Mtu66
Senior Member
- Jun 26, 2007
- 165
- 3
Na Aristariko Konga
MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Dk. Idrissa Rashid ametumia Sh. 49,122,800 kununulia maua, samani, sanamu na mapambo mengine ya nyumba.
Maua hayo, mapambo, sanamu na vitu vingine vya anasa vimewekwa kwenye nyumba hiyo iliyopo kati ya mitaa wa Toure na Chaza Lane, kitalu namba 13, Oysterbay, Dar es Salaam.
Zabuni ya mapambo ya nyumba hiyo ya TANESCO, ambayo inakaliwa na Dk. Rashid inahusu ununuzi wa maua ya plastiki na mapoti yake, fremu za kuwekea picha ukutani, saa za ukutani, mashine za kufulia nguo, vyombo vyote vya kulia, majokofu na mafriza, meza za urembo wa akina mama wanapojiremba na mazulia.
Sh. 26,283,000 zimetumika katika zabuni ya kununulia seti ya maua, meza, viti, mazulia, fremu za picha oveni, taa ya umeme ya mezani, saa ya ukutani,mashine ya kuoshea, masofa na friza. Vilinunuliwa kutoka kampuni ya M/s McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furnitures, ya Dar es Salaam.
Kiasi kingine cha Sh. 12,586,800 kilitumika katika zabuni ya kununulia seti nyingine ya maua na mapoti yake, vitanda, meza, viti, mazulia, stuli na makabati. Vilinunuliwa kutoka kampuni ya M/s Haase General Enterprises Ltd, ya Dar es Salaam.
Sh. 5,850,000 zilitumika katika zabuni ya ununuzi wa masofa kutoka kampuni ya M/s McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furnitures, wakati Sh. 3,724,000 zilitumika kununulia friza, na mashine ya kuoshea. Vilinunuliwa kutoka kampuni ya M/s Game ya Dar es Salaam.
Sh. 680,000 zilitumika katika zabuni ya ununuzi wa mazulia, yakiwamo ya Kichina, kutoka kampuni ya M/s McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furnitures, ya Dar es Salaam.
Zabuni za samani na mapambo zilifanywa bila ya kulinganishwa bei kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni kujitokeza kwa mzabuni mmoja kwa kila bidhaa.
Kampuni ambazo zilikuwa zimeomba zabuni ya kutoa samani na mapambo hayo ni M/s McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furnitures, ya Dar es Salaam, M/s Clock Tower Shopping Centre, Gift Land, Game Ltd na M/s Haase General Enterprises Ltd.
Kila kampuni ilipendekeza bei za samani na mapambo hayo kama ifuatavyo: McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furniture (Sh. 5,585,000), Clock Tower Shopping Centre (Sh. 895,000), Gift Land (Sh. 1,260,000), McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furniture (Sh. 13,831,30, Haase General Enterprises Ltd (Sh. 26,283,000), Game Ltd (Sh. 3,724,000) na McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furniture (680,000).
Hata hivyo, timu ya tathmini ya TANESCO, ikiwa na wajumbe wanne, ilisema kuwa makampuni mawili kati ya hayo, hayakuwa na mwitikio mzuri wa kibiashara. Makampuni hayo ni Clock Tower Shopping Centre na Gift Land.
Kutokana na hali hiyo, timu hiyo iliweza kutembelea makampuni matatu tu ili kukagua bidhaa. Makampuni hayo ni McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furnitures, Haase General Enterprises Ltd na Game Ltd.
Timu ta tathmini ya TANESCO iliwajumuisha Rajabu Mbiro kutoka Kurugenzi ya Raslimali Watu, Gracen H. Ndibalema kutoka kitengo cha Mipango na Miradi, Reward Nyerembe kutoka kitengo cha Mipango na Miradi na Justi Masaua, mhasibu wa miradi mikubwa. Timu hiyo iliteuliwa na mwenyekiti wa bodi ya zabuni ya TANESCO, ambaye jina lake halijatajwa.
Tayari Dk. Rashid amekarabati nyumba ya shirika anayoishi hivi sasa kwa zaidi ya Sh. 500 milioni, jambo ambalo mbunge wa Sumve, Richard Ndassa, alililalamikia bungeni.
