tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,852
- 18,261
Naingia kwenye mada moja kwa moja. Mvua kubwa sana inanyesha hapa Dar sijapata kuona. Tangu nizaliwe sijawahi kushuhudia mvua kubwa kiasi hiki.
Serikali ijiandae kukabiliana na athari za mafuriko zitakazosababishwa na mvua hii kwani kadri muda unavyoenda mvua inazidi kuongezeka
Mara ya mwisho mvua iliponyesha ilingo'a madaraja na kuua watu watatu. Safari hii tujiandae kwa maafa zaidi.
Tuambie mahali ulipo hali ikoje na nini tutarajie baada ya mvua hii.
Pia soma: Mvua ilivyoacha maumivu mmoja adaiwa kufa Dar
UPDATES
*Mawasiliano kati ya Tegeta na Kunduchi yamekatika baada ya daraja la Kunduchi-Mtongani kukatika. Magari, nyumba na mali za raia zimesombwa na maji. Nguzo za umeme zimeanguka na baadhi ya raia wamefariki. Tatizo watu wamejenga karibu na mto kwa kupewa vibali na maofisa ardhi wa Serikali.
*Hadi sasa mvua inaendelea kunyesha baadhi ya maeneo hapa Dar. Serikali itoe tahadhari kwa wananchi na ichukue hatua kukabiliana na mafuriko.
*Serikali inaendelea kufanya tathmini ya uharibifu na hasara iliyojitokeza. Madhara ya mafuriko haya mpaka sasa ni kama unavyoyasikia kutoka kwenye rekodi hapo chini iliyoripotiwa na Radio One Stereo. Katika rekodi hii utamsikia mwananchi akilalamika kupoteza Tsh 5,000,000 ambazo zote zimesombwa na mafuriko. Hakufanikiwa kuokoa hata shilingi moja.
* Nyumba 7, magari na mali za wananchi zimesombwa na maji, mtu mmoja amefariki na madaraja kadhaa yamevunjika na kukata mawasiliano ya barabara.
*Raia mmoja ameokota gari lillilosombwa na mafuriko lakini watu wenye roho mbaya wamemzuia kulichukua.
*Wakandarasi wanaendelea kuzibua barabara zilizozibwa na maji, mawe na magogo ili kurejesha mawasiliano.
Nitaendelea kuwapa updates na picha kadri nitakavyozipata.........
Serikali ijiandae kukabiliana na athari za mafuriko zitakazosababishwa na mvua hii kwani kadri muda unavyoenda mvua inazidi kuongezeka
Mara ya mwisho mvua iliponyesha ilingo'a madaraja na kuua watu watatu. Safari hii tujiandae kwa maafa zaidi.
Tuambie mahali ulipo hali ikoje na nini tutarajie baada ya mvua hii.
Pia soma: Mvua ilivyoacha maumivu mmoja adaiwa kufa Dar
UPDATES
*Mawasiliano kati ya Tegeta na Kunduchi yamekatika baada ya daraja la Kunduchi-Mtongani kukatika. Magari, nyumba na mali za raia zimesombwa na maji. Nguzo za umeme zimeanguka na baadhi ya raia wamefariki. Tatizo watu wamejenga karibu na mto kwa kupewa vibali na maofisa ardhi wa Serikali.
*Hadi sasa mvua inaendelea kunyesha baadhi ya maeneo hapa Dar. Serikali itoe tahadhari kwa wananchi na ichukue hatua kukabiliana na mafuriko.
*Serikali inaendelea kufanya tathmini ya uharibifu na hasara iliyojitokeza. Madhara ya mafuriko haya mpaka sasa ni kama unavyoyasikia kutoka kwenye rekodi hapo chini iliyoripotiwa na Radio One Stereo. Katika rekodi hii utamsikia mwananchi akilalamika kupoteza Tsh 5,000,000 ambazo zote zimesombwa na mafuriko. Hakufanikiwa kuokoa hata shilingi moja.
* Nyumba 7, magari na mali za wananchi zimesombwa na maji, mtu mmoja amefariki na madaraja kadhaa yamevunjika na kukata mawasiliano ya barabara.
*Raia mmoja ameokota gari lillilosombwa na mafuriko lakini watu wenye roho mbaya wamemzuia kulichukua.
*Wakandarasi wanaendelea kuzibua barabara zilizozibwa na maji, mawe na magogo ili kurejesha mawasiliano.
Nitaendelea kuwapa updates na picha kadri nitakavyozipata.........