Duniani Kuna Imani zaidi ya Moja?

Nundu_Tanzania

JF-Expert Member
Apr 19, 2019
811
349
Maisha yote ya mtu hayatenganishwi na yanategemea imani. Kwa maneno mengine, maisha ni imani. Ye yote anayeishi duniani maisha yake ni imani yake.

Hatahivyo, swali ni kwamba imani ni nini? Imani ni kwa nani au nini:tunaamini nini? Duniani kuna imani zaidi ya moja au mbali mbali?

Kuhusu imani ni nini. Kadiri ya Waebrania, 11:1 anaeleza maana ya imani kuwa ni kuwa na uthabiti katika vitu tunavyovitumainia, na hakika ya mambo yasioonekana.

Imani ni uthabiti na uhakika katika vitu tunavyovitumainia na mambo yasioonekana. Maneno "uthabiti" na "uhakika" yana maana ya 'uelewa'.

Uelewa maana yake ni ufahamu wa kina wa mambo, maaarifa na elimu ya vitu. Tukisema Petro ana imani maana yake Petro ana ufahamu wa kina wa mambo, maarifa na elimu ya vitu.

Kwa msingi huo, katika maana yake pana, imani ni kipaji anachokuwa nacho mtu kinachomwezesha kufahamu kwa kina na bayana vitu tunavyovitumainia na mambo yasioonekana. Kwa hiyo imani ni uwezo wa hali ya juu wa akili.

Watu kwa mfano, hawawezi kumchagua mtu ambaye hawamfahamu kwa kina awe mtunza fedha wa kikundi chao. Hawamwamini mtu ambaye bado hawajamfahamu kwa kina ni nani: maisha yake, historia yake na ya ukoo wake; tabia na mwenendo wake awatunzie fedha zao.

Wanaposema tunamwamini Petro awe mtunza fedha wa kikundi chetu maana yake wanamfahamu kwa kina kwamba lolote litakalotokea sasa na baadae, fedha yao itakuwa na itabaki salama.

Kumwamini Petro awe mtunza fedha wa kikundi ni suala la utafiti mwingi kuchunguza kwa kina Petro ni nani: tabia yake, historia ya ukoo wake na maisha yake ya uchumi na kijamii.

Imani mbali ya kuwa ni kipaji, kwa wengine ni suala la elimu: kujifunza na kuchunguza kwa kina tabia na maumbile ya vitu na mambo mbalimbali.

Imani ni ufahamu wa juu wa akili hivyo isichanganywe na ufahamu wa kawaida tunaoupata kwa kupitia milango mitano ya fahamu: pua, macho, masikio, ngozi na ulimi.

Imani ni mambo ya akili hivyo ni kinyume cha hisia au miguso. Kwa sababu hii kwamba imani iko kwenye akili, inafanyika na akili haiwezekani imani kuwa zaidi ya moja au mbali mbali.

Imani inatoka kwa akili inafanya na kufafanua kazi za kiakili. Hii maana yake ni kuwa imani haitenganishwi na kazi za kiakili.

Kama ilivyo akili haifanyi makosa au uchungu pia imani haifanyi makosa na haisababishi uchungu, majeraha au uharibifu.

Kazi za kiakili ni uumbaji, uhai, imani, maarifa, elimu, uvumbuzi, kufafanua mafundisho ya imani na maadili, mfumo, na maendeleo.

Duniani kazi za kiakili ni kwa njia ya imani. Lakini tofauti na tunavyoweza kufahamu imani bila kutengana na akili haifanyi makosa na haisababishi uchungu, majeraha au uharibifu.

Imani ni kwa akili. Kinyume na akili sio imani. Imani sio kwa kingine chochote isipokuwa kwa akili. Kwa sababu hiyo imani ni moja duniani. Duniani hakuna imani zaidi ya moja au mbali mbali.

Ikiwa inatoka kwa akili, imani sawa na akili haifanyi makosa na haisababishi uharibifu, uchungu au majeraha.

Kingine chochote kinachofanya makosa au kusababisha uchungu, uharibifu au majeraha; hiyo sio akili pia hiyo sio imani.
 
