Dkt. Mathayo na Ana Kilango: Same "Wachina" wa Tanzania mpaka "VILAZA" wa Kilimanjaro

Mkuu Nziku,

Unapotosha kabisa dhana ya mbunge kuleta maendeleo au kusukuma maendeleo kwenye jimbo lake.

Haina maana yeye ndiye anaamua nini cha kufanya au yeye ndio anatoa resources za kufanya hayo maendeleo yatokee.

Mbunge ndio kiongozi aliyechaguliwa na wananchi ili awasaidie kutatua matatizo yao. Sasa kama kuna shule mbovu, ni wajibu wa mbunge kuwakutanisha wadau wote na kuangalia namna ya kuongeza ubora.

Kama kuna mabomba yamejengwa na wafadhili, wameondoka na maji nayo yamehama nao, ni wajibu wa mbunge kuangalia kutafuta solution kwa kushirikiana na viongozi wengine wa wilaya pamoja wananchi. Kwanini wafadhili wakiondoka na maji yakauke?

Kama kilimo cha kawaha au mpunga kinaanguka, ni wajibu wa mbunge kupata majibu ya kitaalamu kupitia vyanzo mbalimbali na ikiwezekana ku mobilize resources iliyopo ili kusaidia kutatua tatizo.

Kwa mimi ningetaka mbunge wangu awe a troubleshooter na sio mropokaji tu. Awe na uwezo wa kuwakutanisha watu pamoja kwenye mambo ya maendeleo na sio mtu wa kuwagawa watu.

Aweze kuibana serikali kuu, aweze kuibana halmashauri ya wilaya kwa niaba ya wananchi wake ili watekeleze ahadi walizoahidi, ili miradi wanayoendesha iwe value for money nk.

Nimeshangaa kuona idadi kubwa ya wana JF wanafikiri kazi ya mbunge wa Tanzania ni kwenda kupiga kelele kule Dodoma. Eti kukusanya matatizo ya wananchi na kwenda kuyawakilisha bungeni, nonsense, wala hata huhitaji kusubiri bunge kuwakilisha matatizo yalipo. Kama umeona tatizo, ni hapo hapo kuanza kutafuta solution, kama haiwezekani wilayani, basi huko mkoani, huko wizarani, huko bungeni nk.

Wasanii wetu wengi hawafanyi kitu, anapiga kelele siku moja bungeni, kisha anarudi kwa wananchi na kuwaambia mmenisikia bungeni?

sijamaanisha Mbunge asifanye hayo unayosema, nasema kipaumbele cha kuwajibishwa kiwe kwa watendaji siyo Mbunge. Serikali ndiyo inayowajibika moja kwa moja kwa kuwa ndiyo iliyopewa resources na ndiyo yenye wataalam/watendaji.

Tatizo la huu mfumo mnaoutaka wa kumweka mbele mwanasiasa eti kwa kuwa amechaguliwa ndiyo utakaoendelea kutuletea matatizo. Nasema tunajenga Taifa la wanasiasa ni kwasababu tumeamua kustawisha hii dhana mbovu.

Mbunge atapenda short term plans, ili apate kitu cha kuwaonyesha au kuombea kura. Mbunge anapobeba maendeleo ya Halmashauri ina maana mahali popote atakuwa ndiye mwenyekauli kwani ndiye atakayeulizwa na wananchi au ndiye atakaye wajibika.

Ndiyo maana maamuzi mengi siku hizi yanashinikizwa kisiasa, yaani makatibu wakuu wa Wizara, Wakurugenzi wa Wilaya au Halmashauri wamekosa maamuzi na kuwasikiliza wanasiasa au wanatekeleza kwa kufuata interest za wanasiasa mojawapo Wabunge.

Ndiyo maana watalaam wanaacha kazi zao na kujiunga kwenye siasa. Tena mtendaji fulani akionekana anafanikiwa kazini anatafutiwa zengwe ili kumharibia kwa hofu tu kwamba atakuja kugombea ubunge.Tunajimaliza wenyewe, acha tuwape hiyo nafasi, miaka ijayo ndo tutajua.
 
Mkuu Nziku,

Unapotosha kabisa dhana ya mbunge kuleta maendeleo au kusukuma maendeleo kwenye jimbo lake.

Haina maana yeye ndiye anaamua nini cha kufanya au yeye ndio anatoa resources za kufanya hayo maendeleo yatokee.

Mbunge ndio kiongozi aliyechaguliwa na wananchi ili awasaidie kutatua matatizo yao. Sasa kama kuna shule mbovu, ni wajibu wa mbunge kuwakutanisha wadau wote na kuangalia namna ya kuongeza ubora.

Kama kuna mabomba yamejengwa na wafadhili, wameondoka na maji nayo yamehama nao, ni wajibu wa mbunge kuangalia kutafuta solution kwa kushirikiana na viongozi wengine wa wilaya pamoja wananchi. Kwanini wafadhili wakiondoka na maji yakauke?

Kama kilimo cha kawaha au mpunga kinaanguka, ni wajibu wa mbunge kupata majibu ya kitaalamu kupitia vyanzo mbalimbali na ikiwezekana ku mobilize resources iliyopo ili kusaidia kutatua tatizo.

Kwa mimi ningetaka mbunge wangu awe a troubleshooter na sio mropokaji tu. Awe na uwezo wa kuwakutanisha watu pamoja kwenye mambo ya maendeleo na sio mtu wa kuwagawa watu.

Aweze kuibana serikali kuu, aweze kuibana halmashauri ya wilaya kwa niaba ya wananchi wake ili watekeleze ahadi walizoahidi, ili miradi wanayoendesha iwe value for money nk.

Nimeshangaa kuona idadi kubwa ya wana JF wanafikiri kazi ya mbunge wa Tanzania ni kwenda kupiga kelele kule Dodoma. Eti kukusanya matatizo ya wananchi na kwenda kuyawakilisha bungeni, nonsense, wala hata huhitaji kusubiri bunge kuwakilisha matatizo yalipo. Kama umeona tatizo, ni hapo hapo kuanza kutafuta solution, kama haiwezekani wilayani, basi huko mkoani, huko wizarani, huko bungeni nk.

Wasanii wetu wengi hawafanyi kitu, anapiga kelele siku moja bungeni, kisha anarudi kwa wananchi na kuwaambia mmenisikia bungeni?


Kamsome Adam Smith kuhusu mgawanyo wa kazi. Kazi zinafanyika kwa ufanisi pale kila mtu anaposhughulikia kile alichopangiwa.

Hivyo kazi ya mbunge ni kuwakilisha na sio kazi za kiutendaji. Kuna watendaji waliopewa mamlaka na bajeti ya kufanya kazi zinazopigiwa kelele hapa, je hao wanafanya nini :confused:

Unapomtaka mbunge awe ofisa elimu au Mwalimu mkuu, hujatenda haki. Na hili ndio matatizo yanayo wakabili watanzania.
 
Swali la Kaizer ni la msingi.

Dhana hii ya kumwona Mbunge ndiye anayewajibika kwa maendeleo ya endeo lake ndiyo inayoturudisha nyuma kimaendeleo. Dhani hii inawatutumua Wabunge kujiona ndiyo wenyewe, wanayoyasema lazima yatekelezwe nk. Kibaya zaidi, ndiyo dhana inayolipeleka Taifa kwenye siasa zaidi kuliko utendaji.

Kimsingi, Mbunge ni mwananchi, ni mwakilishi wa wananchi katika maamuzi na kutunga sheria. Mbunge si Serikali, hana bajeti ya miradi ya maendeleo, hapokei kodi. Serikali ndiyo inayopokea kodi, ndiyo yenye bajeti. Ndiyo inayopaswa kutekeleza miradi ya maendeleo. Mbunge ni sawa na diwani katika kata na Halmashauri yake.

Kwa kuwa inadaiwa kuwa kodi zetu, pamoja na mapato mengine ya Serikali hayatoshelezi mahitaji ndipo suala la wananchi kuchangia ili kutekeleza miradi linakuja. Inapotokea suala la kushirikisha wananchi ndipo diwani na Mbunge wanapohitajika sana ili kupitisha maamuzi na kuwashawishi wananchi.

Msimamo wangu:
Mimi naomba hivi; tujenge tabia ya kuimarisha utendaji na watendaji. Tujenge tabia ya kuwafanya watendaji wawe wawajibikaji. Kazi ya diwani na wabunge iwe ni kusimamia Serikali kuu na serikali za Mitaa. Wanaopaswa kuwajibia wawe ni Serikali yaani watendaji.

Hofu yangu:
Tunapojenga mfumo au mtazamo 'Mbunge ndiye mleta maendeleo' tunakuwa tumemwinua sana kiasi cha kujiona yupo juu ya Serikali hali inayoweza kuathiri utekelezaji wa mipango ya maendeleo hasa ile ya muda mrefu. Mbunge atapenda mipango ya muda mfupi ili kuonyesha alichokifanya katika muda mfupi. Atafanya hivyo kwasababu anataka kura za ndiyo.

Hofu yangu ni kujenga Taifa la wanasiasa. Wanasiasa hawajengi nchi, wanaojenga nchi ni watendaji. Tunapokuwa na Taifa lililojaa wanasiasa, kitakachopewa kipaumbele ni michezo ya kisiasa badala ya kutafuta teknolojia na kutekeleza masuala ya maendeleo.

Kwa mfano Mkuu bangusilo anatoa hoja kuwa Mama Anne Malecela (MB) hafai kuwa Mbunge kwa kuwa kidato cha nne wamefeli mitihani. This is redicolous! Hapa Mbunge kama mwananchi, alaumiwe katika jambo ambalo hakulitekeleza.

Hoja ambayo ingeleta msingi, ilitakiwa kuwa, kwa mfano: walimu katika shule hizo hawapo/hawatoshi na katika bajeti kulikuwa na code ya kuajiri walimu, Serikali haikuajiri na Mbunge hajaihoji Serikali. au kulikuwa na tatizo la vitabu shuleni, serikali ilipendekeza vununuliwe lakini madiwani/Mbunge walikataa kupitisha bajeti ya kununua vitabu. nk,

Hoja za namna hii, ndiyo zenye maana yaani zinawajibisha wataalam/watendaji. Mbunge au diwani anawajibika kwa kuto wasimamia watendaji au kukwamisha mipango mizuri ya Serikali.


