Elections 2010 Dr. Slaa aongoza kwa 73% - CACT

Shyt did they say this??? Yaani kama proffessional org. inaongea hivyo mbona safari ni ndeefu!

halafu that fake Dr Bana, kafanana na jina lake yupo kama kabanwa koo or like smbody in toilet, jina lake bana kama kabanwa na haja kubwa vile, hata his face unaonyesha alivyo muongo hawana lolote
 
Huenda this time Kamati Kuu ikatangaza rasmi kuwa REDET ni moja ya jumuia zake kama vile Wazazi, UVCCM, JUWATA, UWT....Aahahah ....aahaha Juwata ilishakufa baada ya mfumo wa vyama vingi.
 
embu tuelezane ukweli jamani...
REDET=Real Enemy of DEmocracy in Tanzania au??
 
REDET:
-Ninaiona kama taasisi inayopinga demokrasia
-Ninaiona kama taasisi inayotaka kuipeleka nchi katika mgogoro wa kisiasa ambao siku zote hugharimu maisha ya watu
 
1.KULINGANA NA ONLINE POLLS ZA RADIO FREE AFRICA,,HAYA NDIYO MATOKEO MPAKA SASA:

Nani kati ya hawa utamchagua kuwa rais wako?

  • Dr. Slaa (90%, 138 Votes)
  • Jakaya Kkiwete (6%, 10 Votes)
  • Prof. Lipumba (3%, 5 Votes)
  • Hashimu Lungwe (1%, 1 Votes)
  • Mutamwega (0%, 0 Votes)
Total Voters: 154
SOURCE: www.radiofreeafricatz.com/polls archieve



2.KULINGANA NA MWANAHALISI ONLINE POLLS:

Mgombea yupi utampa kura yako ya Urais 2010?
Jakaya Kikwete
7%

Willbrod Slaa
87%

Ibrahim Lipumba
4%

Mutamwega Mugahywa
0%

Hashim Rungwe
0%

Paul Kyara
0%

Christopher Mtikila
0%

Peter Kuga Mziray
1%

Total votes: 2313

SOURCE: Polls | Gazeti la MwanaHalisi


3.KULINGANA NA CACT(taasisi ya kiraia inajishughulisha na mambo mbalimbali ya kijamii na utafiti yenye makao yake makuu mwanza),,utafiti huu umefanya kwa njia ya kielectroniki yaani kwa kutumia simu na barua pepe,,umefanyika maeneo yote tanzania,,na matokeo yakawa kama ifuatavyo:

jakaya kikwete(CCM)-18%

Dr wilbrod slaa(CHADEMA)-73%

wengineo-9%

SOURCE:startv habari tarehe 09/10/2010 saa 2 usiku.


KULINGANA NA JAMII FORUMS:

Nani anafaa kuwa Rais wa Tanzania 2010-2015?


Voters 8978.
  • Jakaya Mrisho Kikwete (CCM)
    1,889 21.04%
  • Willibrod Slaa (CHADEMA)
    6,223 69.31%
  • Ibrahim Lipumba (CUF)
    261 2.91%
  • Hashim Rungwe (NCCR-Mageuzi)
    484 5.39%
  • Mutamwega Mugahywa (TLP)
    121 1.35%
SOURCE:https://www.jamiiforums.com/

NAKUOMBA SASA MWANA JF MWENZANGU ULINGANISHE HIZO HAPO JUU NA HII HAPA CHINI:

KULINGANA NA REDET:

Jakaya mrisho kikwete-71.2%

dr wilbrod slaa-12.3%

profesa lipumba-10.1%

wengineo-6.4%

SOURCE:Redet: Kikwete aongoza kura za maoni

FANYA ULINGANIFU YAKINIFU NA UTOE MAONI YAKO KUHUSU HILI.
 
Unajua REDET walichokifanya wanajua wenyewe na ndo maana ata CCM sijawaona kushadadia ayo matokeo
 
Inawezekana Redet walijisahau wakasoma matokeo KINYUMENYUME. Matokeo halisi yalipaswa kuwa Slaa; 68%, Kikwete; 12%, Lipumba; 10%, Waliobaki 10%.