Mkuu umeongea kuhusu imani ila kuna paradox hapo kwenye neno "imani" hujatuelewesha hapo umezungumzia imani gani

1. faith
2. trust


Hivi vitatu vyote kwa kiswahili vina tafsiri moja lakini kimatumizi/kimaana vinatofautiana

Kupitia mfano wako wa mtunza hazina aliyechaguliwa na kikundi kwa ajili ya kutunza fedha utagundua dhana ya imani iliyotumika hapo ni "trust" kwasababu hii ina deal na background history na record za mtu ambaye wanamjua personal na sio "spirituality" kwa tafsiri nyingine unaweza kusema wanachama wa hicho kikundi wana confidence na huyo mtu

Imani ya kusema kuna maisha baada ya kifo hii ni "faith" maana ina deal na spiritual
 
Mkuu umeongea kuhusu imani ila kuna paradox hapo kwenye neno "imani" hujatuelewesha hapo umezungumzia imani gani

1. faith
2. trust


Hivi vitatu vyote kwa kiswahili vina maana moja lakini kimatumizi/kimaana vinatofautiana

Kupitia mfano wako wa mtunza hazina aliyechaguliwa na kikundi kwa ajili ya kutunza fedha utagundua dhana ya imani iliyotumika hapo ni "trust" kwasababu hii ina deal na background history na record za mtu ambaye wanamjua personal na sio "spirituality" kwa tafsiri nyingine unaweza kusema wanachama wa hicho kikundi wana confidence na huyo mtu

Imani ya kusema kuna maisha baada ya kifo hii ni "faith" maana ina deal na spiritual
Kiswahili ni lugha changa sana, bado haina misamiati kukidhi mawasiliano katika nyanja mbalimbali.

Kwa sababu ya uchanga wa lugha ya kishwahili umesababisha makosa kwenye tafsiri ya lugha kwa mfano, kutoka lugha ya kigiriki (kiyunani), kilatini, kifaransa na kingereza kuja katika kishwahili.

Imani ninayoizungumzia hapa ni faith.

Tofauti na trust ufahamu wa kawaida kwa njia ya milango mitano ya fahamu, faith ni uwezo wa hali ya juu wa akili.
 
Kiswahili ni lugha changa sana, bado haina misamiati kukidhi mawasiliano katika nyanja mbalimbali.

Kwa sababu ya uchanga wa lugha ya kishwahili umesababisha makosa kwenye tafsiri ya lugha kwa mfano, kutoka lugha ya kigiriki (kiyunani), kilatini, kifaransa na kingereza kuja katika kishwahili.

Imani ninayoizungumzia hapa ni faith.

Tofauti na trust ufahamu wa kawaida kwa njia ya milango mitano ya fahamu, faith ni uwezo wa hali ya juu wa akili.
Sawa nimeelewa shabaha yako ilikuwa kutumia "faith" ila kupitia mfano wako wa mtunza hazina dhana ya "trust" ina fit vizuri huku "faith" ikipwaya
 
Sawa nimeelewa shabaha yako ilikuwa kutumia "faith" ila kupitia mfano wako wa mtunza hazina dhana ya "trust" ina fit vizuri huku "faith" ikipwaya
Mkuu hapa naunga mkono hoja. Kwa Petro walitumia imani ya Trust kuliko Faith, kwanza ieleweke hivi petro alikuwa mdhaifu sana kwenye imani ya kiroho huyu ndiye aliemkana yesu, pili huyu ndyie aliyemkata mtu sikio yesu akalirudishia na kumfundisha kuwa vita hii sio ya kimwli ni yakiroho.

Walimuamini kuwa mtunza fedha kwa kua alikua mtu anayejiamini na mwenye kazi yake ( mvuvi) . Faith ilichukuwa nafasi ndogo sana kulinganisha na Trust.
 
Kiswahili ni lugha changa sana, bado haina misamiati kukidhi mawasiliano katika nyanja mbalimbali.

Kwa sababu ya uchanga wa lugha ya kishwahili umesababisha makosa kwenye tafsiri ya lugha kwa mfano, kutoka lugha ya kigiriki (kiyunani), kilatini, kifaransa na kingereza kuja katika kishwahili.

Imani ninayoizungumzia hapa ni faith.

Tofauti na trust ufahamu wa kawaida kwa njia ya milango mitano ya fahamu, faith ni uwezo wa hali ya juu wa akili.
Mifano yako imejikita katika Trust, na sio Faith...
 
