Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,570
- 19,444
Nikukumbuka nilivyokuwa nawachukulia jamaa hawa wakati wakiwa wanaishi pale Mazimbu Morogoro kuwa ni ndugu zangu na kuwasaidia kila walipohitaji msaada kulingana na imani tuliyokuwa tumefundishwa na Nyerere kuwa binadamu wote ni ndugu zangu na afrika ni moja, ninapata uchungu kweli kweli. Ni wao waliosababisha kifo cha Sokoine wetu lakini imani ile tukaiweka mbele, halafu leo hii wao wanatuua kama wanyama!!!!