Dkt. Mollel: CHADEMA walipanga njama za kumpiga risasi Lissu

Yaani watolewa walinzi wote halafu wauaji wahakikishiwe kinga na aliyewatuma then wawe labda askari cha ajabu watumie 30+ bullets kwa umbali mdogo hivyo et mtu aishie kupigwa miguu!!! Hakuna miujiza ya hivyo au unadhani yule mhuni wa New Zealand aloowaua mosque hawamjui Mungu?
 
Ujinga huu wa Mollel aliutoa Feb 2019 mbele ya Bunge, ni jambo la ajabu kuwa hadi Leo hii June 23 bado hajaitwa popote kutakiwa asaidie maelezo yatakayo ifikisha Chadema au viongozi wake kortini.
Maana halisi Mbunge Mollel amepuuzwa kuwa ni mjinga au mpumbavu.
Hii inaleta maana kuwa hawa watu walionunuliwa ni wajinga kiasi kwamba hata huko CCM wanapaswa kukaa nao kwa machale kwani wana unafiki kuzidi wa shetani mwenyewe
 
Basi jamani utata umeisha,bwana mollel unaambiwa anao ushahid wooooteeeeee, ila atautoa tu pale chadema itakapoeleza matumizi ya ruzuku
Kwa hiyo tusubiri jeshi la polisi waongee na msajili wa vyama na CAG kuhusu ruzuku ili kumlainisha bwana mollel atoe ushahidi wake huo
**Halii hii inaonyesha wazi kwamba ukihama cdm kwenda ccm akili zako zinaongezeka sana, Dr Mollel katisha vibaya mno.


View attachment 1017124

Kwa ufupi
Mbunge huyo wa Siha aliyehama Chadema na kujiunga CCM amesema tukio la Tundu Lissu kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 ni mpango uliosukwa na Chadema ingawa hakuwa tayari kuthibitisha madai yake.


Dodoma. Mbunge wa Siha (CCM), Dk Godwin Mollel amesema tukio la Tundu Lissu kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 jijini Dodoma ni mpango uliosukwa na Chadema na kutoa sharti kwa chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania kuwa wakilitimiza atakuwa tayari kuthibitisha.

Dk Mollel, mbunge wa zamani wa Siha kwa tiketi ya Chadema aliyejiunga CCM mwaka 2018 na kupitishwa kuwania ubunge na kuibuka na ushindi, ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Februari 8, 2019 bungeni jijini Dodoma.

Amesema hata siku ya kufanya uchunguzi baada ya Lissu kupigwa risasi, kuna baadhi ya sampuli aliziiba lakini uongozi wa Chadema ulikataa pendekezo lake la kupeleka sampuli hiyo Afrika Kusini kufanya uchunguzi kwani walikuwa na hofu ya kuumbuliwa.

“Mimi nilikuwa huko lakini nilikimbia kwa mipango yao, hata katika tukio la kushambuliwa Lissu mimi niliingia ndani kwenye uchunguzi na niliiba baadhi ya vitu lakini wakakataa mapendekezo yangu," amesema Mollel.

Hata hivyo, mbunge wa Tunduma (Chadema), Frank Mwakajoka aliomba taarifa akimtaka Dk Mollel kueleza ni kwa nini alikuwa anakiuka kiapo cha udaktari, na mbunge huyo wa Siha kujibu kuwa alifanya hivyo kwa sababu alikuwa kada mwaminifu wa Chadema.

Wakati Mwakajoka akieleza hayo, mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini alimtaka Dk Mollel kuthibitisha madai yake kuhusu Lissu.

Katika majibu yake Dk Mollel amesema hawezi kuthibitisha hadi Chadema watakapomueleza fedha za ruzuku zinakwenda wapi na mpango waliotaka kuufanya kwa Zitto Kabwe (mbunge wa Kigoma Mjini) na marehemu Chacha Wangwe, walipotaka kugombea uenyekiti wa Chadema.

Soma Zaidi: Alichokisema dereva wa Lissu katika mahojiano Ujerumani
When was the case opened?!
 
Nadhani ni vema tukawa tunajadili kauli za watu ambao wana akili timamu.

Mole sidhani kama ni mzima. Mtu yeyote anayeweza kukubali kununuliwa lazima awe na upunguani wa aina fulani. Huyu definately ni punguani.

Hata serikali yenyewe inajua kuwa kauli hii imetoka kwa punguani ndiyo maana hakuna atakayeifanyia kazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Badala ya kujibu hoja wewe unajikita kurusha vijembe?
 
Napenda kuwashauri wana JF kuacha tabia ya kuwasingizia watu maneno magumu haiwezekani mtu kama mollel atamke maneno kama hayo tunajua ni msomi na ni mtunga sheria wa nchi lakini kama ni yeye kweli na aliosema alidhamiria ninaamini sasa atakuwa amelisaidia jeshi letu pendwa namna ya kuanza uchunguzi wao maana waliotenda mollel anawajua na atakuwa tayari kuweka kila kitu wazi huko polisi lakini akiweka wazi hadharani atakuwa anawasaidi wauaji namna ya kujipanga kujibu na ninaamini tena kwa maelezo haya polisi.

Wataanza haraka sana lakini tukiona jeshi letu limepuuza na haliwahoji waliotajwa na wala mollel hajaitwa kutoa ushirikiano tunaweza amini mollel kafilisika ubongo na itakuwa ni ishara tosha ya kuonyesha hana uwezo wa kuongoza na itakuwa ni aibu kwa waliomchagua mimi ninavyowajua polisi huwa hawadharau tuhuma kama huamini sema kwa fulani kuna dawa za kulevya uone muziki wake.
 
Mtoa mada, subiri Tundu Lissu arudi pamoja na dereva wake ili watowe ushirikiano kwa vyombo vya dola, kisha ndipo utajua kwamba, mpango wa kushambuliwa Tundu Lissu ulipangwa ndani ya chadema au hapana.

Aidha katika ushirikiano huo pia utajua kwa nini Tundu Lissu alipigwa risasi mguu wa kulia alikokuwa dereva wake na si mguu wa kushoto ilikodaiwa washambuliaji walikuwa. Pia utajua kwa nini Dereva wa Tundu Lissu alishuka kwenye gari na kwenda kujificha ndipo boss wake akashambuliwa.

Na kama washambuliaji walitoka nje ya chadema, kwa nini walisubiri dereva ashuke? Je, washambuliaji hao walikuwa na makubaliano yoyote ya kutomdhuru dereva isipokuwa Tundu Lissu pekee?

Na mwisho utajua, kwa nini risasi zilizodaiwa kumpiga Tundu Lissu zilitoka 54 tulizoelezwa awali, na sasa tunaambiwa ni 19 tu? Sambamba na yote hayo utajua kwa nini mara baada ya shambulio, chadema haikutaka kumtoa dereva kusaidia vyombo vya uchunguzi kwa kisingizio cha kuathirika kisaikolojia. Je, saikolojia inatibiwa Kenya na baada ya Kenya alipewa rufaa ya kutibiwa Ubelgiji?

Akili za kuambiwa, changanya na za kwako.
 
Njaa ni mbaya sana aisee!! Bora nife rofa kuliko kutumika kwa aibu namna hii.
 
Back
Top Bottom