Bingo !!!!!

Na hii dhana ndio inayosababisha wabunge wanaochaguliwa kuwa mawaziri kuwa wanapendelea wilaya zao.
 
Ukiwa mchapa kazi na kama huna lengo la kushinda Dar na Dodoma ukivizia allowances kwenye kamati, kuna mambo mengi sana unaweza kuyafanikisha kule wilayani. Mambo mengi kinachotakiwa ni mobilization ya resources ile ile ambayo iko wilayani.

- Unaona sasa unaweza kuvizia allowances kwenye kamati basi unaweza kulisaidia jimbo lako, sasa hii inatakiwa kuwa moja ya kazi za mbunge yaani kuvizia allowances kwenye kamati, ahsante sana tutamfikishia mbunge huu ushauri.

Hii ya wabunge kushinda Ulaya kutafuta vitabu na vifaa vingine ambavyo hata havikidhi haja ya kule kwetu, kisha kuongozana na waandishi habari wa kulipwa, lipenenge na mdundiko ni usanii wa hali ya juu mno! Mungu isaidie Tanzania.

- Kama that is the case then hata kuishi Ulaya ni usanii kwa nini wananchi wote tusiihsi bongo tu kama wengine, maana kutafuta vitu vya ulaya vikasiaide jimbo ni usanii, si unaona kumbe hizi kelele zote against mbunge hizi ndio sababu zake, again ahsante sana mkuu labda tuwaambie wananchi wa Same East waliofadika na vitabu hivyo toka nje kuwa waliowaletea ni wasanii.

- Waandishi humfuata mbunge anayeweza kuuza magazeti yao na sio anything else, mbunge wa Same East anauza habari kwa sababu anakubalika na taifa sio jimbo lake tu mkuu, hiyo sio siri sasa ni lazima waandishi wamfuate kila anapokwenda na kila anachosema lazima kiwepo kwenye media maana media ni biashara, sio siasa wao wanatafuta kinachouza na sio lepenenge, mama Kilango hana hela za kuwalipa waandishi kufuatana nao, si unaoan sasa maneno yenu yanavyobadilika kutoka kwenye elimu, maji na sasa waandishi wa kulipwa, bwa! ha! ha!


Toka nimeanza kumfuatilia prof. Mwandosya sijawahi kuona akitafuta Waandishi wa habari wa kwenda kumwandikia anayoyafanya kule jimboni kwake. Aliyesema chema chajiuza na kibaya cha jitangaza hakukosea kabisa. Timiza wajibu wako, wananchi watajua, wala sio wajinga.

- Vipi lile sakata la Posta na simu mbona aliwalipa sana waandishi kumsafisha, kama ni ufisadi anao ule wa small scale au umesahau jinsi anavyosomeshewa mtoto wake na kampuni moja ya SA iliyopata tenda ya Posta wakati akiwa waziri. Eti kuna mbunge wa CCM anayetimiza wajibu wake na extra mile kuliko mbunge wa Same East? Mkuu vipi ndio hizi tunaita chuki za binafsi maana sasa ukisema eti kuna kujitangaza kwa mbunge Kilango, unakuwa nje ya mstari mkuu hasa wa ustaarbu wa siasa bongo maana huyu mbunge yuko level nyingine kabisaa inapokuja kueleweka anachokifanya kwa jimbo lake na taifa, infact CCM wanajua kuwa ahata kumsumbua kwenye kamati zao, hawawezi maana akitoka na kuingia upinzani, wataadihirika sana, mkuu naona huyajui vizuri ya uwezo wa kikazi wa huyu mbunge na kukubalika na wananchi.

- Wakuu labda mtafute sababu zingine lakini hii ya ku-create majungu naona mmekwama, na tutaendelea kuelimishana maana hatuwezi kukaa kimya huku wabunge waaminifu na wenye kukubalika na wananchi wa Tanzania wakiharibiwa majina yao huku JF bila sababu za msingi. Hii thread ni nothing out of nothing ila kujaribu kumchafua mbunge bila sababu, wananchi wa Tanzania wanajaua kazi nzito anazozifanya huyu mbunge yaani hahitaji kuandikwa tena, na wala hana harufu za ufisadi kama kina Mwandosya ambao kazi ni kunyamaza tu toka akiwa mbunge mpaka akiwa waziri, kazi ni kunyamaza eti chema kinajiuza nonesense, kwenye siasa hizi ideas za kizamani hazi-apply mkuu zimepitwa sana na wakati hizi hadithi za kale, siku hizi kina Mama kilango ni kumkoma nyani tu bila kuangalia usoni.

Mama kilango is doing just fine, wala hahitaji huu ushauri wa kumtukana kwanza eti kilaza, what a shame maana yeye akiwa kilaza sisi wananchi tunakuwa nini, wakuu acheni haya matusi ya nguoni toeni heshima wka wanaostahili heshima maana Mama Kilango anastahili heshima kubwa sana kama anayopewa na wananchi walioko nyumbani Tanzania, watashangaa sana kusikia wapenda mabadiliko tunavyojaribu kumchafua hapa bila sababu, yaani just because mtu mmoja humu ameamua tu antaka kumchafua basi anakurupuka na to my shock anapata washabiki tena wananchi wa Tanzania kama sisi wengine, that is wasup!

