Kimilidzo
JF-Expert Member
- Jan 3, 2011
- 1,346
- 613
Mkombozi wa watanzania Dr Wilbroad Slaa alihamia Chadema akitokea CCM. Wakati yuko CCM hatukuwahi kusikia kuwa huyu jamaa ni Padri na ataifanya nchi kuwa ya kikristo. Na hata CCM walipomchakachua ubunge mwaka 95 hawakusema kuwa sababu ni kupiga kampeni za kidini au katumwa na baraza la maaskofu Tanzania. Iweje leo Dr huyuhuyu kwa kuwa yuko chama kingine watu wa CCM na JK wao wanaeneza propaganda kuwa ni mdini, katumwa na maaskofu, mbona wakati yuko kwenu hamkusema chama chenu ni cha kikristo??? Au ndio siasa mlizoanzisha za kulialia kwa wananchi mara udini mara nchi haitawaliki, mara JK hawezi kuleta mvua... Tuachieni Dr Slaa wetu afanye siasa kwa amani, afungue matawi ya CDM kila kijiji kwa maandalizi ya ushindi 2015