DR Slaa aeleza sababu ya CHADEMA kususa

Chenye matatizo hapa ni Katiba. Kama sheria ya nchi inatafsiriwa kuwa Tume ya Uchaguzi ikiishatangaza mshindi hakuna atakayeweza kuhoji matokeo yake, tunapoteza muda kumtafuta Makame & Kiravu Co. Ltd. Jamani, basi sheria ingetupa mwanya hata kuwaburuza hawa akina Makame kwa Pilato walau watimuliwe kazi zao.
Suala zima la kujumuisha kura lilienda kombo. Sidhani hio "program" wanayosema ilisababisha kompyuta ku-crash ni kweli. Jamani, kura hizo zinaingizwa kwenye spreadsheet, sasa watuambie walikuwa wanatumia programu ipi? Ingekuwa tunapiga kura kwenye kompyuta ningeweza kukubali kidogo kisingizio cha ku-crash. Nafikiri wanatudanganya wanafikiri watanzania hatujui kompyuta inavyofanya kazi.
Dr. Slaa tunakuomba uweke ushahidi wako wote hadharani na kopi zake uwape nchi marafiki na wahisani wajue pesa wanazotupa tunazitumia vipi.
Huu ni wakati wa kuambiana ukweli na wala sio wakubaki nyuma na kulalama. Dr. Slaa inabidi uelewe kuwa hata yale yalioitwa matokeo rasmi waliyoyatangaza haya-kubalance. Yaani namba za kujumlisha na kugawanya kuweka asilimia, ziligoma.
Kama huwezi kuvipeleka Mahakamani, tumwagie hapa vielelezo vyako vyote, na sisi tutakuwa Mahakama .
 
Wadau, JK kwa sasa anakanganywa na mengi, habari kutoka jikoni zinapasha kuwa ukiacha ule mkanganyiko wa Sitta kumgomea uwaziri (ingawa sasa naye inasemekana kashauriwa kama njia ya kumpa nguvu ya kupambana kusaidia kundi la haki kwa mwaka 2015 akubali uteuzi na atake wizara nyeti), imepashwa kuwa Lowassa amekuwa akimshinikiza 'msela' wake apate ama yeye binafsi au watu wake muhimu moja au zote katika wizara hizi nyeti ktk kujijenga kwa 2015.

Mambo ya Nje:Kujijenga kimataifa na kufahamika kwa wanadiplomasia
Mambo ya Ndani:Hii itampa fursa ya kufanya fitna nchi nzima kwa kisingizio cha kuzunguka kuangalia usalama wa raia etc.
Tamisemi:Huku Halmashauri, majiji na mitaa viko chini yake so madc na maRC wato watakuwa upande wao.
Miundombinu:Huku kuna uwekezaji mpana sana so kuna fedha zinazoweza kufanyiwa EPA zikaingizwa kwenye kampeni za kujiandaa, kununua wanamtandao wapya na kuwarejesha wa zamani walioparaganyika. Huu ndio mkakati wa Lowassa et al, wapambanaji kina Mwakyembe, Manyanya, Membe wanafanya nini, au ndio kina Manyanya wamerudi kundini kama CUF (rejea maswali ya Manyanya na Ole Sendeka Bungeni karibuni).

Hii Jamii forums imegeuka imekua Global Publisher siku hizi. Wewe inakuhusu nini?? fanya mabadiliko hapo ulipo, unapoishi, kwa wanaokuzunguka na kikubwa zaidi changes zinaanzia kwako. Hao wa-CCM kama huwapendi acha umbea na kufatilia mambo yao. Grow Up
 
Habari ni nzuri sana. Na ni kama wengine wote watakavyokuwa wamehisi kukasirishwa na Prof. Wamba. Nimekosa la kusema ila siyo kwamba limekosekana bali litatoka neno baya tuu.... kwahiyo. Mungu ibariki Tanzania ni bora zidi!


Mnashangaa nini? wamba dia wamba si MTANZANIA, angesema kinyume angechapa mwendo tena fasta, unadhani hajupendi.
 
(3) Bunge laweza kutunga sheria inayoweka masharti yatakayohakikisha kuwa vyama vya siasa vinazingatia mipaka na vigezo vilivyowekwa na masharti ya ibara ndogo ya (2) kuhusu
uhuru na haki ya watu kushirikiana na kujumuika.


