Dunia isimdharau Kim Jong-un

Kiduku ana mkwara tu siku USA wakilamsha dude atafyata mkia
Sasa utasemaje ana mkwara huku akiwa na uwezo wa kumpiga mmarekani akiwa kwake tu, utasemaje ana mikwara huku Ana uwezo wa Bomu la nuclear na lile la hydrogen . utasemaje ana mikwara wakati anatumia operating system ya kwake . kiufup yupo vizuri sizan kama ni jambo jepesi kumpiga
 
Mwaka 1958 General Douglas McArthur wa Jeshi la Marekani alipoamuru askari wa Marekani wavamie North Korea Kabla White house haijaidhinisha, Wachina 2000000 walijiandikisha kwenda kupigana na kuisaidia Korea. Vita iliisha mapema kwa aibu kubwa kwa Marekani.McArthur alikuwa discharged na Mkuu wa Nchi. Leo Mrusi na Mchina kuna uwezekano mkubwa wakaingia Katika vita ile. Trump ameliona hilo ndio maana hajafanya kitu kikubwa hadi sasa.
Uko sahihi mkuu, hata mimi nilikuwa na wasi wasi Sana na jeuri ya Nk Inaonekana urusi na China, hawa ndo wanampa kiburi Kiduku.
 
Ana technologia ya kufa mtu ambayo mataifa yote duniani yanaitafakari. Kim sio mpumbavu kumbwekea Marekani vile. Huyu jamaa inasemekana ana uwezo wa kuzima satellites zote angani zinazoendesha mifumo yote ya ki-eletronic duniani ikiwemo ile ya bwana mkubwa wa Lushoto.

Anaweza kusababisha nyambizi na ndege za bwana mkubwa zikajam zote.

Tusishabikie vita ya Korea na majirani zake na Marekani inaweza kuiyumbisha dunia nzima.
Wewe wa namanyere rukwa umejuaje hiyo unayosema technologia ya kufa mtu ambayo jirani yake mjapani hajaijua
 
kiduku mkwala tu.....ni sawa na mtu una nyumba ya nyasi na una miliki SMG.
Hiyo Nyumba ina heshima kuliko kuwa na gorofa lenye manati ndani... Mtafute masikini mwingine mwenye kiburi kwa Marekani kama alivyo NK.
 
Kuna watu hawafikiri vizuri. Chuki zao binafsi dhidi ya marekani zinawafanye wawe na ndoto halisia za kuona marekani imefutika. Hawapendi kuwaza na kufikiri kiuhalisia. Historia tu inakataa kabisa dunia kukaliwa na nchi mbili au zaidi super power. Haijawahi kabisa kutokea. NK anavumiliwa tu ili kuepusha majanga na gharama kubwa za vita hasa baada ya vita. Wakubwa wakimwamulia hats hizo ICBM hazitaruka, zitaharibiwa hapo hapo NK.

Mpaka sasa hakuna viashiria vinavyoonyesha kuwa marekani ita-collapse soon zaidi tunaiona ikiimarika kila Siku hivyo itakuwepo sana kwa muda mrefu.
Marekani ina silaha nyingi sana za kinuclear ambazo hana uhakika kama hakuna mtu anaeweza kuvipiga kombora vikalipuka. Maana vikilipuka vitailipua nchi nzima. Ndiyo maana Marekani hataki vita inayoweza kupiganiwa ndani ya Marekani kwa kuepusha hilo. Siku zote Marekani anakuwa wa kwanza kurusha risasi hukohuko adui iliko ili kueousha hilo. Angekuwa na uhakika 100% wa kumpiga NK angeshapiga muda mrefu uliopita. Tukubali tu kwamba bw mkubwa hapa atabaki kukenua tu.
 
kama kuna uchawi duniani basi uchawi mkubwa ni Technology north siyo watu wakupuuza linapokuja suala la technology !!
Sijaona jipya walilo lifanya mpaka sasa kombora wanazo fanya majaribio wenzao walisha yafanya 60 years back unazan technology ni stagnant ivo watu wako na
Laws/laser weapons system nn midubwana iyo??
 
Sijaona jipya walilo lifanya mpaka sasa kombora wanazo fanya majaribio wenzao walisha yafanya 60 years back unazan technology ni stagnant ivo watu wako na
Laws/laser weapons system nn midubwana iyo??
Huwezi kuona siyo technology zote huwa zinawekwa wazi !!
uchawi wa technology ni siri kubwa sana !!
North wanaweza fanya jambo ambalo linaweza shangaza dunia !!
Siyo wepesi linapokuja suala la technology hizo laser zinaweza kuwa loser yote yanawezekana wala hujawahi kuona sehemu iyo loser ilipo fanyiwa majaribio!!
 
Ana technologia ya kufa mtu ambayo mataifa yote duniani yanaitafakari. Kim sio mpumbavu kumbwekea Marekani vile. Huyu jamaa inasemekana ana uwezo wa kuzima satellites zote angani zinazoendesha mifumo yote ya ki-eletronic duniani ikiwemo ile ya bwana mkubwa wa Lushoto.

Anaweza kusababisha nyambizi na ndege za bwana mkubwa zikajam zote.

Tusishabikie vita ya Korea na majirani zake na Marekani inaweza kuiyumbisha dunia nzima.
Upo sahihi , kwanini dogo anajiamini sana
 
Putin aliwahi sema kumwekea vikwazo north Korea ni kuzidi kumhamasisha atengeneze mabomu zaidi kwani lengo lake ni kufeel safe,hivyo kuhatarisha usalama wake kutazidi kumfanya apambane zaidi,hivyo njia bora ni negotiations!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom