Mhache
JF-Expert Member
- Jun 20, 2008
- 345
- 24
Je! Hii si hujuma za TANESCO? Siku chache zilizopita kulikwa na malumbano kati ya TANESCO na kampuni ya DOWANS kuhusiana na serikali kutaka kununua mitambo ya umeme kutoka kampuni hiyo. TANESCO walitishia kwamba nchi itakumbwa na giza. Na sasa mkwara huo umetimia. Mimi hainiiingii akilini? Hii ni hujuma inabidi serikali ifanye utafiti wa kina kujua uhalali wa DAR kuwa gizani masaa nane kwa siku. Je wanajamii forum mna maoni gani?
Nawatakia kila la heri katika wakati huu mgumu wa kuwa gizani masaa nane kwa siku. Hii itakuwa ni baraka kwa vibaka hasa maeneo ya Manzese, Tandale na kwa Mtogole. Kufa kufaana.
Nawatakia kila la heri katika wakati huu mgumu wa kuwa gizani masaa nane kwa siku. Hii itakuwa ni baraka kwa vibaka hasa maeneo ya Manzese, Tandale na kwa Mtogole. Kufa kufaana.