Nawakilisha

Can you really reason out or you are just there.......among the ******...........................or among the dunces of this nation?
 
Sina uhakika. tetesi au????? NAELEWA NCHI INAONGOZWA NA SIIII KIKWETE. YEYE YUKO KAMA NEMBEO. LAKINI HAYA???????
 
Upande wng nawaunga mkono chadema kwn msg waliyokusudia imewafikia ccm kikamilifu na nadhani watajaribu kujirekebisha ama sivyo wawe tayari kupoteza majimbo zaidi na hatimaye kuondolewa madarakani!
 
Ni watu wachache sana wenye MOYO wa kuchukua RISK ili wenzao wapate mafanikio. Japo wale ambao watu wamechukua RISK kwa ajili yao hata hawaelewi kwa nini wenzao wamejitotea kubeba mzigo mkubwa wa Lawama! Nnachosema hapa ni kwamba Wabunge wetu wamechukua RISK sana kutetea maslahi yetu kwa kudai mfumo urekebishwe...Bali nashangaa sana watanzania ambao wanawalaumu wabunge wetu wakati wameamua kubeba MSALABA kwa ajili yetu. Nashangaa kuona vijana wa UDOM ambao nilitegemea wana upeo mkubwa wa kuelewa mambo lakini haohao ndio wa kwanza kutoa tamko la kulaani uamzi wa wabunge wetu....Siwashangai kwani ni hao hao waliojikomba kumchangia KIKWETE zaidi ya milioni moja ili achukue fomu za kugombea urais. Wanajipendekeza tu wakisahau kuwa bibi na baba zao waliowaacha kwenye nyumba za udongo,makuti,majani na matobo kibao huko vijijini katika karne hii imetokana na udhalimu wa CCM na kushindwa kusimamia rasilimali kwa usawa toka enzi za uhuru! Sijui wanapita angani kwenda chuoni kwani wangeona vijumba vya mbavu za mbwa humo singida,dodoma vijijini au kati ya dodoma na moogoro....vijumba ambavyo havikustahili kuonekana Tanzania katika karne hii sijui kama wangeisupport CCM.
Kimsingi nawapongeza sana wabunge wangu..wamefanya SUALA la kishujaa....Hakuna haja ya kususia posho kama wanavyobeza wana CCM kwani mimi nakatwa zaidi ya Laki 5 kama kodi katika kamshahara kangu kadogo.....Nipende nisipende! na kodi hiyo ni lazima utumiwe na Mbunge wangu kunitetea
CCM inafahamu kuwa WATANZANIA ni WAOGA.. Inacheza na UOGA wao kwa kueneza Propaganda kuwa CHADEMA wataleta Vita. Hawajui kuwa vita nyingi hutokana na watu kushindwa kuvumilia udhalimu na wakaamua kuingia msituni hata wasipopata msukumo wa Chama chochote.
CCM inafumbia Macho ukweli kuwa KIKWETE na viongozi wengine wamewahi KUTUPIWA MAWE na Wananchi. Kikwete amewahi KUZOMEWA..CCM ikakaa kimya! Leo wabunge wetu kugoma kumsikiliza rais wa NEC na CCM ati ni utovu wa Nidhamu...ati waadhibiwe kwa hoja ya kufukuzwa Bungeni! Mbona hawakuja na Hoja ya Kuwafukuza wananchi humu nchini pale walipomzomea na kumtupia Mawe KIKWETE? Mbona hawakuja na HOJA ya kumfukuza yule aliyetia Maji katika mafuta ya Gari la Kikwete huko Ziarani Arusha?
CCM wameishiwa sera......wamebakiza sera moja tu...Ya kueneza propaganda na kucheza na hofu ya Watanzania.
Tunawahitaji wabunge wachache tu kama hawa wa kwetu ili kuleta Mabadiliko.
 
From Dr Slaa FACEBOOK PAGE

Link: Dr. Wilbrod Slaa | Facebook

Wabunge wetu wamechukua uamuzi mgumu sana, uamuzi ambao unataka ujasiri na uthubutu wa vitendo. Ni lazima tuelewe kuwa mgogoro uliopo siyo na Kikwete kama Kikwete, la hasha bali na mfumo uliomuingiza madarakani safari hii, mfumo ambao tunautuhumu kuwa haukuwa huru na wa haki. Uamuzi huu haukuwa wa chuki binafsi au kisirani dhidi ya Kikwete kama Kikwete, bali dhidi ya mfumo ulioundwa na kulelewa na CCM na ambao umetuonesha kuwa hauwezi na haupaswi kulelewa kwa muda mwingine wowote ujao.



