Darasa la saba aukwaa u-DC

mhe. kanyunyu una hakika na ulichokiandika? bw. maneno alikuwa mbunge wa jimbo la chalinze katika bunge lililopita na minimum qualification ya ubunge ni elimu ya kidato cha nne, ni vipi angeukwaa ubunge bila kuwa na elimu hiyo. kumbuka huyu aligombea na omary madega kwenye kura za maoni ndani ya ccm mwaka 2005 ambaye kwa vyovyote asingenyamaza angemlipua tu maneno kama kweli ni darasa la saba. bunge lililopita mbunge pekee aliyefahamika kutokuwa na elimu ya kidato cha nne ni samwel
naomba kuuliza mkuu..majimarefu na deo sanga(jah people)..wamefika 4m 4..?
 
Ndugu wana jamii katika kile kinachoonekana kulipana fadhila ndani ya serikali hii, aliyekuwa mbunge wa chalinze 2005-2010 RAMADHANI A MANENO, alishindwa vibaya kwenye kura za maoni mwaka 2010 baada ya kuwadanganya wapiga kura wake kwamba angejiendeleza kielimu,na hakufanya hivyo, mpaka anateuliwa mkuu wa wilaya ya KIGOMA elimu yake ni DARASA LA SABA_____________TAFAKARI.

mkuu jitahidi kuwa na data ili ujenge hoja.huyu jamaa sio darasa la saba,nakumbuka alimaliza diploma cbe then akiwa mbunge alikuwa anasoma chuo cha ustawi wa jamii-night college akichukua degree.
 
Nini darasa la saba, Maji Marefu kaishia darasa la pili na leo hii ni mbunge tena wa kuchaguliwa na wapiga kura kuliko huyo alyezawadiwa. Ukishangaa ya Mussa..............!
 
Kabla ya kupata ubunge alikua anafaya kazi TRA lakini hakufika ngazi ya kuwa officer, he was just a clerk (motor vehicle registration), lakini alijiendeleza kidogo chuo cha biashara (CBE) akapata certificate ya business administration. Alipokua TRA alijihusisha sana na usajili wa magari ambayo hayakua na uhalali wa kusajiliwa.
 
Mkuu haya mambo ndio yanayoiua nchi hii. Cheo cha DC kwa asili yake kina majukumu makubwa sana. DC ana mamlaka yanayompita hata RC unless Job description zao zimebadilishwa ila nijuavyo DC ana mamlaka hata ya ku-declare kutomhitaji mtu katika wilaya yake na huyo mtu akaondolewa wilayani humo ndani ya saa 48.
Mvurugano ulikuja kutokea pale cheo hicho kilipopewa mtazamo wa kisiasa zaidi in the 70s kwa kuwaita Area Commisioners instead of DCs. AC akawa vested na majukumu ya Katibu wa Wilaya wa TANU then CcM.
Tunahitaji wachambuzi wa masuala ya kisiasa waliobobea kama Jenerali Ulimwengu na Joseph Mihangwa kutupambanua waTZ kuwa kwa kupuuza cheo hiki cha DC na kuegeme sifa za udugu na uwezo wa mtu kuigiza (mockery traits) tunaiua nchi hii.
Nakumbuka huko nyuma tuliona watu wa Std. VII Failures wakiteuliwa kuwa DC eti kwa vile tu ya kuwa wahamasishaji wazuri wa mikutano ya chama. This riduculousy shouldn't be allowed to continue/go on unabated.
Itoshe tu kuwa huko nyuma tumewahi kuwa na darasa la saba wenyekiti wa UV-CCM Taifa two times; Masanje na Guninita na baada ya kuachia cheo hicho wateuliwa kuwa DC na wakashindwa kazi. Leo hii ni wenyeviti wa CcM wilaya na mkoa respectively.
 
elimu siyoigezo lakini kwa upand emwingine haswa kwa science and technology inabidi darasa liwepo nje yahapo atandanganywa sana
 
Ndugu wana jamii katika kile kinachoonekana kulipana fadhila ndani ya serikali hii, aliyekuwa mbunge wa chalinze 2005-2010 RAMADHANI A MANENO, alishindwa vibaya kwenye kura za maoni mwaka 2010 baada ya kuwadanganya wapiga kura wake kwamba angejiendeleza kielimu,na hakufanya hivyo, mpaka anateuliwa mkuu wa wilaya ya KIGOMA elimu yake ni DARASA LA SABA_____________TAFAKARI.

