Dr. Slaa akosoa uharibifu wa nyavu za uvuvi haramu ulinaofanywa na Magufuli

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,174
Alipokuwa kwenye kampeni zake katika kanda ya Ziwa, Dr. Slaa alionyesha kukerwa na mkakati wa Dr. Magufuli - Waziri wa uvuvi na ufugaji - katika kupambana na uvuvi haramu.

Kwa Dr. Magufuli ni kuharibu nyavu za uvuvi haramu ambazo yasadikiwa zinavua samaki wachanga na ambazo husababisha kupungua kwa kasi ya kukua kwa uzao wa samaki. Hivyo, kuwaharibia nyavu wavuvi hao Dr. Magufuli anaamini ya kuwa kwanza anawaongezea gharama za uvuvi haramu wahusika hao na pili analinda uzao wa samaki hao kutovunwa au kubakwa mapema mno kwa vichanga hivyo..

Kwa Dr. Slaa kitendo cha kuchoma nyavu ni uchafuzi wa mazingira. Nyavu zingeliweza kurudishwa kiwandani na kutengenezwa upya badala ya kuchomwa kwa nyavu hizo. Lakini kubwa zaidi mbona hao wakubwa wenye hivyo viwanda au wasafirishaji na wauzaji wa hizo nyavu zinazokamata samaki wachanga hawathibitiwi?

Sasa inakuwaje mvuvi ambaye ana kipato kidogo aumizwe na hatua za serikali wakati yule aliyemsababishia madhara hayo anaachwa aendelee na biashara yake hiyo haramu?

Haya ni maswali ya kimsingi kabisa na ndiyo maana vita dhidi ya uvuvi haramu havina mafanikio kwa sababu vita hivyo havitafuti kumaliza kiini cha tatizo ila kumjenga Mheshimiwa Magufuli ili aonekane machoni pa watanzania kuwa anachapakazi lakini ukweli ni kuwa anatwanga maji kwenye kinu.............
 
Alipokuwa kwenye kampeni zake katika kanda ya Ziwa, Dr. Slaa alionyesha kukerwa na mkakati wa Dr. Magufuli - Waziri wa uvuvi na ufugaji - katika kupambana na uvuvi haramu.

Kwa Dr. Magufuli ni kuharibu nyavu za uvuvi haramu ambazo yasadikiwa zinavua samaki wachanga na ambazo husababisha kupungua kwa kasi ya kukua kwa uzao wa samaki. Hivyo, kuwaharibia nyavu wavuvi hao Dr. Magufuli anaamini ya kuwa kwanza anawaongezea gharama za uvuvi haramu wahusika hao na pili analinda uzao wa samaki hao kutovunwa au kubakwa mapema mno kwa vichanga hivyo..

Kwa Dr. Slaa kitendo cha kuchoma nyavu ni uchafuzi wa mazingira. Nyavu zingeliweza kurudishwa kiwandani na kutengenezwa upya badala ya kuchomwa kwa nyavu hizo. Lakini kubwa zaidi mbona hao wakubwa wenye hivyo viwanda au wasafirishaji na wauzaji wa hizo nyavu zinazokamata samaki wachanga hawathibitiwi?

Sasa inakuwaje mvuvi ambaye ana kipato kidogo aumizwe na hatua za serikali wakati yule aliyemsababishia madhara hayo anaachwa aendelee na biashara yake hiyo haramu?

Haya ni maswali ya kimsingi kabisa na ndiyo maana vita dhidi ya uvuvi haramu havina mafanikio kwa sababu vita hivyo havitafuti kumaliza kiini cha tatizo ila kumjenga Mheshimiwa Magufuli ili aonekane machoni pa watanzania kuwa anachapakazi lakini ukweli ni kuwa anatwanga maji kwenye kinu.............

Nakubaliana na Mzee Slaa kwenye mada hii. Na Mzee Magufuli nadhani ajitahidi kuwadhibiti hao wanyonya damu wa soko huria. Sheria ni Msumeno. Soko huria bila sheria bora turudi tuliko kua. tafadhalini wakuu. looo!
 
hana lolote mbona hoja ni dhaifu sana


magufuli alitembelea hadi maduka yenye kuuza nyavu na kutoa angalizo la kushughulikiwa

ila anapaswa ajue ktk utekelezaji wa jambo kuna vyombo vingi na ngazi nyingi zinahusika

mropokwaji ambae yeye kila kitu lazima akisemee hata kile asichokijua unajiangusha sio kujishusha
 
hana lolote mbona hoja ni dhaifu sana


magufuli alitembelea hadi maduka yenye kuuza nyavu na kutoa angalizo la kushughulikiwa

ila anapaswa ajue ktk utekelezaji wa jambo kuna vyombo vingi na ngazi nyingi zinahusika

mropokwaji ambae yeye kila kitu lazima akisemee hata kile asichokijua unajiangusha sio kujishusha
ok sasa tuambie wewe hoja yako nini? ungekuwa wewe ungefanya nini, ungewafuatilia hao wanaotengeneza nyavu au ungeenda kuharibu nyavu za hao watu ambao hata hawaelewi impact ya hizo nyavu wanazouziwa? acha negative zako zisizo na msingi wowote. Ukitaka kupambana na matatizo hayo lazima uende kwenye root of the cause, lazima uhakikishe kuwa wattengenezaji wa hizo nyavu wanaeleimishwa au wanadhinitiwa and then uende kuwaaelimisha watumiaji.

Achana na ushabiki usio na tija yoyote
 
hana lolote mbona hoja ni dhaifu sana


magufuli alitembelea hadi maduka yenye kuuza nyavu na kutoa angalizo la kushughulikiwa

ila anapaswa ajue ktk utekelezaji wa jambo kuna vyombo vingi na ngazi nyingi zinahusika

mropokwaji ambae yeye kila kitu lazima akisemee hata kile asichokijua unajiangusha sio kujishusha

Sio lazima kila hoja uchangie na negative views zako.Mropokaji ni wewe ambaye whatever concerns Dr Slaa argument lazima ukurupuke tu.
 
Back
Top Bottom