Kuanzia wakati wa kutangaza matokeo tulitoa malalamiko yetu kwa Tume ya Uchaguzi ili waweze kuyafanyia kazi ili mshindi apatikane katika mazingira ya haki na uwazi. Tume haikusikiliza na ikaendelea na mfumo wake mbovu wa kutangaza matokeo bila kujali malalamiko yetu. Tukazungumza hadharani juu ya kutopatana kwa matokeo ya uchaguzi yanayotangazwa na tume na yale yaliyoko majimboni na kuomba tume wasitishe ili waangalie ushahidi tulio nao, tume haikusikiliza na matokeo yake wakamtangaza Kikwete kuwa Rais licha ya kwamba matokeo majimboni yalikuwa yanaashiria vinginevyo.





Ni muhimu kutambua kuwa ni rahisi kukubali matokeo ya Ubunge kwa sababu yanarasimishwa majimboni na yanaweza kupingwa mahakamani. Katika urais kimsingi ukiangalia Katiba utaona kuwa haijalishi nani kashinda kwenye kura, bali nani katangazwa mshindi. Tunachotuhumu sisi ni kuwa matokeo ya Uchaguzi yangetangazwa kama ilivyoahidiwa na Tume mwezi Machi yangeonesha wazi mshindi ni tofauti na yule aliyetangazwa. Lakini wao tume wakijua kuwa mara wakishatangaza hakuna mahakama inayoweza kuhoji wakafanya hila na haraka ya kutangaza matokeo ya Urais kwa kumtangaza Kikwete kuwa ni Rais.



Kama toka siku ya kwanza tulitoa malalamiko na zikapita siku tano bila kujibiwa wala kusikilizwa na baadaye tunatakiwa tukubali tu kwa vile "keshatangazwa" katika dhamira safi tunaweza vipi kufanya hivyo? Ugomvi wetu wa kisiasa (na siyo chuki wala uhasama binafsi) hauko zaidi na Kikwete bali natume iliyomtangaza. Na kwa vile yeye mwenyewe haoni matatizo katika tume au mfumo wetu wa uchaguzi tunaona kuwa aidha alitoa baraka zake au alikubali kunufaishwa na mfumo huo mbovu.



Hivyo, wabunge wetu kutoka nje ni kutuma ishara mbili: Kwanza, tunapinga mfumo wa kichakachuaji wa tume ya Uchaguzi uliomtangaza Kikwete kuwa Rais, na pili kwa vile Tume imeshindwa kutuonesha uwazi wa ushindi wa Kikwete tunashindwa kukubali kama ni mshindi halali. Ni mpaka pale uchunguzi huru wa kura utakapoonesha kuwa Kikwete kashinda kihalali ndipo tutakuwa tayari kumtambua ukiondoa uwezekano mwingine wa kuelewana.



Tukumbuke kuwa, kama uchaguzi huu ungeendeshwa katika hali ya uwazi, haki na ufanisi tusingefika hapa. CHADEMA siyo wa kulaumiwa katika hili wala wabunge wetu wasibebeshwe mzigo kwa hili; watu waliotufikisha hapa ni Serikali ya CCM na vyombo vyake ikiwemo Tume ya Uchaguzi. Wangeonesha weledi na kutokupendelea kwa wazi tusingefikia mahali pa kutulazimisha kuchukua hatua hizi ambazo kwa kila kipimo ni za wastani sana ukilinganisha na hatua ambazo tungeweza kuzichukua.



Nawasihi tuwaunge mkono wabunge wetu na uongozi wetu kwa kuwatia moyo kwani uamuzi waliouchukua ni uamuzi wa kijasiri lakini ulioweka historia katika Tanzania kuwa hatuwezi tena kusukumwa na kuburuzwa kwa kutumia nguvu ya taasisi au cheo cha mtu. Tuwatie shime na tusimame nao katika wakati huu wa kihistoria.



Pamoja tunaweza, mpaka kieleweke!

Dr. wa Theolojia naye anaongea pumba kabisa!!!!!!!! hii inaonesha hana nguvu ya maamuzi ndani ya chama. Naungana na Zitto Kabwe
 
Back
Top Bottom