"Imani huambatana 100% uwezo mkubwa wa kiakili"
Uhakika ya mambo yatarajiwayo. Ni maneno yanao dai elimu,Maarifa,Uwezo wa hali ya juu na uelewa wa mambo.
Kutarajia kitu flan lazima ujue ni nn hicho?Nn kitakifanya kitimie? kwa mchakato upi? Na kwann(factors depends) and for how long?
 
Mifano yako imejikita katika Trust, na sio Faith...
Nimeandika kuwa imani si kwa kingine chochote isipokuwa kwa akili.

Kwa hiyo watu wanaposema wanamwamini fulani kuwa mtunza fedha wao, wanaona usalama wa fedha zao badae. Hapa "baadae" hawaioni lakini wana uhakika kuwa fedha yao itakuwa salama. Hii ni akili si maoni.
 
Sio kweli kwamba kuwa na imani au kutokuwa na imani kuna uhusiano wowote na uwezo wa akili.
"Imani huambatana 100% uwezo mkubwa wa kiakili"
Uhakika ya mambo yatarajiwayo. Ni maneno yanao dai elimu,Maarifa,Uwezo wa hali ya juu na uelewa wa mambo.
Kutarajia kitu flan lazima ujue ni nn hicho?Nn kitakifanya kitimie? kwa mchakato upi? Na kwann(factors depends) and for how long?
 
Sio kweli kwamba kuwa na imani au kutokuwa na imani kuna uhusiano wowote na uwezo wa akili.
Wakristu tunakubaliana kwamba ukisoma biblia na kutaka kumjua mungu lazima upate usaidiz wa holy spirit.
sasa unadhan kazi ya holy spirit ni kuongeza appitite?


Ok .Ivi Mr YODA kwa akili yako unadhani kuna na uhakika na mambo yatarajiwayo Imani hiyo ni rahis? LAMZIMA UWE UNAJUA NA UNAELEWA JUU YA MAMBO KUHUSU. The more u read and understand the bible your bilieve power become stronger and stronger (Manipulation power)
Manipulation power we can measure it with time ili kupata matokeo
strong short time
weak long time
In spiritula Cosmology we call it vibration vibration the higher vibration, short time and vice versa and many other lawas that are interconnected to each other

YOUR MIND IS EVERYTHING THUS EVVERY THING IS CONNECTED


Yoda read and keep questioning, bring t yoo suggestions labda u may have a good point.

try Prove me wrong that is gow we learn.
 
Kuna tofauti Kati ya neno “faith” na “beliefs”. Pamoja na uelewa wangu mdogo wa mambo ya kidini na elimu dunia. Binafsi fikra zangu huteseka sana kuhusiana na mapokeo ya kiimani. Imani ya kuamini kuwa ipo nguvu inayotuweka duniani naamini 100%. Neno linalofuata kwangu. Je! Ni lazima kuwa na imani ya kidini.? Halo nakosa jibu kwa mitazamo ya kielimu, ni kuwa dini hizi tulizo nazo tulizipokea toka kwa wakoloni walioitwa missionaries. Tukaacha ya kwetu hatimae tukashika ya wakoloni. Ninapochanganyikiwa kabisa dini hizi tumezishika kuliko wenye dini. Imani hizi kwetu ndio uponyaji, nguvu za kiuchumi na maisha ya baadae baada ya kuacha ulimwengu huu . Najiuliza tungebaki na zile imani za zamani tungekuwaje hizi sasa. Je nisipofuata imani hizo itakuwaje! Imani kwangu ni jambo zito naombeni uelewa zaidi.
 
Kuna tofauti Kati ya neno “faith” na “beliefs”. Pamoja na uelewa wangu mdogo wa mambo ya kidini na elimu dunia. Binafsi fikra zangu huteseka sana kuhusiana na mapokeo ya kiimani. Imani ya kuamini kuwa ipo nguvu inayotuweka duniani naamini 100%. Neno linalofuata kwangu. Je! Ni lazima kuwa na imani ya kidini.? Halo nakosa jibu kwa mitazamo ya kielimu, ni kuwa dini hizi tulizo nazo tulizipokea toka kwa wakoloni walioitwa missionaries. Tukaacha ya kwetu hatimae tukashika ya wakoloni. Ninapochanganyikiwa kabisa dini hizi tumezishika kuliko wenye dini. Imani hizi kwetu ndio uponyaji, nguvu za kiuchumi na maisha ya baadae baada ya kuacha ulimwengu huu . Najiuliza tungebaki na zile imani za zamani tungekuwaje hizi sasa. Je nisipofuata imani hizo itakuwaje! Imani kwangu ni jambo zito naombeni uelewa zaidi.
Andiko lako ni zuri.

