Dr Slaa alipokuwa CCM

Kimilidzo

JF-Expert Member
Jan 3, 2011
1,346
613
Mkombozi wa watanzania Dr Wilbroad Slaa alihamia Chadema akitokea CCM. Wakati yuko CCM hatukuwahi kusikia kuwa huyu jamaa ni Padri na ataifanya nchi kuwa ya kikristo. Na hata CCM walipomchakachua ubunge mwaka 95 hawakusema kuwa sababu ni kupiga kampeni za kidini au katumwa na baraza la maaskofu Tanzania. Iweje leo Dr huyuhuyu kwa kuwa yuko chama kingine watu wa CCM na JK wao wanaeneza propaganda kuwa ni mdini, katumwa na maaskofu, mbona wakati yuko kwenu hamkusema chama chenu ni cha kikristo??? Au ndio siasa mlizoanzisha za kulialia kwa wananchi mara udini mara nchi haitawaliki, mara JK hawezi kuleta mvua... Tuachieni Dr Slaa wetu afanye siasa kwa amani, afungue matawi ya CDM kila kijiji kwa maandalizi ya ushindi 2015
 
waache wabwabwaje hao madomo kaya (ccm) ndo kawaida yao kwa kila wanaomwona adui wa itikadi zao za kfisadi,,! wiseman says ''Never try to teach a shwyne (pig) to sing a melodic tune it waste your time and annoy the pig'' Ananias' 1999
 
interesting! wazuie wasiseme! hiyo ndiyo siasa au si-hasa kulialia hakusaidii toa mawazo CDM ifanye nini.
 
hakuna watu walionikera kama viongozi wa CCM.wameonyesha udhaifu mkubwa katika uongozi kwa kutokuwa makini katika utendaji wao.zipo mbinu za kuudhofisha upinzani na siyo kupagawa na maneno yanayoonekana si kweli. propaganda za
 
waache wabwabwaje hao madomo kaya (ccm) ndo kawaida yao kwa kila wanaomwona adui wa itikadi zao za kfisadi,,! wiseman says ''Never try to teach a shwyne (pig) to sing a melodic tune it waste your time and annoy the pig'' Ananias' 1999

Kwa jinsi hali ilivyo ngumu kimaisha tunayo haki ya kufananisha CCM na nguruwe... Shwyne...
 
Mkuu ccm inachukiwa Mwanza usipime. Nimepata taarifa kwamba siku ya kufunga kampeni mh. Lau MASHA akiwa eneo la Bugarika alipanda on the stage wananchi wakamzomea, akalia kwa uchungu akauliza "jamani nimewakosea nini? Naomba mnisamehe kama kuna kitu nimewakosea" watu wakazomea zaidi mh. Akashindwa kuomba kura akasema "basi jamani naomba mchague Jakaya kikwete" akashuka on the stage huku akifuta machozi. Huyu jamaa sijui aliwakose nini watu Nyamagana lakini mi nafikili hii ilitokana sumu zilitemwa na Dr wa uhakika Slaa na kuwafanya wakazi wa Mwanza kuichukia Ccm, hali iliyopelekea kijana Hayness mp Ilemela kuchukua kiti kiulaini wakati hakupiga kampeni za kutosha jimboni mwake. Kwa hiyo Ccm lazima wamchukie Slaa anawapa adha kubwa sana mbele ya wtz, na asipoangalia wanaweza kumpoteza kwa gharama yoyote.
 
Kwani nini kilimtoa kanisani/madhabahuni na kukimbilia siasa? Je alifukuzwa huko kanisani? Na kama alifukuzwa kuna mwenye data ni kwanini? Au ni kiu tu ya kuwa RAIS? Au kuna zaidi ya hilo? Je kondoo wa Bwana walimshinda na sasa anataka awachunge watanzania? Na alipokuwa CCM alitetea au kusimamia msimamo huu huu alionao au? maana hatukumsikia wakati ule.
 
Kwani nini kilimtoa kanisani/madhabahuni na kukimbilia siasa? Je alifukuzwa huko kanisani? Na kama alifukuzwa kuna mwenye data ni kwanini? Au ni kiu tu ya kuwa RAIS? Au kuna zaidi ya hilo? Je kondoo wa Bwana walimshinda na sasa anataka awachunge watanzania? Na alipokuwa CCM alitetea au kusimamia msimamo huu huu alionao au? maana hatukumsikia wakati ule.

Dr. Slaa (PhD) aliamua kuacha upadri-kazi ya kuwaongoza watu kiroho na kuhamia kwenye siasa kwa sababu demokrasia iliyoko huko kanisani kwake ilimruhusu kufanya maamuzi na kuacha upadri na kuhamia kwenye siasa. Pili aliamua kuja kwenye siasa ili kuwakomboa watu kwani alishaona mapungufu na unyonyaji unaofanywa na viongozi wa wakati huo.

