Dk. Ndulu wa BoT apata tuzo ya gavana bora Afrika

Josh Michael

JF-Expert Member
Jun 12, 2009
2,523
77
Na Victoria Msina, Uturuki

GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania, Profesa Benno Ndulu ameshinda tuzo ya mwaka huu ya Gavana bora kwa Afrika inayotolewa na jarida maarufu la Emerging Markets.

Kila mwaka gazeti hilo linalochapishwa jijini London, Uingereza, hutambua mafanikio yaliyofanywa na watendaji wakuu wa benki kuu na mawaziri wa fedha na kuwapa tuzo wakati wa mikutano ya Benki Kuu ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).

Gazeti hilo linaongoza kwa kuandika habari zinazohusu mikutano ya Benki ya Dunia, IMF na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB). Limekuwa likifanya hivyo kwa miaka 18 sasa.

Sherehe za kutoa tuzo hiyo zitafanyika leo katika mji wa Binbidirek Cistern, Istanbul, Uturuki, ambako Gavana anahudhuria mikutano ya kimataifa.

Tuzo aliyopata Gavana Ndulu inatokana na kura za maoni zilizokusanywa kitaalamu na gazeti la Emerging Markets kutoka kwa magavana wa benki kuu wa nchi za Afrika na Ulaya, wawekezaji, wachumi na wachambuzi wa kimataifa.

Profesa Ndulu ametambuliwa kutokana na jitihada kubwa alizozifanya kuiongoza Benki Kuu ya Tanzania tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo na Rais Jakaya Kikwete Januari 2008.

Katika kipindi hicho, Gavana huyo amehakikisha kuwa hali ya uchumi wa nchi umetengemaa kwa kuhakikisha hali ya ubadilishanaji wa fedha za kigeni na masoko ya fedha iko imara. Hadi mwishoni mwa mwaka 2007, viwango vya riba vya dhamana za serikali za muda mfupi vilikuwa vinapanda na kushuka kila wakati. Hata hivyo, hali hiyo imebadilika na kuwa tulivu, huku viwango vya riba vikishuka. Chini ya uongozi wa Profesa Ndulu, Benki Kuu haitegemei sana kuuza dhamana za serikali peke yake.

Kwenye upande wa ubadilishanaji wa fedha za kigeni, Julai 2007, mtu alihitaji kuwa na Sh 1,300 kupata dola moja ya Marekani. Hali hiyo imebakia karibu hivyo hivyo kwa kipindi cha miaka miwili ambapo sasa dola moja ya Marekani inabadilishwa kwa kati ya Sh 1,310 na 1,320.

Huko nyuma, viwango vya kubadilishana fedha za kigeni vilikuwa vinaongezeka kwa karibu asilimia 10 hadi 15 kwa mwaka na kufanya thamani ya shilingi iwe inashuka tu.

Chini ya uongozi wa gavana Ndulu, akiba ya fedha za kigeni, katika kipindi cha miaka miwili imeongezeka kutoka dola za Kimarekani bilioni 2.4 hadi kufikia dola bilioni 3.6, sasa, kiwango ambacho hakijawahi kufikiwa hapa nchini.

Magavana wa benki kuu barani Afrika, wachumi na wawekezaji, pia wametambua jitihada za Prof. Ndulu kusimamia mzunguko wa fedha. Ukiondoa chakula, mfumuko wa bei uko katika asilimia 2, utendaji ambao pia unapongezwa na IMF.

Profesa Ndulu ametambuliwa pia kutokana na jinsi alivyosimamia kwa utaalamu mkubwa wa changamoto mbalimbali ambazo zimejitokeza wakati wa uongozi wake wa BoT, zikiwemo mdororo wa uchumi wa kimataifa na ufisadi katika akaunti ya madeni ya nje (EPA).

Akizungumzia kuchaguliwa kwake kupata tuzo hiyo, Gavana Ndulu alisema: “Tuzo hii inatokana na viwango vya utendaji kazi vya Benki Kuu. Ninafurahi kutambuliwa. Tuzo hii ni tuzo ya Benki Kuu ya Tanzania.”

Mhariri wa Emerging Markets, Taimur Ahmad, anasema: “Tuzo hii ni alama ya wazi kabisa ya imani ambayo wewe (Prof. Ndulu) umeijenga kwa wadau muhimu.”

Washindi waliopita wa tuzo ya Gavana wa Mwaka wa Benki Kuu barani Afrika ni pamoja na Gavana wa Benki Kuu ya Zambia, Dr Caleb Fundanga na aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Nigeria, Prof Charles Soludo.
 
Duh kweli watu wanaandika. The man deserves the award. Mtu kama anastahili sifa tusema. Amefanya reform inayoonekana. Tatizo ameingia kipindi ambacho nchi imepitia katika mgogoro wa kiuchumi, let be realistic
 
Ni kweli kabisa kuwa amefanya mambo makubwa na pia kama mtu akifanya vizuri lazima tuseme, sasa mimi nashangaa sana kuona huyu jamaa anasema kuwa mafisadi wameamua kugawanya??
 