Thanxs!
 
...bottom line matokeo ya mitihani ni mabaya sana and something must be done,sasa swala la mbunge kama anawajibika na hayo matokeo is still debatable,lakini nafikiri kwa namna moja au nyingine THEY ARE kwa sababu ni wawakilishi wa waliowachagua na nina uhakika kwa kutumia nguvu zao za uhamasishaji na access to the corridor of power wanaweza kufanya chochote ili kusaidia,wanaweza hata demand accountability na wanaohusika moja kwa moja wakabadilishwa ili kuweka more competent personelly,hata lobbying ili kupata walimu zaidi/fund wilayani kwao wanaweza,hata kuhamasisha hali nzuri ya mazingira ya shule kuanzia vitabu,madarasa,uongozi wa shule etc wanaweza,mkuu field marshal nafikiri mbunge kuwa insulted kwa kuitwa kilaza ni jambo la kawaida sana as a politician na tumeona hata leaders of free world Bush,Obama etc wakiitwa mbaya zaidi lakini wengi wao wamechukulia kama challenge tuu na kujua ni frustration za wananchi wao na wananchi wana haki hiyo na tujue sio wote tunaweza kuongea lugha ya kistaarabu,nina uhakika mama kilango akiona haya malalamiko na hizo failure number atafanya kila kitu ili kuokoa wananchi wake...wanasiasa wataendelea kutukanwa kila siku but that means nothing to them,na mara zote matusi yana hidden message ambayo ni muhimu sana
 
Mkuu FMES,

Soma tena hiyo statement uliyo quote, umeelewa kinyume na maana yake. Wapi umetoa hilo la kwamba ukivizia allowances kwenye kamati unaweza kulisaidia jimbo lako?

Hili la ukilaza nafikiri unamwonea bure Gabusile maana hakusema mama Kilango au Mathayo ni vilaza. Alikuwa ana maana Same imegeuka kuwa vilaza. Tusiwe tunapotosha maana ya kitu maana kama ni kuelemishana basi ni muhimu mno kujadili ukweli na sio kuanza kujadili statements ambazo zimepindishwa.
 
Last edited:
Kamsome Adam Smith kuhusu mgawanyo wa kazi. Kazi zinafanyika kwa ufanisi pale kila mtu anaposhughulikia kile alichopangiwa.

Hivyo kazi ya mbunge ni kuwakilisha na sio kazi za kiutendaji. Kuna watendaji waliopewa mamlaka na bajeti ya kufanya kazi zinazopigiwa kelele hapa, je hao wanafanya nini :confused:

Unapomtaka mbunge awe ofisa elimu au Mwalimu mkuu, hujatenda haki. Na hili ndio matatizo yanayo wakabili watanzania.

Mkuu Zakumi,

Wala sihitaji kumsoma Adam Smith kuelewa hili. In facts nina lundo zima la vitabu na knowledge kwenye area ya management, wacha tusiende huko.

Katika mjadala huu hakuna hata mtu mmoja aliyetaka mbunge awe mwalimu mkuu au afisa elimu.

Ni dhana potofu na isiyofanya kazi kufikiri kazi kubwa ya mbunge ni kuwakilisha wananchi wake bungeni.

Ndio maana wabunge wote wanaojua grassroot politics wataendelea kutamba huku wengi wa wale wanaofikiri kazi zao ni kupiga kelele kule Dodoma, wakibwagwa kila baada ya miaka mitano.
 
No offense, Kuwa na lunda la vitabu aina maana unaelewa unachosoma.

Ukubwa wa jamii zetu na muundo wa uongozi ni sawa na assembly line ya kutengeneza magari. Kuna mtu kazi yake ni kufunga nati za matairi. Mwingine kupaka rangi n.k.

Kama nati zimekosewa kufungwa kwanini unamlaumu mpaka rangi :confused:.

Tumehamua kufuta utawala wa kidemokrasia na sheria na hiyo ndio price unayolipa.

Ingekuwa mama Kilango hafanyi kile alichotumwa kukifanya bungeni lawama zingekuwa halali.

Sasa mlichotaka mama Kilango afanye nini ??? Achape viboko waalimu ??? Kumbukeni kila shule Tanzania ina kamati ya walezi au wazazi. Je hao wana kamati wanafanya nini ???

Nikiwa boarding, kamati ya shule ilikuwa kazi yake kujadili nidhamu ya wanafunzi waliokamatwa wakigawiana URODA.

Grassroot politics ni pilau tu au mbunge akiteuliwa kuwa mbunge basi apendelee jimbo lake.

Tupeni mbunge mmoja tu bila kutumia misaada ya wahisani au nafasi yake ya kuteuliwa, aliyeweza kuongeza kiwango cha elimu jimboni kwake.
 
