Ally Msangi
JF-Expert Member
- Jun 29, 2010
- 608
- 120
Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi Zanzibar- ZEC, Khatibu Mwinyichande ametangaza matokeo hayo mbele ya waandishi wa habari, ambapo amesema katika jimbo la Fuoni watu elfu 9, 367 sawa na (86.0%) kati ya wapiga kura 10,880 waliojiandikisha wamepiga kura. Dkt. Sheini amejipatia kura 6,351(61.0%) katika jimbo hilo.
Mtoni - ugunja watu 8, 768(90.7%) kati ya 9, 672 waliojindikisha wamepiga kura ambapo Dkt. Sheini amepata kura 3, 746(43%)Huko Dole kati ya watu 8, 017 waliojiandikisha ni asilimia 86.6 ya wapiga kura 6, 972 ndio wamepiga kura.Mgombea huyo wa CCM amepata kura 4, 777 sawa na asilimia 69.9%
Katika jimbo la Dimani waliojitokeza kupiga kura ni watu 11,383(88.8%) kati ya watu 12,813 waliojianikisha, Dkt. Sheini alijipatia kura 6, 225(55.5%)Kiembesamaki ni asilimia 35 nukta nne tu yaani watu 3, 856 kati ya watu 10, 884 wamejitokeza kupiga kura ambapo Dkt.Sheini amepata kura elfu 2,734 sawa na asilimia 71.8
Kwa upande wa jimbo la Mwanakerekwe ni watu elfu 7,293 sawa na asilimia 90.5 kati ya watu 8,064 waliojiandikisha kupiga kura ndio wameshiriki katika zoezi la kupiga kura. Mgombea wa CCM amekipata asilimia 60.4 yaani kura 5338. Huko Bububu Dokta Sheini amepata kura 4, 458(51.8%) kati ya kura 8,727 ya kura zilizopigwa. Watu 9,809 walijiandikisha kupiga kura katika jimbo la Bububu
Wapiga kura elfu 6,203 kati ya 7,242 waliojiandikisha kupiga kura wameshiriki katika uchaguzi ambapo Dkt.Sheini amepata asililimia 62.2 baada ya kupata kura 3,755Mfenesini Dokta Sheini amepata kura 3755 sawa na asuiimia 62.2. Wapiga kura 6203(85.75) kati ya 7242 waliojiandikisha kupiga kura wameshiriki uchaguzi huo.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa ZEC katika jimbo la Mpendae watu 8,596 sawa na asilimia 90.9 ya watu waliojiandikisha kupiga kura wameshiriki katika uchaguzi huo na Dkt. Sheini wa CCM amepata kura 4,870 ambazo ni sawa na asilimia 57.5 wakati mpinzani wake wa karibu Sharif Hamad Seif wa CUF akipata kura 3,546 sawa na asilimia 41.8.
Huko Kuhani katika wapiga kura 7,497 waliojiandikisha 6,459(86, 2%) wameshiriki kupiga kura, katika kura hizo Dkt Sheini amepata asilimia 78 .1 ya kura zilizopigwa. Katika jimbo hili Hamad amepata asilimia21.1.
Katika jimbo la mji mkongwe idadi ya waliojitokeza kupiga kura ni 6, 414 sawa na asilimia 85.6 ya watu 7, 495 waliojiandikisha, mgombea wa CCM Dkt Sheini amepata kura 1,589 sawa na asilimia 25.1. Hamad amepata kura 4, 717 sawa na asilimia 74.5.
Matokeo pia yameonyesha kuwa katika jimbo la Amani watu 6,837 (89.5%) kati ya 7,641 waliojiandikisha kupiga kura. Sheini ameibuka na kura 4, 367 sawa na asilimia 64.9 % huku Hamad akipata kura 2, 312 sawa na asilimia 34.4.
Katika jimbo la Raha Leo Dokta Sheini amepata asilimai 64.2%(4043) kati ya kura 6,399 zilizopigwa kutoka watu 7,229 waliojiandikisha kupiga kura na Hamad amepata kura 2216 (35.2%)
Kutoka Kikwajuni Sheini imejipatia kura 4,534(70.5%) kati ya kura 6,513 zilizopigwa na waliojiandilkisha ni watu 7,910 nae Hamad amepata kura 1, 860 (28.9%)
Dkt. Sheini amepata kura 2734 sawa na asilimia 71.8% ya kura 3856, nae Hamad amepata kura 1, 041(27.2%) ambapo watu 4698 walijiandikisha kupiga kura katika Jimbo la Kiembe Samaki.