Enzi Hizoooooooooo RIP

chigwiyemisi huko aka jumanne au john aka ndugu zangu wa dodoma khaa aka msituuuuu
 
Maisha ya mpira mabaya sana Tanzania, siku hizi Zamoyoni unamkuta anashinda kijiweni na miwani mikubwa anaganga njaa pale Hadees Posta Mpya kwa Kassim Dewji, wakati in real footballing world ya leo baada ya kutandika daluga alitakiwa muda huu awe ana many investments anasimamia. Pengine wakati wao hawakuwa na washauri wazuri.
 
Dah huyu jamaa alikuwa fundi kweli RIP Method Mogela.Nilibahatika kucheza nae kwenye timu ya JKT Oljoro aliyojiunga nayo kwa mujibu wa sheria baada ya kumaliza Arusha Technical College mwaka 1989.Mwaka huo alichaguliwa kwenye kombaini ya timu ya JKT iliyoshiriki kwenye mashindano ya majeshi huko Ruvu,alikuwa star wa mashindano na mkuu wa JKT kipindi hicho Makame Rashid ambae alikuwa mpenzi mkubwa wa Simba alimpeleka Msimbazi hata hivyo alikuwa ni mpenzi mkubwa wa wana Jangwani hivyo alipokutana na hela za Marehemu Gulamal Abbas alienda Jangwani.

Wakaja unda dream team ambayo sijui kama timu yangu ya Yanga itakuja tokea tena.First eleven hiyo ilikuwa hivi 1.Steven Nemes 2.Mrundi mmoja jina nimesahau 3.Keneth Mkapa 4.Method Mogela 5.Constatine Kimanda 6.Nico Bamabaga 7.Sekilojo Chambua 8.Steven Musa 9.Said Mwamba 10.Mohamed Hussein 11.Lunyamila.Kama kuna mtu anakumbukumbu zaidi anaweza nisahihisha hapo,hasa wewe mwana Jangwani mwalimu gfsonwin upo hapo
 
Maisha ya mpira mabaya sana Tanzania, siku hizi Zamoyoni unamkuta anashinda kijiweni na miwani mikubwa anaganga njaa pale Hadees Posta Mpya kwa Kassim Dewji, wakati in real footballing world ya leo baada ya kutandika daluga alitakiwa muda huu awe ana many investments anasimamia. Pengine wakati wao hawakuwa na washauri wazuri.
Katika wachezaji wa generation yake huyu Zamoyoni Mogela ana nafua sana ukilinganisha wa wenzake,hata afya yake sio mbaya sana anag'aa kidogo ukilinganisha wa wenzake wa enzi hizo.Alikuwa anafanya biashara biashara sijui kama bado anaendelea na japo sina uhakika lakini anaweza akawa na nyumba moja,mbili kama sio zaidi hapa mjini
 
RIP Method Mogellla, alikuwa Ruvu jkt 1989/90 kwa mujibu wa sheria akitokea nadhani Arusha Tech College. Alikuwa ni mchezaji hodari sana kabla ya kujiunga na Simba na baadae Yanga.
 
Methord A Magella ,Shule - Mtwara Technical Secondary School ,
Chuo- Arusha Technical College(TCA)
Timu- RTC Mtwara, RTC Arusha, AICC, Simba SC, Young African FC( Yanga)
 
Back
Top Bottom