sifongo
JF-Expert Member
- Jun 5, 2011
- 4,896
- 5,302
Mungu mtu wa baadhi ya raia.Cheki utakavyoshukiwa
Sio kushukiwa mkuu, kuna vitu vingi vya msingi vya kujadili ndani ya CCM zaidi ya DR SLAA, CCM ndio imeshika dola kila kero na manun'guniko juu ya serikali CCM haiwezi kukwepa lawama, tatizo ni kuwa hizo kero za wananchi hazijibiwi badala yake tunasikia hadithi za Slaa kila kukicha, Slaa kawafanya nini CCM, ukweli wa maneno yake juu ya Serikali dhaifu ndio vinafanya CCM wamuandame au kuna lingine?
Mpaka leo kero za EPA, MEREMETA,RICHMOND,KAGODA na matakataka mengine kibao bado havijapatiwa majibu lakini wenye midomo mirefu (NAPE, MWIGULU na wapambe wao) wala hawatoi maelezo badala yake wana -skip na kuhamia mambo yasiyo na tija.