Sasa hiyo ni kinyumenyume ama kuanza kati halafu kwenda kushoto halafu kwenda kulia? Mara nyingi akili yenyewe ikiwa imekaa "kinyumenyume" ndiyo unaweza ikaona mambo kinyumenyume. Kwenye Physics hii wanaitwa "reference point"! Teh teh teh! :A S 13:
 
Nilikua nasikiliza taarifa asubuhi hii kutoka Radio Free Africa, nimeshtushwa na taarifa ya mtu aliyejitambulisha kua ni mkurugenzi wa taasisi inayojishughulisha na utafiti (CACT) kama wa REDET) akiipinga report ya REDET kwa kusema taasisi yao nayo inaendelea na utafiti huo kwa njia mbalimbali, sms, emails, kuhoji moja kwa moja, etc nchi nzima.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo hadi sasa Dr. Slaa anaongoza kwa 73%, JK 12% na Lipumba 9%. Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo anapinga kitendo cha REDET kuchagua baadhi ya mikoa na kuacha mikoa mingine especially kanda ya Ziwa ambako ndio kuna wapiga kura wengi na anapinga report yenye only 2600 samples.

Siifahamu kampuni hii (CACT), wanaJF mwenye taarifa zaidi atuhabarishe

kwa hiyo matokeo haya ndio tuyaamini?? Acha kuwa na mawazo mgando kaka..amka sasa, usishabikie siasa kama mpira
 
halafu that fake Dr Bana, kafanana na jina lake yupo kama kabanwa koo or like smbody in toilet, jina lake bana kama kabanwa na haja kubwa vile, hata his face unaonyesha alivyo muongo hawana lolote

Jokes za shule ya msingi... Easy kama ndizi, banana ndizi... Childish mwanzo mpaka mwisho! :tonguez:
 
Peronally nimeipenda report ya REDET ili CCM wawe na confidence then ghafla wakianguka wasipate pa kutokea
 
Nimeona mambo mawili makubwa hapo
Mosi: kunatofauti kubwa kati ya tafiti za kisayansi zilizo endeshwa na wasomi na polls za media zinazo wezesha mtu kupiga kura hata mara 1000
Kenda:..................................
 
Taarifa ya REDET inaweza kuwa sahihi kabisa inategemea umemwoji nani? cha msingi hapa ni sampling.
ktk hawa watu 2600 ni lazima kuna wenye na wasio na vyama.

Kwahiyo ktk ripoti yao ilibidi waonyeshe ktk waliowaoji ni wangapi wana ccm, wangapi wapinzani na la msingi wangapi kati ya hao 2600 hawana vyama. Hawa ni muhimu kwa maana ndio hasa wanaochagua Rais kwa maana watanzania wengi hawana vyama.

Kwa Tanzania kama sample yako haina asilimia 30, aslimia 20 wapinzani na asimilia 50 ambao hawana
vyama. Basi utafiti au survey yako nzima haina maana kwa maana it does not reflect reality.

Acha kuwatetea. Kama walifanya utafiti, na walitumia vigezo vyote vya utafiti walitakiwa wafanye sampling inayokubalika katika fani ya kitafiti. kama hawakufuata utaratibu unaopaswa kufuatwa katika utafiti basi walikuwa wanafanya utafiti unaowafikisha kwenye majibu ambayo wanayataka na tayari walikuwa nayo. Ni ujinga kutaka kujua Watanzania wangapi wanataka kumchagua mgombea wa Chama gani na wewe unkwenda kuhoji wanachama wa chama hicho kama sample pekee. Huo si utafiti ni usanii?
 
paulss, kumbuka watakopiga kura trh 31Oktoba ni hao unaowaita si wasomi kwani ndiyo walio wengi na nafasi waliyoipata kueleza msimamo wao ni kwenye hizo media unazozidharau.
 
Back
Top Bottom