Kwangu mimi dini ninaipa nafasi kubwa sana japo wapo wengine huwa wanaichukulia kawaida na wala hawaoni kama yaweza kuwa kikwazo. Ila huwa najiuliza maswali mengi sana kati yake ni je mkianza mahusiano mkafikia hatua ya kuanzisha familia na mkabahatika kuwapata watoto je wenyewe watakuwa upande upi au wataabudu sehemu gani? Na hakika familia nyingi imara zenye upendo na amani ni zile zenye maadili ya kidini.
My point of view ni kuwa kama ni platonic relationship, dini sio issue. Lakini kama ni uhusiano wa longterm na hasa ule wa kujenga family, I believe the family that prays together stays forever.
thanx, Madamex but ingekuwa wewe umempenda mtu wa dini tofauti na hautaki kumpoteza ungechagua aina ipi ya uhusiano..na hasa ungekuwa umempenda kimapenzi zaidi na vile dini imekuwa kikwazo cha kuishi pamoja, je wewe ungekua tayari kubadili dini?
unachosema Aisha ni kweli, lakini mbona wahenda walisema mapenzi na mahususiano hayachagui dini wala kabila.. Swali:- mbona imekuwa rahisi kwa mwanaume wa kiislam kumuowa mwanamke wa kikristo ila inakua vigumu kwa mwanaume wa kikristo kuowa mwanamke wa kiislam, je ni alali kumuacha mtu umpendae kisa dini?
Jf imekua msaada mkubwa sana kwangu, nimebahatika kuwasiliana na watu wengi na wengine kufikia kuanzisha uhusiano ila nasikitika mara nyingi dini imekuwa kikwazo..kwani ahiwezekani watu wenye dini tofauti kuishi pamoja?