X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
Dawa Ya Mchungaji Ambilikile Mwasapile a.k.a Babu. Je Ni Ulaghai?
Asalaam Aleikum, Aman iwe nanyi...!
Wana JF, habari za miangaiko ya kila siku... Poleni na majukumu na miangaiko ya hapa na pale.
Leo nami nimeonelea kwa mara ya kwanza kutoa mchango wangu, kuhusiana na kadhia hii inayo endelea uko Loliondo. Japokuwa baadhi ya haya yaliyomo humu, nimesha yaeleza kwenye thread nyingine, lakini nimeonelea kuyaunganisha hapa, ili niweze kueleweka kwa watakao penda kuelewa.
Hizi habari za Mchungaji Mstaafu Ambilikile Mwasapile wa kijiji cha Samunge wilayani Loliondo, ambaye anajulikana kwa jina la umaarufu kama babu, zimechukuwa nafasi kubwa sana kwenye vichwa vya Watanzania wengi.
Mimi ni mmoja wa wengi ambao wanafuatilia habari zake kwa kina na ukaribu...! Huyu babu kwenye mahojiano yake... ameelezea kuwa yeye amepata mahono kutokwa kwa Mwenyezi Mungu na dawa yake inaponyesha baada ya siku zisizo pungua saba.
Kusema ukweli tumesikia mengi sana, kutoka kwa wadau mbali mbali...! Lakini kitu cha ajabu ni kwamba, wengi ambao wamekunywa hiyo dawa, hatuwasikii tena kwenda hospitalini au zahanati ya karibu, ili kupima na kujua afya zao zinaendeleaje? Yaani zimekuwa simulizi za mdomoni tu, kuwa fulani kapona na wengine wamediliki hata kujitaja wao binafsi kuwa wamepona na hali hawana uthibitisho wa kitabibu kuonyesha kuwa wamepona.
Vile vile kuna wadau wanao mtete, huyu mzee, ambaye mimi namwita Kinjeketile Ngwale wa karne hii ya 22. Wale walio soma historia ya vita vya majimaji, wanajuwa kilicho wapata wale wote waliokunywa na kujipaka ile dawa ya Kinjeketile... Dawa ambayo ilikuwa ni mchanganyiko wa mbegu za Mbarika na Mtama... Matokeo yake kila mtu anajuwa kilicho wapata wazee wetu wale. Ingawa hata Kinjeketile naye kuyapa uzito madai yake alidai kuwa ameoteshwa na Mwenyezi Mungu.
Ajabu ni kwamba, leo hii ni miaka 100 imepita tangia vita vile vipiganwe. Na hivi sasa tupo karne ya Sayansi na Technolojia, bado wapo watu wenye kuamini yale yale yalio wapata wazee wetu karne moja nyuma. Hawa wadau kila kukicha wao wanakuja sera mpya mpya za kumtete huyu mchungaji mstaafu...!
Matokeo ya hii dawa ya huyu mchungaji, yameanza kuonekana kwa wengi, kuna ambao wamezidiwa na maradhi wakakimbizwa hospitalini na wale wasio na bahati wamepoteza maisha. Kwangu mimi naona kuwa ni uzembe na ujinga wa makusudi, ulio sababishwa na wao kuacha kula dawa za hospitalini wakitarajia miujiza ya uponyaji kutoka kwa huyu mzee.
Licha ya watu kupoteza uhai, bado kuna ambao wanamtetea...! Utawasikia wakisema "Oooh babu hazuii kifo..!" Ndio tunajuwa kuwa hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzuiya vifo... Hata hao mitume tunao waamini kwenye dini zetu, ziwe za jadi au hizi ambazo tuna ziita za kimapokeo, hawakuwa na uwezo wa kuzuiya watu wasife... Lakini kama vifo vinatokana na uzembe na ujinga wa makusudi kwa kuacha kula dawa zenye kukuongezea uhai, mnataka tuwaeleweje?
Sasa tunasikia tena kuwa watu wasiache kula dawa zao, japokuwa wamepata kunywa dawa za Kinjeketile Ngwale wa karne hii ya ishirini na mbili... Kulikoni tena?
Hao waliokwisha kunywa dawa mpaka leo hatusikii wakisema kuwa wamekwenda kupima... Wanaogopa kitu gani...!? Utawasikia wakijisifia kuwa wamepona kwa kujiangalia kwenye kioo...! Na hali maradhi yanawatafuna ndani kwa ndani...!