...bottom line matokeo ya mitihani ni mabaya sana and something must be done,sasa swala la mbunge kama anawajibika na hayo matokeo is still debatable,lakini nafikiri kwa namna moja au nyingine THEY ARE kwa sababu ni wawakilishi wa waliowachagua na nina uhakika kwa kutumia nguvu zao za uhamasishaji na access to the corridor of power wanaweza kufanya chochote ili kusaidia,wanaweza hata demand accountability na wanaohusika moja kwa moja wakabadilishwa ili kuweka more competent personelly,hata lobbying ili kupata walimu zaidi/fund wilayani kwao wanaweza,hata kuhamasisha hali nzuri ya mazingira ya shule kuanzia vitabu,madarasa,uongozi wa shule etc wanaweza,mkuu field marshal nafikiri mbunge kuwa insulted kwa kuitwa kilaza ni jambo la kawaida sana as a politician na tumeona hata leaders of free world Bush,Obama etc wakiitwa mbaya zaidi lakini wengi wao wamechukulia kama challenge tuu na kujua ni frustration za wananchi wao na wananchi wana haki hiyo na tujue sio wote tunaweza kuongea lugha ya kistaarabu,nina uhakika mama kilango akiona haya malalamiko na hizo failure number atafanya kila kitu ili kuokoa wananchi wake...wanasiasa wataendelea kutukanwa kila siku but that means nothing to them,na mara zote matusi yana hidden message ambayo ni muhimu sana

Koba:

Matatizo yanayotokea hapa yanategemea resources na resources zipo direct proportion na vipato vya wananchi wenyewe.

Sehemu nyingi tu nchi Tanzania vipato vya wananchi vimeshuka kutokana na sababu mbalimbali.

Pamoja na kushuka kwa vipato bado kuna watu wanadai high standard. High standard haiwezi kuja bila mapato.

Kuna uwezekano mkubwa shughuli zilizokuwa zinafanywa Same miaka ya nyuma hazi-make sense miaka ya sasa.
 
Kamsome Adam Smith kuhusu mgawanyo wa kazi. Kazi zinafanyika kwa ufanisi pale kila mtu anaposhughulikia kile alichopangiwa.

Hivyo kazi ya mbunge ni kuwakilisha na sio kazi za kiutendaji. Kuna watendaji waliopewa mamlaka na bajeti ya kufanya kazi zinazopigiwa kelele hapa, je hao wanafanya nini :confused:

Unapomtaka mbunge awe ofisa elimu au Mwalimu mkuu, hujatenda haki. Na hili ndio matatizo yanayo wakabili watanzania.

Hebu fafanua maana ya uwakilishi na kazi za mwakilishi!

Tatizo linalowakabili watanzania si kutaka wabunge wao wawe maafisa elimu bali kukataa/kuogopa kudai kuona matokeo ya wao kupewa uongozi huo. Tunatanguliza ushabiki, kufahamiana badala ya kuwa-hold responsible kwa ahadi walizotoa wakati wakiomba kura zetu. Tunaridhika tunapotupiwa makombo na tunapoona wanapigwa picha na wale tunaowaona ni wakubwa!

Bangusule kama mpiga kura na mkazi wa eneo lake amewauliza wabunge wake yale yanayomkwaza nasi tunamwandama na shutuma na matusi. Tumefikia hatua ya kudai ati amewatukana hao wabunge kwa kuwaita vilaza wakati alichosema ni kuwa watu wa Same ( yeye akiwemo,)wangeitwa Vilaza wa Kilimanjaro na Mwalimu R.I.P kama angefufuka leo! Ipo kazi.

Amandla.......
 
Mtanzania,

.....kule kajunjumele......tumeambiwa jana kwenye Alasiri kuwa wanafunzi 3,000 wameponzeka kutokana na upungufu wa madarasa.......ooohh yeah......Dr.Mwakyembe is to blame......!!

..........i mean where do we draw the line here..........between the case of Mh Kilango na Dr. Mwakyembe...........assuming arguments za bangusule....!!
 
Hebu fafanua maana ya uwakilishi na kazi za mwakilishi!

Kiswahili kinaeleweka vizuri kabisa Mkuu, 'uwakilishi' ni neno lisilo tata.

Tatizo linalowakabili watanzania si kutaka wabunge wao wawe maafisa elimu bali kukataa/kuogopa kudai kuona matokeo ya wao kupewa uongozi huo.

Ni haki ya mwananchi kumuuliza Mbunge juu ya masuala ya maendeleo kwani ndiyo mwakilishi wao. Kinachokataliwa hapa ni kumuona Mbunge ndiye aliyepaswa kuleta maendeleo au kuona kwamba mhusika namba moja ni Mbunge kwa lugha rahisi kumuona Mbunge ndiye kipaumbele (answerable) badala ya Mkurugenzi wa Halmashauri, Tanroads (ktk barabara), Mamlaka za Maji safi na maji taka (kwenye miji) nk.

Kumpatia uwajibikaji huu mbunge ni kujenga Taifa linalowategemea wanasiasa badala ya kuwategemea wataalam.

Bangusule kama mpiga kura na mkazi wa eneo lake amewauliza wabunge wake yale yanayomkwaza nasi tunamwandama na shutuma na matusi.

bangusilo anayohaki ya kuhoji, anayetoa matusi anakosea na amekosa ustaarabu. Bangusilo anakosea kuweka mategemeo pekee kwa Mbunge, anaendeleza dhana ya kujenga Taifa la wanasiasa. Hapo ndo kosa lilipo.

Tumefikia hatua ya kudai ati amewatukana hao wabunge kwa kuwaita vilaza wakati alichosema ni kuwa watu wa Same ( yeye akiwemo,)wangeitwa Vilaza wa Kilimanjaro na Mwalimu R.I.P kama angefufuka leo! Ipo kazi.

aisee! no comment.
 