Naona mafisadi wameanza kugawiana ma tuzo
Nascent rhetoric, watu hata wakiona hawaelewi.
This guy Benno Ndullu is doing a thankless job of sweeping the wrongs that have accumulated over the years.
-watoto wa vigo kuajiriwa BOT
-uchapishaji feki wa noti
-wizi wa EPA na Import support
-BOT towers
Na mengine mengi sana.
Si kwamba Magavana hawakuwapo miaka yote hiyo la hasha.
Sasa kama mtu haoini hilo,kilichobaki ni kumhurumia tu.
 
Si yote ya kubeza. Wengine wanachangia siasa kwenye proffessionalisms. mambo mengine yapo wazi. Kuna nchi zina hali mbaya zaidi hasa katika kipindi hiki cha economic crisis. Jamaa amesimamia sera za kiuchumi vizuri. Honestly I can see we are moving forward when we dig deep the history of the institution and other macro economic variables.
 
I really agree this guy hata ukisoma mambo yake kweli amefanya vizuri sana, Tatizo moja letu kubwa ni politics nyingi sana
 
Miye naombwa kufahamishwa makubwa yepi aliyofanya? Akiwa naibu gavana ndiyo wizi wa EPA wa $133 millioni au Shilingi bilioni 133 (wakati ule) ulitokea. Alipoingia alitangaza kuunda tume ili kuchunguza kama kama shilingi bilioni 8 alizolipwa Nimrod Mkono kama wakili wa BoT zilikuwa halali na alisema kama malipo hayo hayakuwa halali watamuomba Mkono arudishe malipo hayo na atakuwa tayari kufungua mashtaka dhidi ya Mkono, lakini hadi leo hatujasikia chochote kuhusiana na matokeo ya uchunguzi wa tume aliyoiunda.
 
I really don't see what this guy has done that is so great, not that he has done a bad job, but what exactly did he do to merit this award? That whole institution is rotten to the core and i think it is to early to start giving the guy awards. Or is the competition so bad that he wins by default?
 
Miye naombwa kufahamishwa makubwa yepi aliyofanya? Akiwa naibu gavana ndiyo wizi wa EPA wa $133 millioni au Shilingi bilioni 133 (wakati ule) ulitokea. Alipoingia alitangaza kuunda tume ili kuchunguza kama kama shilingi bilioni 8 alizolipwa Nimrod Mkono kama wakili wa BoT zilikuwa halali na alisema kama malipo hayo hayakuwa halali watamuomba Mkono arudishe malipo hayo na atakuwa tayari kufungua mashtaka dhidi ya Mkono, lakini hadi leo hatujasikia chochote kuhusiana na matokeo ya uchunguzi wa tume aliyoiunda.
Kama swali lako ni makubwa tu basi mie nitakutajia ni reform iliyofanyika baada ya kuwa yeye gavana, kusimamia uchunguzi wa EPA(kumbuka hakuna mshtakiwa aliyemtaja kuhusika), kupitia ajira za wafanyakazi na usimamizi wa uchumi katika kipindi hiki kigumu.
 
Miye naombwa kufahamishwa makubwa yepi aliyofanya? Akiwa naibu gavana ndiyo wizi wa EPA wa $133 millioni au Shilingi bilioni 133 (wakati ule) ulitokea. Alipoingia alitangaza kuunda tume ili kuchunguza kama kama shilingi bilioni 8 alizolipwa Nimrod Mkono kama wakili wa BoT zilikuwa halali na alisema kama malipo hayo hayakuwa halali watamuomba Mkono arudishe malipo hayo na atakuwa tayari kufungua mashtaka dhidi ya Mkono, lakini hadi leo hatujasikia chochote kuhusiana na matokeo ya uchunguzi wa tume aliyoiunda.

BAK kumbuka , hizi scandal nyingi zilifanya kukiwepo na Magavana wengine juu ya huyu aliyepo.
Na hao Magavana wengine hawakuwa wana act unilateraly, walikuwa wanashirikiana na vigogo wengine serikalini.
Vigogo hao hawajafa, bado wapo.
It makes sense to me not to bite more than you can chew.
 
Miye naombwa kufahamishwa makubwa yepi aliyofanya? Akiwa naibu gavana ndiyo wizi wa EPA wa $133 millioni au Shilingi bilioni 133 (wakati ule) ulitokea. Alipoingia alitangaza kuunda tume ili kuchunguza kama kama shilingi bilioni 8 alizolipwa Nimrod Mkono kama wakili wa BoT zilikuwa halali na alisema kama malipo hayo hayakuwa halali watamuomba Mkono arudishe malipo hayo na atakuwa tayari kufungua mashtaka dhidi ya Mkono, lakini hadi leo hatujasikia chochote kuhusiana na matokeo ya uchunguzi wa tume aliyoiunda.

