Gsana
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 4,383
- 1,321
Jk wakati Nec imekutangaza rais,ulitwambia kuwa chadema na wapinzani ni vyama vya msimu. Uliwaagiza baada ya kampeni na baada ya kura wawe na utamaduni wa kutembelea taifa zima,ulienda mbali ukasema wawe wanazunguka kufungua matawi wasiishie dar tu.(Rejea hotuba yako ya kufunga mwaka 2010). Sasa cdm wameanza kuzunguka na kufanya mambo unalalama kuwa wanataka kukupindua! Juzi umetugeuka kuwa mabomu yalitokea tar.17 february wakati sie tuliokumbwa na mabomu ya gongo la mboto,tuliumizwa tar.16. Je ni lini utakuwa na msimamo,au kusalimu amri na kukiri thinking capacity inaelekea turning point? Sina imani na Rais Jk. Kama umelemewa na mzigo utue,kama hamna wa kukupokea mzigo,uweke chini na ukimbie! Jk tukueleweje?