Dkt. Mpango: Askari wa Barabarani wakianza kuvaa Kamera itapunguza Rushwa

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,454
8,288
DODOMA: Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango amelitaka Jeshi la Polisi kukamilisha mchakato wa matumizi ya Kamera zitakazokuwa zikivaliwa na Askari wakiwemo wa Usalama Barabarani kwa lengo la kudhibiti Vitendo vya Rushwa

Dkt. Mpango ameeleza hayo wakati akizindua Kituo cha Polisi Daraja A, Mtumba Jijini Dodoma ambapo amesema "Waziri wa Mambo ya Ndani amenihakikishia mchakato wa ufungaji Kamera za Barabarani Kamera za Mavazi (Body Cam Jacket za Askari umeanza ili kuongeza weledi kwa Trafiki na usalama Barabarani"

Ameongeza "Askari Polisi anapokuwa anaongea na Madereva huko Barabarani kila kitu kinakuwa kinaonekana na kwa hiyo nafasi ya Rushwa inakuwa imepungua sana"
 
Wafanye hivyo mapema maana Hawa maaskari wamegeuka kero kwa madereva na pia kua sehemu ya kuchangia ajali nyingi.
 
Sisi tutawasaidia kupata chochote kitu ili waendelee kuishi. Rushwa mnajua kuwabana askari ila sio wale waliotajwa kwenye ripoti ya CAG.

Mnaonea wafanyakazi wa serikali kada ya chini huku juu wala hamkazanii, mbona hamsemi ripoti ya CAG ifanyiwe maamuzi.
 
Waacheni askari wanatusaidia
Nikiwa na kosa la eld 30 nawapaga buk 2 wanapoa kabisa
Waacheni askari
 
Mbona mtaweka kamera hadi chooni na wizi na rushwa bado utawazidi nguvu.
Hapo kupewa tenda tu ya kushona hizo nguo zenye camera rushwa itaanzia hapo
 
Hayo ni mawazo ya kuofilisi nchi. Hapo labda pana mkubwa anaitaka tenda hiyo.
Kama mnataka kawafungeni tembo na mafisi kamera wakienda kwenye makazi ya watu mzuiye mauaji
 
DODOMA: Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango amelitaka Jeshi la Polisi kukamilisha mchakato wa matumizi ya Kamera zitakazokuwa zikivaliwa na Askari wakiwemo wa Usalama Barabarani kwa lengo la kudhibiti Vitendo vya Rushwa

Dkt. Mpango ameeleza hayo wakati akizindua Kituo cha Polisi Daraja A, Mtumba Jijini Dodoma ambapo amesema "Waziri wa Mambo ya Ndani amenihakikishia mchakato wa ufungaji Kamera za Barabarani Kamera za Mavazi (Body Cam Jacket za Askari umeanza ili kuongeza weledi kwa Trafiki na usalama Barabarani"

Ameongeza "Askari Polisi anapokuwa anaongea na Madereva huko Barabarani kila kitu kinakuwa kinaonekana na kwa hiyo nafasi ya Rushwa inakuwa imepungua sana"
Mimi kama driver nitatambua vp kua hiyo camera alovaa haijazimwa ipo ON?
 
Tenda hii anatafutiwa mtu achote speed governer zilikoishia hazijulikani yani Trafic uwadhibiti kwa makoti ya kamera sijui, makoti watavaa na tutapigwa tu na Mapato halali ya Serkali yanaweza kupungua vile vile
 
DODOMA: Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango amelitaka Jeshi la Polisi kukamilisha mchakato wa matumizi ya Kamera zitakazokuwa zikivaliwa na Askari wakiwemo wa Usalama Barabarani kwa lengo la kudhibiti Vitendo vya Rushwa

Dkt. Mpango ameeleza hayo wakati akizindua Kituo cha Polisi Daraja A, Mtumba Jijini Dodoma ambapo amesema "Waziri wa Mambo ya Ndani amenihakikishia mchakato wa ufungaji Kamera za Barabarani Kamera za Mavazi (Body Cam Jacket za Askari umeanza ili kuongeza weledi kwa Trafiki na usalama Barabarani"

Ameongeza "Askari Polisi anapokuwa anaongea na Madereva huko Barabarani kila kitu kinakuwa kinaonekana na kwa hiyo nafasi ya Rushwa inakuwa imepungua sana"
Isiinyie hapo. Camera ziwepo vituo vya polisi, Ofisi za TRA, Hospitali, Benki na ofisi nyingine zote za umma pale reception. (Reception tu) Itaongeza nidhamu, uchapakazi kwa watumishi wengi wa umma.
 
DODOMA: Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango amelitaka Jeshi la Polisi kukamilisha mchakato wa matumizi ya Kamera zitakazokuwa zikivaliwa na Askari wakiwemo wa Usalama Barabarani kwa lengo la kudhibiti Vitendo vya Rushwa

Dkt. Mpango ameeleza hayo wakati akizindua Kituo cha Polisi Daraja A, Mtumba Jijini Dodoma ambapo amesema "Waziri wa Mambo ya Ndani amenihakikishia mchakato wa ufungaji Kamera za Barabarani Kamera za Mavazi (Body Cam Jacket za Askari umeanza ili kuongeza weledi kwa Trafiki na usalama Barabarani"

Ameongeza "Askari Polisi anapokuwa anaongea na Madereva huko Barabarani kila kitu kinakuwa kinaonekana na kwa hiyo nafasi ya Rushwa inakuwa imepungua sana"
Hakika
 
Ameongeza "Askari Polisi anapokuwa anaongea na Madereva huko Barabarani kila kitu kinakuwa kinaonekana na kwa hiyo nafasi ya Rushwa inakuwa imepungua sana"
Huyu jamaa yuko soft sana, anazungumza kama hisani ati "Imepungua" hafikirii kuiondoa na kuitokomeza kabisa isiwepo
 
Back
Top Bottom