Mmmh! Sasa hapo unashangaa nini, huyo mbona ni MPWAE kabisa na mkulukulu...! 1+1=3
 
Ndo maana amepelekwa KIGOMA,,,,,NO CHALLENGES OVA THERE
..Mh!! Sidhani ungejaribu kumuuliza the former RC. Joseph Simbakalia anajua alichokumbana nacho kigoma!!! Si rahisi sana kama unavyofikiria..
0
 
Darasa la saba sio mtu? Sio raia? MGombea mwenza CHadema 2010 alikuwa pia darasa la saba!!!! KUNYA ANYE KUKU...AKINYA BATA KAHARISHA....!
 
Kwa hali kama hii kupata maendeleo itakuwa ndoto! Hawa watu wana ushawishi mkubwa katika maamuzi, kwa bahati mbaya wanashinikiza hoja bila ya kujua madhara yake i.e wanatumia uzoefu. Mfano, Diwani, Mwanyekiti wa Kijiji ambaye hajasoma, ila anashinikiza aina fulani ya uongozi wa shule au kupanga miradi, majukumu ya wazazi n.k. Inafaa wenye elimu waachiwe nafasi za maamuzi. Hata Aristotle (Mwanafalsafa) alipendekeza hivyo. Tanzania tunaenda kinyume
 
Wanasema huko hakuna kazi ya kutumia taaluma yeyote ndiyo maana ata ukiwa os wa ofisi kuteuliwa kuwa DC sio tatizo cha muhimu uwe mwanachama mtiifu wa CCM

Tena utendaji wa kazi utategemea maagizo yote kutoka magogoni.
 
Yaani JK alivyoshusha hadhi ya ma-DC mpaka nawaonea huruma. Walikuwa wanajisikia sana hao jamaa.......... sasa JK kawaweka wanapostahili. Ikifikia wananchi wanamkataa DC hata kabla hajawasili kuanza kazi then ujue kuna tatizo.
 
Huyu jamaa alimaliza degree ya social works mwaka 2010 pale chuo cha ustawi. Tuandike vitu baada ya kufanya utafiti. Sio kila mtu aliyeteuliwa hana uwezo. Au ulitaka uteukiwe wewe.

Ni kweli kabisa jamaa ana bachelor degree ni social work kwa tuwe tunaandika vitu tulivyo na uhakika.
 
Huyu jamaa alimaliza degree ya social works mwaka 2010 pale chuo cha ustawi. Tuandike vitu baada ya kufanya utafiti. Sio kila mtu aliyeteuliwa hana uwezo. Au ulitaka uteukiwe wewe.

sina uhakika na uwezo wake wa kuongoza lkn kuhusu chuo Ni kweli kabisa jamaa ana bachelor degree ni social work na sio darasa la saba tuache upotoshaji kwa hyo tuwe tunaandika vitu tulivyo na uhakika.
 
Wana bodi kwa mfumo tunaoenenda nao tukiongozwa na CCM,sion kama kiwango cha elimu ni kipimo cha utendaji kazi bora na wenye tija kwa taifa,mifano ni mingi sana,tuna maproffesor,kuna viongozi wa master,1st degree na ghasia nyingi tu,laikin je input ikoje?kwa mfuomo wa ccm hii sioni tofauti katika utendaji kati ya mwenye elimu ya juu na ase na elimu,bado elimu za watanzania hazijawa ni kipimo katika kutenda kazi zenye tija tukiwa na CCM hii.na mbona ni wengi tu.Ni mpaka hapo mfumo wa utawala utakapobadilishwa.
Hao wote walioteuliwa ama kuchaguliwa kuwa ma-DC kwani hamjui ya kuwa wanaenda kufanya kazi za chama cha magamba?kuna elimu gani inahitajika?wapo watendaji wanatamfanyia kazi kumbukeni kuna DAS na bado upande mwingine kuna DED yeye huyu maneno anakwenda kufanya maneno ya magamba tu,elimu yake inatosha sana.
 
Alisoma wapi lete CV yote itapunguza chumvi

CV ya nini iletwe wakati haombi kazi? Huyo ameshateuliwa tayari na DC siyo kazi ya ujuzi. Ingekuwa ule wa kikoloni wakati DC akiitwa 'Bwana Shauri' ni lazima awe mwanasheria na awe Graduate wa Manchester au Oxford University.

U-DC sasa hivi ni nafasi ya kufarijiana.
 
Back
Top Bottom