Kwa bahati mbaya alipoingia CCM akakuta misingi, nguzo, maadili na miiko ya uongozi iliisha kiukwa na kuvunjwa. Ndo akagundua huwezi kuwa mpiganaji ukiwa ndani ya CCM huwa kuwakomboa watanzania wanaokandamizwa, wanaonyonywa na CCM yenyewe.

Ndo akaendeleza demokrasia yake ya uchaguzi na kuchagua chama mdala ambacho sera zake zinanendana na ukombozi wa watanzania na ndipo akahamia CHADEMA.

Viva Slaa, Viva Chadema, Viva Peoooooooooooooooooooooooples poweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeer..........................
 
..tumeshapata kuwa na Mashekhe wabunge, mfano: Shekhe.Professor.Mikidadi.

..pia tumewahi kuwa na wabunge Mapadri, mfano: Yohana Misigila , wa Tabora mjini.

..Dr.Slaa aliwahi mwanachama na kiongozi wa CCM alipokuwa Rome, Italy.

..sioni sababu ya kumsakama mwanasiasa yoyote ile kutokana na imani yake.

..mbona sisi wengine tuna imani zetu na bado tunashiriki siasa?


Salimia said:
Kwani nini kilimtoa kanisani/madhabahuni na kukimbilia siasa? Je alifukuzwa huko kanisani? Na kama alifukuzwa kuna mwenye data ni kwanini? Au ni kiu tu ya kuwa RAIS? Au kuna zaidi ya hilo? Je kondoo wa Bwana walimshinda na sasa anataka awachunge watanzania? Na alipokuwa CCM alitetea au kusimamia msimamo huu huu alionao au? maana hatukumsikia wakati ule.

Salimia,

..Dr.Slaa ni mwanachama wa JF. haya maswali yako alishayajibu yeye mwenyewe zaidi ya mara moja.

..hakuna haja ya kusubiri kusimuliwa alichokisema wewe tafuta majibu ya Dr utayapata.

..Dr.Slaa aligombea ubunge wa Karatu kwa tiketi ya CCM baada ya kuombwa na wananchi wenzake waliokuwa wamechoshwa na mbunge wa wakati huo.

..Dr.Slaa alishinda kura ya maoni, lakini jina lake likakatwa na Kamati Kuu ya CCM, na badala yake wakamsimamisha Patrick Qorro aliyekuwa amechokwa na wananchi.

..baada ya matukio hayo ndiyo Dr.Slaa akajiunga na Chadema.
 
....hakuna haja ya kusubiri kusimuliwa alichokisema wewe tafuta majibu ya Dr utayapata..

Kwa nini usiweke link hapa mkuu JokaKuu? kwanini wewe una majibu ya kueleweka na huna matusi kama wenzako?
 
Sababu zipi walitoa CCM za Slaa "kuchakachuliwa" kwenye ubunge 1995?

Halmashauri kuu ilgundua udhaifu wake kwa wanawake ndio maana ikalikata jina lake ili asije kukiabisha chama kama alivyofanya kule CDM.
 
Mti mwenye matunda ndio unapigwa mawe . hivyo Hongera sana Dr.Slaa na pia Mungu akutangulie
 
Halmashauri kuu ilgundua udhaifu wake kwa wanawake ndio maana ikalikata jina lake ili asije kukiabisha chama kama alivyofanya kule CDM.
huoni kama wao ndio walichemsha,kwani tangu hapo hawajawahi shinda katika jimbo hilo
 
Halmashauri kuu ilgundua udhaifu wake kwa wanawake ndio maana ikalikata jina lake ili asije kukiabisha chama kama alivyofanya kule CDM.

Nduka
Usituletee porojo za CCM hapa.

Kama ni udhaifu wa WANAWAKE BASI KAMATI KUU WANGELIANZA NA KIWETE MWENYEWE HALAFU BAADAYE MSHAMBAA MAKAMBA!

 
Nduka
Usituletee porojo za CCM hapa.

Kama ni udhaifu wa WANAWAKE BASI KAMATI KUU WANGELIANZA NA KIWETE MWENYEWE HALAFU BAADAYE MSHAMBAA MAKAMBA!


Kama unaushahidi wa JK au Makamba kufanya mambo yanayoishushia CCM heshima weka hapa, au unatumia 'utafiti' dr slaa kuwa makamba alibaka kigoma lakini hatujawahi kujua jina la aliyebakwa wala hakuna ushahidi zaidi ya umbeya tu kama kifo cha rc.
 
Back
Top Bottom