Uchunguzi wa MwanaHALISI umebaini kuwa Dk. Rashid mkataba wake wa miaka mitatu hauruhusu kukaa kwenye nyumba ya shirika, na kwa hiyo ununuzi wa samani na mapambo hayo ni kwa manufaa binafsi. Mkataba wake ulianza Novemba, 2006 unakwisha mwezi huu.
Mameneja wa Net Group Solution, ambao nao walikuwa na mkataba kama wa Dk. Rashid hawakukaa kwenye nyumba za shirika hilo.
Mfanyakazi mmoja mwandamizi kwenye wizara ya nishati na madini anasema hata kama mkataba wa Dk. Rashid ulikuwa unamruhusu kukaa kwenye nyumba ya shirika, basi angekaa kwenye nyumba ambayo miaka yote ya uhai wa TANESCO, imetengwa kwa ajili ya mkurugenzi mtendaji.
Nyumba iliyokuwa inatumiwa na mkurugenzi mtendaji kabla ya TANESCO kukabidhiwa kwa Net Group Solution ipo kitalu namba 7, Kenyatta Drive, Oysterbay, Dar es Salaam, ambayo inakaliwa na mkurugenzi mmoja wa shirika hilo, ambaye jina lake halikuweza kupatikana.
Dk. Rashid analipwa Sh. Milioni 11 kwa mwezi na TANESCO.
Taarifa za ndani ya TANESCO zinasema Agosti mwaka huu, Dk. Rashid alinunua magari ya bei mbaya aina ya Toyota Hilux na kuyatawanya nchi mzima.
Hali hiyo ni kinyume na agizo la Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwamba viongozi wa umma, wakiwamo mawaziri, kuachana na mtindo wa kununua magari ya kifahari.
Habari zaidi zinasema kuwa Dk. Rashid amenunua gari jipya kwa ajili ya matumizi yake, lenye thamani ya Sh. 180 millioni.
Dk. Rashid pia anadaiwa kuwa amewanunulia viongozi wengine sita wa juu wa TANESCO (Executive Management Members) magari yanayofanana na lake kwa thamani ya Sh. 160 milioni. Maofisa waliopewa magari mapya tayari walikuwa na magari mengine ambayo bado yalikuwa kwenye hali nzuri.
Wafanyakazi wa TANESCO wanashangazwa na ununuzi wa magari hayo wakati ofisi za shirika hilo mikoani zina matatizo makubwa ya usafiri, yanayozorotesha huduma kwa wateja.
Ofisi hizo zinashindwa kukidhi matakwa ya kuwafungia wateja umeme au kushughulikia matatizo ya dharura, kama nguzo zinapoanguka au waya kukatika.
Mchakato wa kumpata mkurugenzi mtendaji mpya wa TANESCO unaendelea na MwanaHALISI limedokezwa kuwa majina 12 yamepatikana baada ya mchujo kutoka watu 30, ambao waliomba wadhifa huo ulipotangazwa.
Kamati maalum yenye wajumbe kutoka bodi ya wakurugenzi, wizara ya nishati na madini na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Idara ya Uhandisi) walitarajiwa kukutana juzi na jana (tarehe 9 na 10 Novemba, 2009) ili kufanya usaili wa watu hao 12 na kupata majina matatu ambayo yangepelekwa ngazi za juu ili mmoja ateuliwe kushika nafasi ya Dk. Rashid.
Habari zinasema kuwa Dk. Rashid ameonyesha nia ya kutokuendelea na wadhifa huo na wala hakuomba kuendelea, na hivi karibuni alituma waraka kwa wafanyakazi kuwashukuru kwa ushirikiano wao miaka mitatu aliyofanya kazi.
Ingawa baadhi ya watu wanasema Dk. Rashid alifanya kazi nzuri akiwa TANESCO na kuimarisha hali ya shirika kifedha, wengine wanasema shirika liliimarika kutokana na mikataba ya Aggreko na Alstom, ya miaka miwili kukamilika, mkataba wa Dowans kuvunjwa, IPTL kusimamisha uzalishaji umeme na TANESCO kukataa kulipa malipo yake ya capacity charges, hivyo shirika likaweza kupeleka fedha sehamu nyingine, licha ya mkopo wa Sh. 280 bilioni, ambao mwaka 2007 TANESCO ilichukua kwenye mabenki kadhaa, yakiwamo Stanbic, CRDB, Exim na National Microfinance (NMB).
Source: Mwanahalisi
HIVI TANZANIA TUMELOGWA???????
MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Dk. Idrissa Rashid ametumia Sh. 49,122,800 kununulia maua, samani, sanamu na mapambo mengine ya nyumba.
Maua hayo, mapambo, sanamu na vitu vingine vya anasa vimewekwa kwenye nyumba hiyo iliyopo kati ya mitaa wa Toure na Chaza Lane, kitalu namba 13, Oysterbay, Dar es Salaam.
Zabuni ya mapambo ya nyumba hiyo ya TANESCO, ambayo inakaliwa na Dk. Rashid inahusu ununuzi wa maua ya plastiki na mapoti yake, fremu za kuwekea picha ukutani, saa za ukutani, mashine za kufulia nguo, vyombo vyote vya kulia, majokofu na mafriza, meza za urembo wa akina mama wanapojiremba na mazulia.
Sh. 26,283,000 zimetumika katika zabuni ya kununulia seti ya maua, meza, viti, mazulia, fremu za picha oveni, taa ya umeme ya mezani, saa ya ukutani,mashine ya kuoshea, masofa na friza. Vilinunuliwa kutoka kampuni ya M/s McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furnitures, ya Dar es Salaam.
Kiasi kingine cha Sh. 12,586,800 kilitumika katika zabuni ya kununulia seti nyingine ya maua na mapoti yake, vitanda, meza, viti, mazulia, stuli na makabati. Vilinunuliwa kutoka kampuni ya M/s Haase General Enterprises Ltd, ya Dar es Salaam.
Sh. 5,850,000 zilitumika katika zabuni ya ununuzi wa masofa kutoka kampuni ya M/s McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furnitures, wakati Sh. 3,724,000 zilitumika kununulia friza, na mashine ya kuoshea. Vilinunuliwa kutoka kampuni ya M/s Game ya Dar es Salaam.
Sh. 680,000 zilitumika katika zabuni ya ununuzi wa mazulia, yakiwamo ya Kichina, kutoka kampuni ya M/s McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furnitures, ya Dar es Salaam.
Zabuni za samani na mapambo zilifanywa bila ya kulinganishwa bei kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni kujitokeza kwa mzabuni mmoja kwa kila bidhaa.
Kampuni ambazo zilikuwa zimeomba zabuni ya kutoa samani na mapambo hayo ni M/s McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furnitures, ya Dar es Salaam, M/s Clock Tower Shopping Centre, Gift Land, Game Ltd na M/s Haase General Enterprises Ltd.
Kila kampuni ilipendekeza bei za samani na mapambo hayo kama ifuatavyo: McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furniture (Sh. 5,585,000), Clock Tower Shopping Centre (Sh. 895,000), Gift Land (Sh. 1,260,000), McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furniture (Sh. 13,831,30, Haase General Enterprises Ltd (Sh. 26,283,000), Game Ltd (Sh. 3,724,000) na McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furniture (680,000).
Hata hivyo, timu ya tathmini ya TANESCO, ikiwa na wajumbe wanne, ilisema kuwa makampuni mawili kati ya hayo, hayakuwa na mwitikio mzuri wa kibiashara. Makampuni hayo ni Clock Tower Shopping Centre na Gift Land.
Kutokana na hali hiyo, timu hiyo iliweza kutembelea makampuni matatu tu ili kukagua bidhaa. Makampuni hayo ni McSOMS Furniture Mart T/A Royal Furnitures, Haase General Enterprises Ltd na Game Ltd.
Timu ta tathmini ya TANESCO iliwajumuisha Rajabu Mbiro kutoka Kurugenzi ya Raslimali Watu, Gracen H. Ndibalema kutoka kitengo cha Mipango na Miradi, Reward Nyerembe kutoka kitengo cha Mipango na Miradi na Justi Masaua, mhasibu wa miradi mikubwa. Timu hiyo iliteuliwa na mwenyekiti wa bodi ya zabuni ya TANESCO, ambaye jina lake halijatajwa.
Tayari Dk. Rashid amekarabati nyumba ya shirika anayoishi hivi sasa kwa zaidi ya Sh. 500 milioni, jambo ambalo mbunge wa Sumve, Richard Ndassa, alililalamikia bungeni.
