa nini BoT inawalipa hizo fedha?

Shahidi: Alinijibu ni deni la EPA.

Wakili: BoT waliingizia fedha akaunti kwa Tsh au fedha za kigeni ambayo zina thamani gani?

Shahidi: Paundi 921,178.83.

Wakili: Kuna siku yoyote BoT waliwahi kuwaandikia kwamba malipo hayo si halali?

Shahidi: Hawajawahi kuiandikia benki yetu kwamba malipo hayo si halalali.

Wakili: Kuna siku wateja wangu walikiuka masharti ya benki mliyowapa kabla ya kufungua akaunti yao?

Shahidi: Sikumbuki kama waliwahi kukiuka masharti.

Wakili: Ni wakati gani benki inaweza kumwambia mteja hapo umekiuka taratibu?

Shahidi: Pale mteja anapokiuka taratibu za kibenki.

Wakili: Nyie benki mnaruhusiwa kuingilia matumizi ya fedha za mteja wenu?

Shahidi: Hatuingilii.

Wakili: Mteja anapokuja na leseni na deed of partnership ya kampuni yao zinazoonyesha wanafanya biashara mbili tofauti, yaani leseni inasema wanafanya biashara ya kukusanya manyoya halafu deed of partnership inasema wanakusanya madeni mnafanyaje?

Shahidi: Sisi tulimwangalia mdhamini wa Kiloloma & Brothers ambaye ni Rashhaz(T)Ltd, ambaye ndiye alimtambulisha kwetu tukawafungulia akaunti. Na kwa mujibu wa saini ya akaunti ya Rashhaz(T)Ltd inaonyesha Maranda ndiye mmiliki kwa kampuni hiyo.

Wakili: Utakubaliana na mimi benki yenu, suala la leseni na deed of pertneship mnalifumbia macho?

Shahidi: Kimya.

Wakili: Kimsingi mtakubaliana na mimi benki yenu, Kiloloma & Brothers hamna tatizo nayo?

Shahidi: Hatuna tatizo nayo.

Wakili: Benki yenu mliwahi kuona makubaliano ya Kiloloma & Brothers kuitumia fedha BC Cars Export Ltd?

Shahidi: Hatujawahi kuyaona.

Wakili: Benki yenu ilishawahi kupata malalamiko toka BC Cars Export Ltd kwamba wamedhulumiwa fedha zao na Kiloloma & Brothers?

Shahidi: Hatujawahi kupata malalamiko.

Wakili: Mnawaamini wateja wenu (washtakiwa)?

Shahidi: Tunawaamini ndiyo maana tuliendelea kufanya nao biashara.

Aidha shahidi wa tatu katika kesi hiyo, Meneja wa Kenya Commercial Bank Tawi la Mlimani, Twilumba Talawa (34), alidai yeye ndiye aliyewafungulia akaunti ya Kiloloma & Brother washtakiwa wakati huo akiwa Meneja Msaidizi Kitengo cha Huduma kwa wateja wa benki ya United Bank of Africa.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya Wakili wa Serikali na shahidi:

Wakili: Agosti mwaka 2003 ulikuwa ukifanya kazi katika benki gani?

Shahidi: United Bank of Afrika (UBA).

Wakili: Kuna umoja wa biashara unafahamika kwa jina la Kiloloma & Brothers, uliufahamu lini na vipi?

Shahidi: Niliufahamu baada ya wateja wangu kufika ofisini kwa ajili ya kufungua akaunti.

Wakili: Angalia hii fomu, waliomba kufungua akaunti ya kampuni hiyo ni akina nani?

Shahidi: Farijara na Maranda.

Wakili: Watu hao wapo hapa mahakama ebu watambue?

Shahidi: Wale wawili walioketi pale kizimbani (anawanyooshea kidole).

Wakili: Fomu hiyo ya kufungulia akaunti ya kampuni hiyo ililetwa na nani ofini kwenu?

Shahidi: Farijara Hussein na fomu hiyo alinikabidhi mimi.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili wa utetezi Majura Magafu na shahidi:

Wakili: Je huyu Farijara na Maranda walileta leseni wakati wanafungua akaunti?

Shahidi: Ndiyo.

Wakili: Hiyo leseni benki inawasaidia nini?

Shahidi: Haitusaidii kitu. Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa leo.


 
Back
Top Bottom