- Mtanzania unawaita wananchi wa Same, vilaza kwa msingi gani hasa kwa sababu kama ni matokeo mabya ya elimu ni tatizo la taifa zima sasa kwa nini wananchi wa Same tu na wabunge wao ndio wawe vilaza? Vilaza ni taifa zima na sisi hapa included kama ni the ishu ya ukilaza, elimu ni tatizo la kila mwananchi, no way kuwa linapaswa kuwa tatizo la mbunge, tena in three years.

- Wewe na ndugu yako tuonyesheni namba za huko nyuma na za sasa tuweze kuona ni mbunge gani in the past wa hilo jimbo aliyeiinua elimu, wajibu wa mbunge wote tunaujua sasa nashangaa kwamba all over sudden sasa ni tatizo la mbunge na elimu, mbunge anaweza kufanya nini hasa kama amewapatia jimbo kila kitu, kuanzia vitabu mpaka waalimu, madarasa yapo sasa nini tena cha mbunge kufanya?

- Mbunge anapokuwa bungeni anakuwa sawa na wabunge wote wengine anahitaji kuombahela kutoka kwa serikali, asipopewa basi, lakini mbunge wa Same East amefanya mengi sana in the last three years which ni kusaidiwa kutokana na profile yake nationally ndio maana ameweza kupewa milingoti ya simu za mkono, rais wa jamhuri amekenda kufungua ujenzi wa bara bara muhimu kwa jimbo lake, ameleta vitabu contena nzima kutoka nje, maji ya visima vipya vya kisasa, I mean wananchi wa Same wanaridhika sana na kazi ya mbunge, maana kuna wananchi wengi sana wa jimbo lake ambao ni hihg political profiles wa taifa, kumbuka kuwa kuna viongozi kama Joyce Mapunjo, Asha Migiro, Balozi Manongi, Balozi Radhia, Mama Malale, na wengineo hawa ni viongozi wa taifa toka jimbo hilo la Same na wako very close katika kufuatilia maendeleo ya jimbo lao maana wako huko kila wakati kuangalia na siku zote wako makini sana kumpa maelekezo mbunge wao of what to do.

Sasa msitutishe hapa kwamba et nyinyi tu ndio wananchi wa hilo jimbo wakuu, hapana kuweni na heshima na wabunge wanaolisaidia taifa letu na majimbo yao, hizi siasa za kuharibiana majina humu JF haziwezi kutufikisha popote, zaidi tu ya kutushusha hadhi tu tena wengine mnaheshimika sana hapa JF, sasa kujiunga hii mijadala isiyokuwa na kichwa wala miguu ni aibu wakuu!

Thanxs!
 
........................Ni haki ya mwananchi kumuuliza Mbunge juu ya masuala ya maendeleo kwani ndiyo mwakilishi wao. Kinachokataliwa hapa ni kumuona Mbunge ndiye aliyepaswa kuleta maendeleo au kuona kwamba mhusika namba moja ni Mbunge kwa lugha rahisi kumuona Mbunge ndiye kipaumbele (answerable) badala ya Mkurugenzi wa Halmashauri, Tanroads (ktk barabara), Mamlaka za Maji safi na maji taka (kwenye miji) nk.

Kumpatia uwajibikaji huu mbunge ni kujenga Taifa linalowategemea wanasiasa badala ya kuwategemea wataalam..................

.......well said Nziku........tunapoendekeza/kutegemea wanasiasa kiasi hichi.....ndio maana tunawaachia watu kama akina Masha kufanya vitu watakavyo............na wengine wansema potelea mbali.............Damn!

......kama nilivyosema awali.........concerns za bangusule ni valid........however, ni vema watu tukaelewa responsibilities at different levels.........and ask ourselves where did we go wrong.....and correct where possible.........na sio mtu kuanza ku-point finger............which appear like pure politics...............Yes one can argue that..........why single out politicians on this failure........while its absolutely responsibilities of many other officers...........
 
Hebu fafanua maana ya uwakilishi na kazi za mwakilishi!

Tatizo linalowakabili watanzania si kutaka wabunge wao wawe maafisa elimu bali kukataa/kuogopa kudai kuona matokeo ya wao kupewa uongozi huo. Tunatanguliza ushabiki, kufahamiana badala ya kuwa-hold responsible kwa ahadi walizotoa wakati wakiomba kura zetu. Tunaridhika tunapotupiwa makombo na tunapoona wanapigwa picha na wale tunaowaona ni wakubwa!

Bangusule kama mpiga kura na mkazi wa eneo lake amewauliza wabunge wake yale yanayomkwaza nasi tunamwandama na shutuma na matusi. Tumefikia hatua ya kudai ati amewatukana hao wabunge kwa kuwaita vilaza wakati alichosema ni kuwa watu wa Same ( yeye akiwemo,)wangeitwa Vilaza wa Kilimanjaro na Mwalimu R.I.P kama angefufuka leo! Ipo kazi.

Amandla.......


Nadhani Nziku amefanya a fabulous job kukujibu. Labda mie nitie chachandu tu. Tunakubaliana kuwa maendeleo yako nyuma. Na hiyo sio Same pekee yake bali sehemu nyingi ambazo baada ya uhuru zilionyesha kuwepo kwa unafuu fulani.

Maendeleo ya elimu na mambo mengine ni lazima yawe direct proportion na mapato yao. Mpaka sasa madai ya Banguthule hayana mpango wowote hule. Kwa sababu anadai maendeleo wakati anajua wapare hafanyi kazi kama ilivyokuwa miaka ya zamani.

Kama maendeleo yao yalitokana na kufanya kazi kama waChina; walitakiwa kuendelea kufanya kazi kama waChina hili ku-sustain maendeleo yao. Kinachoonekana ni kuwa waPare wameacha kufanya kazi kama waChina na wanategemea sifa alizowapa Nyerere ziendelee kuwapa maendeleo.

Sasa kama waPare wameacha kufanya kazi, je mama Kilango afanye nini :confused:
 
Mtanzania,

.....kule kajunjumele......tumeambiwa jana kwenye Alasiri kuwa wanafunzi 3,000 wameponzeka kutokana na upungufu wa madarasa.......ooohh yeah......Dr.Mwakyembe is to blame......!!

..........i mean where do we draw the line here..........between the case of Mh Kilango na Dr. Mwakyembe...........assuming arguments za bangusule....!!

Mkuu Ogah,

Hakuna anayemlaumu Dr. kwasababu wanafunzi 3,000 waliofaulu wamekosa madarasa. In fact kinachofanyika sasa ndio kinatakiwa, cha kuunganisha wadau mbalimbali wa Kyela ili wachangie kujenga hayo madarasa.

Mfano wako ni tofauti kabisa na wa Bangusule. Ingelikuwa sawa kama Dr. baada ya kuona kuna tatizo angekaa kimya.

Hicho kilichofanyika ndio ambacho wengine tunakiona ni wajibu wa kiongozi yeyote yule. Ku mobilize resources mbalimbali kwa ajili ya kufikia lengo fulani.

BTW: Mimi nimeshatoa mchango wangu ili hao wanafunzi wapate madarasa na wakasome. Japo sikubaliani na sera hiyo ya quantity badala ya quality, lakini pamoja na tofauti zetu, la mgambo likilia hakuna kubishana tena. Viongozi wameomba msaada wa wananchi na tumeitikia.
 
No offense, Kuwa na lunda la vitabu aina maana unaelewa unachosoma.

Ukubwa wa jamii zetu na muundo wa uongozi ni sawa na assembly line ya kutengeneza magari. Kuna mtu kazi yake ni kufunga nati za matairi. Mwingine kupaka rangi n.k.

Kama nati zimekosewa kufungwa kwanini unamlaumu mpaka rangi :confused:.

Tumehamua kufuta utawala wa kidemokrasia na sheria na hiyo ndio price unayolipa.

Ingekuwa mama Kilango hafanyi kile alichotumwa kukifanya bungeni lawama zingekuwa halali.

Sasa mlichotaka mama Kilango afanye nini ??? Achape viboko waalimu ??? Kumbukeni kila shule Tanzania ina kamati ya walezi au wazazi. Je hao wana kamati wanafanya nini ???

Nikiwa boarding, kamati ya shule ilikuwa kazi yake kujadili nidhamu ya wanafunzi waliokamatwa wakigawiana URODA.

Grassroot politics ni pilau tu au mbunge akiteuliwa kuwa mbunge basi apendelee jimbo lake.

Tupeni mbunge mmoja tu bila kutumia misaada ya wahisani au nafasi yake ya kuteuliwa, aliyeweza kuongeza kiwango cha elimu jimboni kwake.

Mkuu Zakumi,

Nimecheka kuhusu mfano wako wa mpaka rangi na mfunga nati. Kwa taarifa tu kwenye uzalishaji wa kisasa mambo sio hivyo tena mkuu. Management ime kua mno kiasi kwamba sasa ownership ya kitu au jambo lolote ni wadau wote. Hakuna tena ya kwamba mimi mimi ni mpaka rangi, yule ni mfunga nati. Any way nisingetaka kwenda huko zaidi, huo unaweza kuwa mjadala mwingine na siku nyingine.

Unataka nikupe majina mara ngapi? Si nimekutajia mfano jimbo la Rungwe? Kwanini kwenye masuala ya shule na maendeleo liko mbele kuliko majimbo mengine Mbeya? Unafikiri ni bahati ya Mungu?

Sio mwanasiasa ila nakuhakikishia ningelikuwa kwenye hizo nafasi za Wabunge, nina uhakika ningeongeza kiwango cha elimu kwenye wilaya husika. Hakuna rocket science hapo, ni management tu. Kwa watu hao hao ambao leo wanasua sua kuchangia maendeleo yao, wakipata mtu anayejua anataka kufanya nini na akawa na nia ya kufanya hivyo, inawezekana kabisa mkuu wala sio kujisifu lakini nakuhakikishia ningekuwa kwenye wilaya hizo zenye elimu duni kwa nafasi yoyote ile, kuna kitu kitasogea.

Mimi ni mpenzi wa elimu na hata nikienda huko wilayani nakuwa frustrated na hali duni za shule nyingi. Naamini ni possible kabisa kuongeza huo ubora.
 