BAK

Nantanguliza heshima. Naomba nikufahamishe kuwa Prof. Ndulu hakuhusika kabisa na masuala ya EPA. Prof. Ndulu alikuwa akifanya kazi World Bank Washington DC kwa muda mrefu. Karibu na mwishoni wa mwaka 2007, Rais wa Jamhuri ya Muungano alifanya mabadiliko ya uongozi wa Banki Kuu ambapo aliamua kuwa kuwe na madeputy watatu, Prof. Ndulu aliteuliwa kuwa mmoja wa hao madeputy, hivyo mwezi wa kumi, mwalimu Ndulu aliondoka Washington kurudi Tanzania kuchukua nafasi ya deputy gavana, miezi miwili baadaye, Balali akachishwa kazi kwa sababu tunazozijua wote, ndiyo hapo prof. Ndulu alipopandishwa cheo na kuwa gavana, kwa msingi huu, naomba ieleweke kuwa Gavana Ndulu alifanya kazi kama deputy gavana kwa pungufu ya miezi mitatu mwishoni mwa mwaka 2007 wakati matatizo ya EPA yalikuwa yameishatokea, hakuhusika kabisa hasa ukizingatia kuwa alikuwa nje ya nchi kwa muda mrefu akifanya kazi world Bank. Tumhakiki ufanyaji wake wa kazi kuanzia 2008 alipoteuliwa kuwa Gavana. Wakati wa sakata la EPA, Prof. hakuwa mfanya kazi wa BOT, licha ya kuwa deputy gavana. Kaa salama.
 
Namkubali sana kwa uongozi wake na pia nampongeza. hata hivyo sio lazima kila mtu amkubali kila kiongozi, watu wengine tumekuwa negative zaidi, tunatafuta mabay ya mtu ndo tuseme, yale mazuri tunayaponda. Keep going Ndullu
 
BAK kumbuka , hizi scandal nyingi zilifanya kukiwepo na Magavana wengine juu ya huyu aliyepo.
Na hao Magavana wengine hawakuwa wana act unilateraly, walikuwa wanashirikiana na vigogo wengine serikalini.
Vigogo hao hawajafa, bado wapo.
It makes sense to me not to bite more than you can chew.

Unapokuwa Naibu Gavana wa BoT na madudu kama ya EPA yanafanyika pale na wewe kama msaidizi wa Gavana basi na wewe pia unastahili kubeba lawama za yaliyotokea. Uchunguzi wa malipo ya shilini bilioni 8 kwa Nimrod Mkono mbona hadi hii leo hajasema lolote lile!? Miye bado namuona huyu naye ni bomu tu ana shule kubwa sana lakini kwenye utendaji bado kabisa. Kama hili la kuchunguza malipo ya Mkono kama yalikuwa halali au la limechukua zaidi ya miezi sita sasa, basi hali hii ni mfano tosha jinsi utendaji wake ulivyo mbovu.
 
Unapokuwa Naibu Gavana wa BoT na madudu kama ya EPA yanafanyika pale na wewe kama msaidizi wa Gavana basi na wewe pia unastahili kubeba lawama za yaliyotokea. Uchunguzi wa malipo ya shilini bilioni 8 kwa Nimrod Mkono mbona hadi hii leo hajasema lolote lile!? Miye bado namuona huyu naye ni bomu tu ana shule kubwa sana lakini kwenye utendaji bado kabisa. Kama hili la kuchunguza malipo ya Mkono kama yalikuwa halali au la limechukua zaidi ya miezi sita sasa, basi hali hii ni mfano tosha jinsi utendaji wake ulivyo mbovu.
Basi kama ndio hivyo Katibu Mkuu wizara ya fedha,Bodi nzima ya BOT ya wakati huo, Waziri wa fedha wa wakati huo pia naye yupo wote walikuwa mabomu tu
 
Basi kama ndio hivyo Katibu Mkuu wizara ya fedha,Bodi nzima ya BOT ya wakati huo, Waziri wa fedha wa wakati huo pia naye yupo wote walikuwa mabomu tu

Naam wewe kama una nafasi kubwa mahali popote pale na ukashindwa kuona wizi mkubwa kama ule wa EPA basi ni bomu tu, lakini siyo kwenye nchi yetu. Watu wanaweza kuwa wanayaona madudu lakini wanafumba macho makusudi au kwa kuogopa kusulubiwa na vingunge wao au na wao ni washiriki katika wizi huo. Hatujui ushahidi kuhusu EPA si ajabu katika wizi huo labda Ndullu alishiriki katika baadhi ya mijadala ya kuidhinisha malipo hayo, lakini kwa vile waliamua kumbalali Balalli labda siri ya wizi ule itabaki ni siri milele.
 
Back
Top Bottom