Dkt. Tulia atakuwa mbunge wa kwanza Tanzania nzima kutangazwa mshindi wa kiti cha Ubunge 2025

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,293
9,723
Ndugu zangu Watanzania,

Kwa namna dkt Tulia anavyokubalika,kupendwa, kuaminika na kuungwa mkono na wana Mbeya. kwa hakika uchaguzi ujao Dr Tulia atakuwa mbunge wa kwanza kushinda na kutangazwa mshindi mapema sana na kuacha wananchi wakifunga barabara na jiji zima kwa shangwe, nderemo na vifijo kushangilia ushindi wake.

Maana kila mtu anasubiri kwa hamu na kwa kiu kubwa sana siku na wakati ufike ili ampigie kura ya ndio Dr Tulia. kila mtu anataka kujiwekea historia ya kumpigia kura Rais wa IPU. kila mtu anataka kuitangazia Dunia kuwa hawakukosea kumchagua kuwa Rais wao wa IPU ,kwa kuwa hata wao wana Mbeya bado wanaendelea kumpenda na kumhitaji kuendelea kuwa mbunge wao.

Kwa sasa kila mwana Mbeya anataka kuja kupiga kura kama sehemu ya kutoa shukurani na asante kwa Dr Tulia kwa kazi kubwa aliyoifanya na kugusa maisha ya wana Mbeya wengi. Dr Tulia kwa sasa hahitaji kutumia nguvu katika kampeni maana wana Mbeya wanaendelea kumpigia kampeni kila siku, wanaendelea kuonyesha na kutaja mambo aliyoyafanya katika uongozi wake ambayo yalikuwa hayajawahi kufanywa na mbunge aliyemtangulia.

Kikubwa tuendelee kumuombea afya njema na nguvu za kuendelea kuwatumikia wana Mbeya .tumuombe Mungu aendelee kumpigania, kumtetea na kumlinda wakati wote. Mungu aendelee kuwa upande wake na kumuongoza katika kila hatua apigayo .lakini pia Dr Tulia naye aendelee kumtumainia na kumtegemea Mungu katika kila jambo kama ambavyo amekuwa akifanya siku zote .

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
 
Wee jamaa waliokuloga ni makatili sana ! Maana wameloga kuanzia nyayo hadi utosi .
Shida ni pale alipokaribishwa na kukabidhi medulla, na bahati mbaya aliyemkabidhi ame rest in peace
20231116_044137.jpg
 
Wakati fulani unatakiwa kupunguza njaa na kujipendekeza kulikopitiliza. Halafu siyo jambo la kawaida kwa mwanaume aliyekamilika, kujipendekeza hovyo eti!!

Maana ukiulizwa kama mchakato wa kumtafuta mgombea wa chama kwa hiyo nafasi kama umeshafanyika, au uhakika wa asilimia ngapi kama huyo Tulia wako atakuwepo hiyo 2025! Sidhani kama utakuwa na majibu sahihi.
 
Aibu kubwa sana !
Aibu ni ile ya mtangulizi wake kukaa miaka kumi katika ubunge pasipo kufanya jambo lolote analoweza kuonyesha kwa watu wala kuonekana machoni pa watu. Embu fikiria muda wote huo alishindwa hata kusaidia tu chama chake kujenga hata ofisi ya chama mkoa kwa ajili ya kufanyia vikao na kukutana na wanachama wenzake. Sugu alikosa ubunifu,upeo,maono,akili ya kujuwa nini wana Mbeya wana taka,nini kiu cha wengi,aseme nini bungeni kwa ajili ya wana Mbeya na kipi kipewe kipaombele.

Sasa ngoja barabara za njia nne zitandikwe pale Mbeya ili awe wa kwanza kwenda kukatisha katisha na kupiga nazo picha.Dr Tulia angeongoza miaka kumi aliyokuwepo sugu basi leo hii Mbeya na jiji lingekuwa mbali sanaaa kimaendeleo.lingekuwa ni jiji la mfano .

Mwenzie Haonga alishabakia anavizia kunakotokea misiba ndio anakwenda kuuza sura na kujipitisha pitisha kama machinga.
 
😄😄😄Wewe endelea na biashara yako hapo Desderia. Lakini jimbo la Mbeya mjini ni mali halali ya Dr Tulia uchaguzi ujao.kapewa kibali na wana Mbeya ili aendelee kuwaletea maendeleo
Kwa jinsi chaguzi zetu zilivyo za kishenzi, na zilivyopuuzwa na wananchi hata mkimtangaza wiki ijayo kuwa ni mbunge ni sawa. Kama unadhani ukileta hizi nyuzi unadhani watu watahamasika na huo ushenzi uitwao uchaguzi, basi umeukalia.
 
Kwa jinsi chaguzi zetu zilivyo za kishenzi, na zilivyopuuzwa na wananchi hata mkimtangaza wiki ijayo kuwa ni mbunge ni sawa. Kama unadhani ukileta hizi nyuzi unadhani watu watahamasika na huo ushenzi uitwao uchaguzi, basi umeukalia.
Pole sanaa mkuu maana naona umejikatia tamaa sana hasa baada ya kuona upepo mkali wa Dr Tulia unaovuma jiji la Mbeya, ambao umeisambaratisha CHADEMA na kuifanya kwenda kujifungia kabatini.
 
