Chillipo
Member
- Mar 27, 2012
- 37
- 6
Katika Gazeti la Jana la Tanzania Daima lilikuwa na maelezo kuhusu vurugu zilizotokea huko Zanzibar pamoja na picha mchanganyiko wa vurugu hizo lakin cha kustua na kuhuzunisha ni kufanya mambo kinyume na taaluma ya uandishi wa habari kwa kuweka picha ambayo haikutokea huko zanzibar je mnafanya kazi kwa maslahi ya nani? nini mnachofaidika nacho kwan picha hiyo ilipigwa mwaka juzi huko Morogoro na mwenye picha mwenyewe jana amejitokeza redion na kukiri kwa ulimi wake kuwa hajawahi kufika Zanzibar hata siku moja.Picha yenyewe imepewe namba mbili kijana kashika kitambaa ukurasa wa kwanza swali langu mnafanya haya mambo kwa kutumwa na nani nyuma yenu mbona kila siku nyie pekee yenu tu ndio mnaopata malalamiko na kesi kuhusu habari zenu.KIBANDA nilikuwa nakuamini sana ila ninaanza kupoteza iman na uadilifu wako kabisa.Igeni mfano wa Gazeti la Mwananchi, Raia Mwema etc