Dr. Nchimbi je kutofautiana Bungeni (hata sio jeshini) ni utovu wa nidhamu?

babykailama

JF-Expert Member
Mar 5, 2012
251
243
Je ni kweli na ni halali kuwa pale Mh. Lugola, Mbunge na ‘Askari wa Akiba’ alipotofautiana na Waziri kwa kutaka posho ya chakula (lishe) iwe sawa kwa Maskari wote, Mh. Dr. Nchimbi (Waziri wa Mambo ya Ndani) akamjibu kwa kulieleza Bunge kuwa huo ni utovu wa nidhamu?

Fikra zangu:



Hata kama ingekuwa ni katika kutii amri, Je Nchimbi (Waziri) ndiye wa kumpa amri Lugola (Mbunge)? Mimi nafikiri ni karibu zaidi na kinyume chake yaani Bunge ndilo linaelekeza na kiuidhibiti Serikali!

Hata context ingekuwa ni jeshini; dhana ya kulazimisha Askari yeyote kutotofautiana kabisa kwa jambo lolote na Mkuu wake ni ya kukandamiza ubunifu na wakati mwingine haki?

Kinachozungumzwa Jeshini ni utii wa Sheria, Taratibu na Amri halali na si kuminya na kuzuia mawazo tofauti (diversity in thoughts)-chemchem ya maendeleo katika jamii yeyote.

Aidha pia sikubaliani na mtu anayeweza kuhalalisha jambo kama hili kuwa Waziri alikuwa anatania; maana Mbunge alikuwa hatanii bali alikuwa akisubiri jibu la swali makini linalotaka uwepo wa haki katika namna ya kuwa treat makamanda wetu wote. Tena, Katibu wa Bunge hatujasikia akituelekeza kipindi cha kuwasilisha utani Bungeni.


Dr. Nchimbi pata somo kwamba, diversity & differentiations cannot be construed as disharmony and impudence
 
Wala sioni haja ya kuwatetea Polisi, waachwe na kijiposho hicho hicho. Ni wezi, majambazi, waonevu, wabambika kesi na uchafu mwingi tu against wananchi. Halafu mjue hili sio Jeshi (Army) kama mnavyolazimisha liwe. Jeshi ni moja tu, JWTZ. Polisi ni Idara kwenye Wizara ya Mambo ya Ndani kama zilivyo Idara nyingine za Uhamiaji na Zimamoto. Zaidi unaweza kuitazama na kuilinganisha Idara hii ya Polisi kama genge la wahuni tu, kwasababu wanafanya uhuni kuanzia ngazi za juu hadi chini kabisa.
 
Halafu mjue hili sio Jeshi (Army) kama mnavyolazimisha liwe.

sawa, lakini huu ni msamiati wako mpya sisi tunajua kuwa linaitwa jeshi la Polisi. Pili bado naunga mkono kuwa swali lilitakiwa kujibiwa sawia na Waziri bila kujali utendaji mbovu au mzuri wa hilo jeshi la polisi.
Usituaminishe kuwa kwa vile Tanzania inafanya vibaya katika mambo mengi kati ya nchi nyingine duniani basi sote ni wabaya ukiwamo na wewe na hivyo hakuna haja ya mtu kuongelea haki za Watanzania ukiwamo na wewe!
 
Wala sioni haja ya kuwatetea Polisi, waachwe na kijiposho hicho hicho. Ni wezi, majambazi, waonevu, wabambika kesi na uchafu mwingi tu against wananchi. Halafu mjue hili sio Jeshi (Army) kama mnavyolazimisha liwe. Jeshi ni moja tu, JWTZ. Polisi ni Idara kwenye Wizara ya Mambo ya Ndani kama zilivyo Idara nyingine za Uhamiaji na Zimamoto. Zaidi unaweza kuitazama na kuilinganisha Idara hii ya Polisi kama genge la wahuni tu, kwasababu wanafanya uhuni kuanzia ngazi za juu hadi chini kabisa.

Ni kweli kabisa na umafia wao unaanzia kwa bosi wao mkuu kushuka chini
 
sawa, lakini huu ni msamiati wako mpya sisi tunajua kuwa linaitwa jeshi la Polisi. QUOTE]

Jishughulishe kidogo angalau kwa kuipata Sheria ya polisi (Police Ordinance) uone namna kikundi hicho kinavyoitwa kwa lugha ya Kiingereza ambako ndiko mlikotohoa sheria husika. Kwa kukusaidia tu, polisi wanaitwa Police Force. Sio Police Army. Sasa kwa tafsiri hii sidhani kama neno Force kiswahili chake ni Jeshi. Kama ndio unataka iwe hivi mbona tutakuwa majeshi mengi sana! Manake kule kule Polisi kuna FFU tena. Yaani Field Force, sijui nalo ni jeshi kwa mujibu wako!
 
Back
Top Bottom