Dokta Greyson: Kula huku unachezea simu hupunguza nguvu za kiume

Mjanja M1

JF-Expert Member
Oct 7, 2018
3,660
12,305
Dokta Greyson Babishomba akiwa anafanya mahojiano na Kituo cha Redio Times Fm, amesema kuwa tabia ya wanaume kula wakati wanachezea simu zao hupelekea tatizo la nguvu za kiume.

ANGALIA VIDEO HAPA


Nini maoni yako?

Written by Mjanja M1 ✍️
 
Dokta Greyson Babishomba akiwa anafanya mahojiano na Kituo cha Redio Times Fm, amesema kuwa tabia ya wanaume kula wakati wanachezea simu zao hupelekea tatizo la nguvu za kiume.

ANGALIA VIDEO HAPA
View attachment 2895905

Nini maoni yako?

Written by Mjanja M1 ✍️
Mihogo inageukaje kuwa mafuta?
Au mafuta yanageukaje kuwa mafuta?
Kajamaa kaungo haka, kanaonekana kanaishi na maumivu mengi sana. Haipaswi kutumia simu wakati wa kula, sawa ila mwisho wakesi hayo ayaongeayo.
 
Huyu Sio Daktari Hata biology ya Darasa la Tatu tu hajui..
Watu waliotoroka Milembe ndo mnawapa Airtime kwenye Radio ndo kosa kubwa la Tanzania..

Metabolic Inahusiana Vipi na Tumbo?
Kwanza afundishwe mifumo inavofanya kazi..
PIli afundishwe Process nzima ya Digestion..
Tatu Asikurupuke kujibu vitu asuvyovijua
Asante..
 
Nashauri huyu Daktari apokonywe Leseni yake.

Hili tatizo la nguvu za kiume naona imekuwa kama fimbo ya kutuchapa Wanaume.

Ukienda Kwa Mganga anakwambia una tatizo la nguvu za kiume.

Hospitali utaambiwa una tatizo la nguvu za kiume.

Mkeo naye nyumbani ukimuudhi anakwambia Mwanaume gani huna nguvu za kuniridhisha

Kwa kweli Wanaume tuanzishe Chama cha kututetea sasa 🙌
 
Nashauri huyu Daktari apokonywe Leseni yake.

Hili tatizo la nguvu za kiume naona imekuwa kama fimbo ya kutuchapa Wanaume.

Ukienda Kwa Mganga anakwambia una tatizo la nguvu za kiume.

Hospitali utaambiwa una tatizo la nguvu za kiume.

Mkeo naye nyumbani ukimuudhi anakwambia Mwanaume gani huna nguvu za kuniridhisha

Kwa kweli Wanaume tuanzishe Chama cha kututetea sasa 🙌
Kumbe mnaumiaga eeh?
😃😃😃
 
Kumbe mnaumiaga eeh?
😃😃😃
Tena hakuna maumivu makali kama ya kuambiwa na Mpenzio/Mkeo eti hauna nguvu za kumridhisha.

Hata kama mnara ulikuwa juu kushinda ule mnara wa Babeli lakini utajikuta umelala doro

Ndiyo maana wengine tunashukuru tulivyo Zeeka sasa maana tumepishana na hayo masimango 😜

Nikiambiwa Sina nguvu za kumridhisha namtolea cheti cha kuzaliwa, namwambia huoni miaka yote hii 78 niliyonayo unataka Mzee miye nikufe kifuani 🏃🏃🏃🏃
 
Simu na tv na all electronic devices light emitting zina punguza chemical inayoitwa melatonin ambayo ni responsible for sleep inawezekana ikawa kweli na inaongeza uchovu pia.
 
Sijamsikiliza ila nimeisoma heading na comments za wadau hapo juu na mimi naunga mkono uyo ni Daktari uchwara kabisa.
 
Dokta Greyson Babishomba akiwa anafanya mahojiano na Kituo cha Redio Times Fm, amesema kuwa tabia ya wanaume kula wakati wanachezea simu zao hupelekea tatizo la nguvu za kiume.

ANGALIA VIDEO HAPA
View attachment 2895905

Nini maoni yako?

Written by Mjanja M1

Huyu jamaa niliwahi kuona tena interview yake nadhani ni hapo hapo Times FM anasema kwamba mwili wa binadamu una mifumo miwili mikubwa ambayo ni mfumo wa homoni na mfumo wa neva..

Sasa sehemu ambazo ambazo hazina neva hasa za uzazi huwa zinatumia mfumo wa homoni kama mbadala wake nikasema kwa nini anapotosha namna hii?

Leo tena kahamia kwenye digestion hahaha...

Ifike wakati tuwe tunaheshimu taaluma za watu.
 
Back
Top Bottom