Elections 2010 Dr. Slaa arudi tena Mbulu

Gurtu

JF-Expert Member
May 15, 2010
1,247
342
Ilikuwa majira ya saa 10:30 mchana alitua na Helkopta kama kawaida. Alizungumzia mambo ya msingi yatakayofanyika siku Chadema itakapoingia madarakani:
1. Kushusha bei ya vifaa vya ujenzi ili wananchi wajenge nyumba za maana.
2. Elimu: Tunapofungua milango yetu kuhusu ajira na huku Watanzania tukiwa nyuma kielimu ipo siku tutashangaa afisa mtendaji wa kata atatokea Uganda.
3. Kupunguza gharama ya uendeshaji wa Serikali: Yeye kama rais atapunguza bajeti ya nyumba ya rais, atatembelea Landcruiser la thamani ya milioni 100 badala ya shangingi la milioni 200 ili aokoe milioni 100. Alisema kuwa ni muda wa serikali kukaza mkanda na wananchi kulegeza mikanda.

Kwa kifupi watua walijaa uwanjani huku Dr. Slaa akitumia dakika kama 30 na hatimaye akaelekea Endabsh hadi Karatu na kabla ya hapo alikuwa akitokea Dongobesh
 
safi sana ukipata picha tupe pia
Nilishindwa kuambatanisha picha. Pia naomba kufanya marekebisho katika neno"Dongobsh".
Badala yake ni Dongobesh.
DSCN4208.JPG


 
Kuna tetesi kuwa huko Kwermusl (mbulu ndani ndani) na irqoor da'aaw wananchi wanapiga yowe pindi wamwonapo Marmo akipiga kampeni.

Vipi Akonaay [Chadema] atampuzisha Marmo?

Tujuze plz!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Ahsante Gurtu kwa kuweka picha ya Dongobesh. Heri ninyi Mkoa wa Manyara kwa vile mmeuchukia ufisadi. Hakuna shaka kura za Dongobesh zitaenda kwa Dr. Slaa, Mh. Akunaay na Diwani Siasi
 
Ilikuwa majira ya saa 10:30 mchana alitua na Helkopta kama kawaida. Alizungumzia mambo ya msingi yatakayofanyika siku Chadema itakapoingia madarakani:
1. Kushusha bei ya vifaa vya ujenzi ili wananchi wajenge nyumba za maana.
2. Elimu: Tunapofungua milango yetu kuhusu ajira na huku Watanzania tukiwa nyuma kielimu ipo siku tutashangaa afisa mtendaji wa kata atatokea Uganda.
3. Kupunguza gharama ya uendeshaji wa Serikali: Yeye kama rais atapunguza bajeti ya nyumba ya rais, atatembelea Landcruiser la thamani ya milioni 100 badala ya shangingi la milioni 200 ili aokoe milioni 100. Alisema kuwa ni muda wa serikali kukaza mkanda na wananchi kulegeza mikanda.

Kwa kifupi watua walijaa uwanjani huku Dr. Slaa akitumia dakika kama 30 na hatimaye akaelekea Endabsh hadi Karatu na kabla ya hapo alikuwa akitokea Dongobesh

Duuh! Mbulu tena.!? Yani mikoa mingine amesusa? Mie nilidhani kwama alipokuwa Kilimanjaro angeunganisha Tanga ,Zanzibar na Pemba..ama kweli nyumbani ni nyumbani.
Au ndio ile ya Chagua mtu na sio chama na kwa kuwa watu wa '' sampuli yetu'' hawako wengi kwenye sehemu ya kaskazini ile ya Tanzania
 
Thank you the Almighty God for listening to our plight.....we have suffered too much........we have endured unnecessarily too much..............now it is our turn to move on and turn the page into a new direction away from CCM cheaters.............................
 
Kwa mwendo huu DR. SLAA atavuna 90% ya kura zote za uchaguzi mwaka huu. Chama kilichokuwa kikidumu kimeufikia mwisho wake!
 
Hali ya CCM ni mbaya sana jimbo,
Marmo hajitokezi kabisa hadharani.

Kesho naenda kijijini haydom, nicheki upepo wa kisiasa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom