Huo sio usemi wa kiongozi makini hata kidogo. Kwa usemi huo hata Katiba ya sasa haina maana kwani haijengi zahanati.Katibu mkuu wa CCM hataki Tume Huru ya Uchaguzi kwa sababu haileti chakula! Hivyo anataka kuendelea na tume iliyopo ili CCM iendelee kubaki madarakani kwa sababu anadai Tume Huru ya Uchaguzi ni ya wanasiasa kuwekwa madarakani.
Kwa akili hizi za viongozi wa CCM bado tuna safari ndefu kupata viongozi watakaochaguliwa na wananchi.
View attachment 1889286