Mwisho hao watetezi watakuja na utetezi mpya kuwa wale wote ambao hawakupona hawana imani ndio maana dawa ya babu Kinjeketile haikufanyakazi...!
Hivi hao waathirika waliozidiwa baada ya kuto endelea na dawa zao za mahospitalini, watajisikiaje watakapo simangwa kwa kushutumiwa kuwa hawakupona kwa kuwa hawana imani...! Je hamuoni ni kuwazidishia maradhi zaidi?
Hivi anayetakiwa kuwa na imani hapa ni nani mgonjwa au babu kinje...! Yeye si ndiye aliye dai kuwa kaoteshwa na mungu na dawa yake inaponyesha maradhi yote...!? Hivi Mwenyezi Mungu anapoleta Neema huwa anachaguwa wa kumpa? Au huwa anawapa hata wale wasio muamini?
Hivi ni kweli uwezi kupona mpaka huwe na imani ...!? Inaingia akilini kweli?
Mbona tunasoma kwenye maandiko ya biblia kuwa kuna watu waliponywa na wala hawakuwa na hiyo imani...! Na wengine walifufuliwa...! Je wale walioponywa na kufufuliwa na Nabii Elisha...! Walikuwa na imani? tena wengine walifufuka kwa kugusa mifupa ya manabii tu.
Jamani tuwache kushabikia vitu ambavyo haviwezekani kwenye karne hii... karne ambayo mwenyezi Mungu ametujaalia utaalam wa kutengeneza madawa ya kutibu maradhi mbali mbali...! Kinacho wafanya watu wasitumie hiyo miujiza ya kunywa dawa mahospitalini ni kitu gani kama si ulimbukeni na kutafuta njia za mkato ni nini...!? Kwani hizo dawa za mahospitalini hazina baraka za Mwenyezi Mungu!?
Hivi tunamwambia nini Mwenyezi Mungu siku ya hukumu... Na hali ametupa akili na tunashindwa kuitumia... Hivi ni neema gani zaidi ya kutumia akili zako na kutambua kuwa hapo Lolly hakuna uponyaji zaidi ya kuwapumbaza watu kwa kivuli cha imani!?
Mara nyingi ni vigumu sana kushindana na wajinga, watakushinda tu...! Watakusumbua na hoja zao za kijinga na kukushusha mpaka ufikie level yao...!
Kisha watajiona kuwa wao ni mahodari na kuanza kujisifia na hali wanaona kuwa ujinga wao umepelekea maangamizi ya ndugu, marafiki na jamaa zao wenyewe...!
Ukiwauliza haya mambo yamekuwaje... Hawakosi hoja hata siku moja...! Utawasikia wakisema "Aaah wale, wale wamekosa imani ndio maana hawakupona, unatakiwa umkiri bwana kwanza..."
Jamani hivi hakuna viongozi wa dini ambao wamefariki kwa maradhi ya kutibika, lakini wakafariki? Je hawakuwa na imani!?
Msije sema kuwa hatukuwaonya na kuwatahadharisha na hatari iliyoko mbele yenu...! Sisi tunawapenda zaidi ya hao ambao wanao wapeleka kwenye mdomo wa mauti, uko mnakoenda hakuna uponyaji, bali kuna mauwaji...!
Nawapa pole sana ndugu, jamaa na marafiki wote walio athirika kwa njia moja au nyingine, nawataka wasikate tamaa na kujiona kuwa imani zao ni haba, bali wanapaswa kurejea kutumia dawa zao za mahospitali, na kufuata masharti ya madaktari na wauguzi wao...!
Namuomba Mwenyezi Mungu awarejeshee afya na siha njema wale wote walio taabika kwenda uko Lolly, ili waweze kurejea kwenye furaha kama zamani... Na wale wenye kutumia dawa za HIV na kisukari basi wasiwache kutumia dawa zao kwa matumaini hewa na ya kilaghai, waswahili tuna msemo wetu mmoja kuwa "Kupotea njia ndio kujua njia", basi msikate tamaa, rejeeni dawa zenu ili muendelee na maisha, sisi wote tunawapenda.
Nawatakia siku njema.
Amani ya Mwenyezi Mungu hiwe nanyi.