Kwa kweli huwa siwaelewi watu wanaodai kuwa tulikuwa na dini yetu (zetu) Afrika. Naweza kusema ni suala la uelewa.

Dini ni utaratibu wa kutekeleza mambo au vitu vitakatifu.

Tunaposema dini tofauti na imani tunazungumzia watu "waliotengwa" na "kuingizwa" kwa kufanyiwa tendo la kidini na kiliturujia la sakramenti, baraka na wakfu linalompatia mtu uwezo wa kutekeleza uweza mtakatifu, ambao hauwezi kutoka mahali pengine popote isipokuwa kwa Mungu.

Yako mambo au vitu ulimwenguni haviwezi kufanywa na kila mtu isipokuwa na watu tu waliopewa mamlaka hayo. Ziko kazi ili kuweza kuzitekeleza lazima kuacha mambo mengine yote ya maisha kwa ajili ya kazi hiyo.

Utaratibu huu sio wa nyakati zetu. Haukuanza wakati wa sheria ya Kristo au wakati wa Musa -sheria ya Musa. Ni utaratibu wa wakati wote. Hivi ndivyo maisha ya mtu (binadamu) yalivyo tangu kuwepo kwake na ni wa mahali pote duniani.

Wafrika wanadai waalikuwa na dini zao kabla ya kuja wamisionari (Ukristo) Afrika. Hii ni kweli.

Lakini kitu Wafrika wanafanya makosa ni kushindwa kuelewa kuwa hata wamisionari (wazungu) nao walikuwa na dini zao.

Hapo hapo, makosa mengine wanayofanya Wafrika wanaodai walikuwa na dini zao ni juu ya namna walivyokuwa wanafanya au wanatekeleza matambiko (kutolea sadaka) ya dini yao na namna dini ya kikristo inavyofanya au kutekeleza tambiko-kutolea sadaka.

Ukichunguza madai hayo ya hao wanaojiita wafrika unagundua ni upotoshaji wenye malengo na tamaa ya uchumi na utawala.

Hakuna ukweli wowote kwamba Wafrika walikuwa na dini zao ambazo jamii za maeneo mengine hawakuwa nazo, hakuna!

Utaratibu wa dini hata kama ni ya uongo ni mmoja, unafanana pote duniani.

Dini ni watu waliopewa na Mungu mwenyewe mamlaka ya kutekeleza uweza mtakatifu; uwezo wa kufanya mambo matakatifu.

Mtu anaweza kuwa na imani lakini sio kila mtu anaweza kutekeleza uweza mtakatifu. Kwa mfano kutolea sadaka au tambiko anatakiwa mtu aliyetengwa na kuingizwa kwa kuwekewa mikono mitakatifu kwa ajili ya dini.

Tufahamu kwamba kutolea sadaka au matambiko ni mambo au vitu vitakatifu. Haya ni mambo ya akili, matakatifu.

Aidha mafundisho ya imani na maadili ni mambo ya akili matakatifu. Hapa moja kwa moja tunaona Kanisa ambalo ni mamlaka ya dini.

Yesu angeweza kusistiza au kusema tu juu ya imani kama kitu pekee anachotakiwa mtu kuwanacho.

Lakini pamoja na kufanya hivyo kusema juu ya imani, Yesu aliweka Kanisa -mamlaka ya dini. Kwa nini? Kwa sababu imani ni pia pamoja na watu waliotengwa na kuingizwa kwa kuwekewa mikono mitakatifu tendo la kidini na kilitirujia la sakramenti, baraka na wakfu linalompatia mtu uwezo wa kutekeleza uweza mtakatifu.

Kama hatujifunzi maana yake hatuwezi kuwa na imani pia hatuwezi kuijua dini.

Wafrika hatufahamu dini tunayosema "Dini Yetu" ndio sababu tunasema dini ya wazungu. Kama tungeifahamu vizuri dini tusingesema hii ni dini yetu na hii ni dini yao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom