Precise Pangolin
JF-Expert Member
- Jan 4, 2012
- 12,998
- 6,659
Huyu Kigwangalla anatumia muda mrefu kwenye vyombo vya habari ikiwemo JF yenyewe kuzungumzia hoja ambazo ni moja ya sera za CCM kwa mfano suala la ajira kwa vijana pamoja na makazi bora inajieleza vizuri wakati mzee wa trip alipokuwa akiomba kura na kuahidi Maisha bora kwa kila Mtanzania.
Kwa hiyo badala ya huyu dr kutumia muda mrefu kutuelezea masuala ambayo tulishayasikia wakati wa kampeni aende jimboni kwake akatekeleze yote waliyo ahidi likiwemo hilo la maisha bora kwasababu chama chake ndio chenye dola na huu ni muda wa kuzitekeleza sera zao.
Kwa hiyo awaachie CDM waende kwenye vyombo vya habari wawaelezee wananchi kwasababu wao hawana nafasi ya kuzitekeleza kwavile sio walioshinda. Pia kuhusu hoja zake binafsi akae na wabunge wenzake ambao ni wengi bungeni ili wamuunge mkono asitafute umaarufu wa kijinga kutoka kwa vijana ambao ndio inaonekana anawalenga.
Kwa hiyo badala ya huyu dr kutumia muda mrefu kutuelezea masuala ambayo tulishayasikia wakati wa kampeni aende jimboni kwake akatekeleze yote waliyo ahidi likiwemo hilo la maisha bora kwasababu chama chake ndio chenye dola na huu ni muda wa kuzitekeleza sera zao.
Kwa hiyo awaachie CDM waende kwenye vyombo vya habari wawaelezee wananchi kwasababu wao hawana nafasi ya kuzitekeleza kwavile sio walioshinda. Pia kuhusu hoja zake binafsi akae na wabunge wenzake ambao ni wengi bungeni ili wamuunge mkono asitafute umaarufu wa kijinga kutoka kwa vijana ambao ndio inaonekana anawalenga.