Mkuu Ogah,

Hakuna anayemlaumu Dr. kwasababu wanafunzi 3,000 waliofaulu wamekosa madarasa. In fact kinachofanyika sasa ndio kinatakiwa, cha kuunganisha wadau mbalimbali wa Kyela ili wachangie kujenga hayo madarasa.

Mfano wako ni tofauti kabisa na wa Bangusule. Ingelikuwa sawa kama Dr. baada ya kuona kuna tatizo angekaa kimya.

Hicho kilichofanyika ndio ambacho wengine tunakiona ni wajibu wa kiongozi yeyote yule. Ku mobilize resources mbalimbali kwa ajili ya kufikia lengo fulani.

BTW: Mimi nimeshatoa mchango wangu ili hao wanafunzi wapate madarasa na wakasome. Japo sikubaliani na sera hiyo ya quantity badala ya quality, lakini pamoja na tofauti zetu, la mgambo likilia hakuna kubishana tena. Viongozi wameomba msaada wa wananchi na tumeitikia.

......kwanza hongera sana kwa mchango wako huko kwenu........

.......Pili, naona sasa unakubaliana nami kwamba wa kulaumiwa panakosekana kitu i.e. kwenye failures kuna factors nyingi na sio kumlaumu moja kwa moja Mh Mbunge..........

....kwa upande wangu niko interested na hii mada kwani nimeishi kwa kipindi fulani pale same...zamani hizo.....hata juzi juzi nilikuwa pale wilayani i.e. Same.....trust me kwa juhudi anazofanya yule mama huwezi ku-justfy kum-blame Kilango eti kwa watu wamefeli vile au eti kwa kuwa mashambani watu hawawajibiki ipasavyo............kama ni juhudi hizo za ku-mobilze resources........huyu mama vilevile anazifanya........so whats the fuss here!.........au ndio politics as usual....attack your opponent......and you guys joined the game blindly.......huh!
 
......kwanza hongera sana kwa mchango wako huko kwenu........

.......Pili, naona sasa unakubaliana nami kwamba wa kulaumiwa panakosekana kitu i.e. kwenye failures kuna factors nyingi na sio kumlaumu moja kwa moja Mh Mbunge..........

....kwa upande wangu niko interested na hii mada kwani nimeishi kwa kipindi fulani pale same...zamani hizo.....hata juzi juzi nilikuwa pale wilayani i.e. Same.....trust me kwa juhudi anazofanya yule mama huwezi ku-justfy kum-blame Kilango eti kwa watu wamefeli vile au eti kwa kuwa mashambani watu hawawajibiki ipasavyo............kama ni juhudi hizo za ku-mobilze resources........huyu mama vilevile anazifanya........so whats the fuss here!.........au ndio politics as usual....attack your opponent......and you guys joined the game blindly.......huh!

Ogah,

Kama nilivyosema mwanzoni hii mifano miwili ni tofauti kabisa. Mmoja kuna watoto wengi zaidi wamefaulu mwaka huu na madarasa zaidi yanatakiwa, juhudi zinafanywa ili madarasa yajengwe na watoto wasome.

Mfano wa pili ni shule tisa kati ya kumi zinazoongoza kwa matokeo mabaya zinatoka wilaya moja ya Same. Hapo je viongozi wanawajibika kwa hilo? Kwa mimi yes.

Kama umeangalia michango yangu juu ya hili na pia baadhi ya wajumbe, mama Kilango hatajwi kabisa. Mimi nilimtaja mama Kilango kwenye post ya kwanza tu. Kwasehemu kubwa nimekuwa nikiongelea juu ya tatizo hili kwa wilaya mbalimbali.

Issue kwasasa sio mama Kilango tena bali ni hili tatizo la wabunge na dhana ya maendeleo kwenye wilaya zao.

Binafsi hata ningelikuwa mbunge nisingeweza hata siku moja kusema shule tisa kati ya kumi kuwa kwenye jimbo langu sio tatizo.

Hapo ndipo tunapotofautiana, labda ifike mahali tukubaliane kutofuatiana.

Huu mjadala umeleta hoja nyingi sana ikiwemo hoja ya misaada. Yaani Watanzania tuna kazi kubwa sana. Binafsi huwa nawaambia watu wakati wote maendeleo ya wilaya yataletwa na wilaya yenyewe.

Mkuu ogah, ukisikia siku mimi ni mbunge wa Kanjunjumele hapo mwaka 2030, nibebee bango tu kuhusu suala la maendeleo na mimi kama mbunge.
 
Unataka nikupe majina mara ngapi? Si nimekutajia mfano jimbo la Rungwe? Kwanini kwenye masuala ya shule na maendeleo liko mbele kuliko majimbo mengine Mbeya? Unafikiri ni bahati ya Mungu?

Hapana si bahati ya Mungu inawezekana kabisa matokeo hayo yamepatikana kwa juhudi za wadau mbali mbali akiwemo Mbunge wa jimbo kwa mchango wake mkubwa jimboni kwake ili kuinua kiwango cha elimu. Na mbunge huyo ana haki kabisa ya kujipiga kifua popote pale kujivunia matokeo ya jimboni kwake na hata kutumia matokeo hayo mazuri kwenye kampeni zake
 
Back
Top Bottom