Pole sanaa mkuu maana naona umejikatia tamaa sana hasa baada ya kuona upepo mkali wa Dr Tulia unaovuma jiji la Mbeya, ambao umeisambaratisha CHADEMA na kuifanya kwenda kujifungia kabatini.
Usifananishe kupuuza na kukata tamaa. Hakuna mtu anayejitambua ataendelea kupoteza muda wake kishiriki hizi chaguzi za kishenzi. Machafuko tu ama mapinduzi ya kijeshi ndio yatarejesha heshima ya box la kura. Ila kwa sasa mazombie ndio mtaendelea kupoteza muda kwenye mstari wa kura kuwa mnachagua viongozi.
 
Aibu ni ile ya mtangulizi wake kukaa miaka kumi katika ubunge pasipo kufanya jambo lolote analoweza kuonyesha kwa watu wala kuonekana machoni pa watu. Embu fikiria muda wote huo alishindwa hata kusaidia tu chama chake kujenga hata ofisi ya chama mkoa kwa ajili ya kufanyia vikao na kukutana na wanachama wenzake. Sugu alikosa ubunifu,upeo,maono,akili ya kujuwa nini wana Mbeya wana taka,nini kiu cha wengi,aseme nini bungeni kwa ajili ya wana Mbeya na kipi kipewe kipaombele.

Sasa ngoja barabara za njia nne zitandikwe pale Mbeya ili awe wa kwanza kwenda kukatisha katisha na kupiga nazo picha.Dr Tulia angeongoza miaka kumi aliyokuwepo sugu basi leo hii Mbeya na jiji lingekuwa mbali sanaaa kimaendeleo.lingekuwa ni jiji la mfano .

Mwenzie Haonga alishabakia anavizia kunakotokea misiba ndio anakwenda kuuza sura na kujipitisha pitisha kama machinga.
Barabara kwani huyo Tulia ndiye anatoa pesa, hizo ni kodi za wananchi na ni wajibu wake kutengeneza barabara hilo hata si la kumsifu. Miaka zaidi ya 60 bado mna siasa za ki5senge kusifu uundaji wa barabara na mashimo ya vyoo shuleni.

Inasikitisha sana, mambo yaisha pitwa na wakati, badilikeni.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kwa namna dkt Tulia anavyokubalika,kupendwa, kuaminika,kuungwa mkono na wana Mbeya. kwa hakika uchaguzi ujao Dr Tulia atakuwa mbunge wa kwanza kushinda na kutangazwa mshindi mapema sana na kuacha wananchi wakifunga barabara na jiji zima kwa shangwe, nderemo na vifijo kushangilia ushindi wake.

Maana kila mtu anasubiri kwa hamu siku na wakati ufike ili ampigie kura ya ndio Dr Tulia. kila mtu anataka kujiwekea historia ya kumpigia kura Rais wa IPU. kila mtu anataka kuitangazia Dunia kuwa hawakukosea kumchagua kuwa Rais wao wa IPU ,kwa kuwa hata wao wana Mbeya bado wanaendelea kumpenda na kumhitaji kuendelea kuwa mbunge wao.

Kwa sasa kila mwana Mbeya anataka kuja kupiga kura kama sehemu ya kutoa shukurani na asante kwa Dr Tulia kwa kazi kubwa aliyoifanya na kugusa maisha ya wana Mbeya wengi. Dr Tulia kwa sasa hahitaji kutumia nguvu katika kampeni maana wana Mbeya wanaendelea kumpigia kampeni kila siku, wanaendelea kuonyesha na kutaja mambo aliyoyafanya katika uongozi wake ambayo yalikuwa hayajawahi kufanywa na mbunge aliyemtangulia.

Kikubwa tuendelee kumuombea afya njema na nguvu za kuendelea kuwatumikia wana Mbeya .tumuombe Mungu aendelee kumpigania, kumtetea na kumlinda wakati wote. Mungu aendelee kuwa upande wake na kumuongoza katika kila hatua apigayo .lakini pia Dr Tulia naye aendelee kumtumainia na kumtegemea Mungu katika kila jambo kama ambavyo amekuwa akifanya siku zote .

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Haya masifa yenu ya kuendelea kuhadaa viongozi wenu kisa maokoto yatawatokea puani, kama ambavyo mnamuhadaa mwenyekiti wenu nakuangukia pua, mfano ya Taifa star jana, kama hajawashutukia yatakua ni matatizo yake binafsi , sasa mnaamia kwa Tulia ili mpige maokoto yake , ambayo mbele yatamsaidia kuwekeza kwa ajili ya vizazi vyake,kwani lazima awe mbunge ,ilo jimbo wamepita wangapi, na je alijua kwamba anaweza kuwa mbunge na kua speaker? Mbona nyuma hamkusifia mpaka leo kisa yupo na maokoto

Tulia atapigwa mapema sana Kwenye jimbo atake asitake pamoja na maokoto yake kama uchaguzi ukifanyika.

Ningekua ni wakaribu yake ,ningemwambia kuacha kugombea angalau Linda heshima kidogo aliyonayo.

Uchaguzi ukifanyika ,utakua ni uchaguzi wa wanahaki vs ccm , na unaweza kwenda vunja history za chaguzi ndani ya bara la Afrika , msichukulie poa jana sio leo ,majira yamebadilika sana
 
Back
Top Bottom