Uchunguzi wa MwanaHALISI umebaini kuwa Dk. Rashid mkataba wake wa miaka mitatu hauruhusu kukaa kwenye nyumba ya shirika, na kwa hiyo ununuzi wa samani na mapambo hayo ni kwa manufaa binafsi. Mkataba wake ulianza Novemba, 2006 unakwisha mwezi huu.
Mameneja wa Net Group Solution, ambao nao walikuwa na mkataba kama wa Dk. Rashid hawakukaa kwenye nyumba za shirika hilo.
Mfanyakazi mmoja mwandamizi kwenye wizara ya nishati na madini anasema hata kama mkataba wa Dk. Rashid ulikuwa unamruhusu kukaa kwenye nyumba ya shirika, basi angekaa kwenye nyumba ambayo miaka yote ya uhai wa TANESCO, imetengwa kwa ajili ya mkurugenzi mtendaji.
Nyumba iliyokuwa inatumiwa na mkurugenzi mtendaji kabla ya TANESCO kukabidhiwa kwa Net Group Solution ipo kitalu namba 7, Kenyatta Drive, Oysterbay, Dar es Salaam, ambayo inakaliwa na mkurugenzi mmoja wa shirika hilo, ambaye jina lake halikuweza kupatikana.
Dk. Rashid analipwa Sh. Milioni 11 kwa mwezi na TANESCO.
Taarifa za ndani ya TANESCO zinasema Agosti mwaka huu, Dk. Rashid alinunua magari ya bei mbaya aina ya Toyota Hilux na kuyatawanya nchi mzima.
Hali hiyo ni kinyume na agizo la Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwamba viongozi wa umma, wakiwamo mawaziri, kuachana na mtindo wa kununua magari ya kifahari.
Habari zaidi zinasema kuwa Dk. Rashid amenunua gari jipya kwa ajili ya matumizi yake, lenye thamani ya Sh. 180 millioni.
Dk. Rashid pia anadaiwa kuwa amewanunulia viongozi wengine sita wa juu wa TANESCO (Executive Management Members) magari yanayofanana na lake kwa thamani ya Sh. 160 milioni. Maofisa waliopewa magari mapya tayari walikuwa na magari mengine ambayo bado yalikuwa kwenye hali nzuri.
Wafanyakazi wa TANESCO wanashangazwa na ununuzi wa magari hayo wakati ofisi za shirika hilo mikoani zina matatizo makubwa ya usafiri, yanayozorotesha huduma kwa wateja.
Ofisi hizo zinashindwa kukidhi matakwa ya kuwafungia wateja umeme au kushughulikia matatizo ya dharura, kama nguzo zinapoanguka au waya kukatika.
Mchakato wa kumpata mkurugenzi mtendaji mpya wa TANESCO unaendelea na MwanaHALISI limedokezwa kuwa majina 12 yamepatikana baada ya mchujo kutoka watu 30, ambao waliomba wadhifa huo ulipotangazwa.
Kamati maalum yenye wajumbe kutoka bodi ya wakurugenzi, wizara ya nishati na madini na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Idara ya Uhandisi) walitarajiwa kukutana juzi na jana (tarehe 9 na 10 Novemba, 2009) ili kufanya usaili wa watu hao 12 na kupata majina matatu ambayo yangepelekwa ngazi za juu ili mmoja ateuliwe kushika nafasi ya Dk. Rashid.
Habari zinasema kuwa Dk. Rashid ameonyesha nia ya kutokuendelea na wadhifa huo na wala hakuomba kuendelea, na hivi karibuni alituma waraka kwa wafanyakazi kuwashukuru kwa ushirikiano wao miaka mitatu aliyofanya kazi.
Ingawa baadhi ya watu wanasema Dk. Rashid alifanya kazi nzuri akiwa TANESCO na kuimarisha hali ya shirika kifedha, wengine wanasema shirika liliimarika kutokana na mikataba ya Aggreko na Alstom, ya miaka miwili kukamilika, mkataba wa Dowans kuvunjwa, IPTL kusimamisha uzalishaji umeme na TANESCO kukataa kulipa malipo yake ya capacity charges, hivyo shirika likaweza kupeleka fedha sehamu nyingine, licha ya mkopo wa Sh. 280 bilioni, ambao mwaka 2007 TANESCO ilichukua kwenye mabenki kadhaa, yakiwamo Stanbic, CRDB, Exim na National Microfinance (NMB).
Source: Mwanahalisi
HIVI TANZANIA TUMELOGWA???????