Cuf and company kukimbilia viti vya chadema ni kieleelzo cha usaliti wao

jana wakat wabumge wa chadema wanatumia haki yao ya kikatiba kumsusia rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania ambaye wanaamini kuwa hakupatikana katika uchaguzi huru na wa haki, wabunge wa vyama vingine hususan cuf n.k vyenye viti 8 tu tanzania bara kwa pamoja (cuf 2, nccr , tlp 1 na udp 1) walionekana haraka haraka wakikimbilia kujaza viti vya wabunge wa chadema ili kuepusha aibu hiyo.

Nafurahi kitendo hiki kimetokea wakati ambapo mjadala uundwaji wa kambi ya upinzani ukiwa bado mbichi kabisa; ambapo waliokuwa wakitetea kushirikishwa kwa vyama vingine katika kambi hiyo natumai wamejionea wenyewe namna ambavyo wawakilishi hao wanavyoshiriki kuunga mkono kuendelea kuwepo katiba ya sasa katika mfumo na maudhui yake pamoja na tume ya uchaguzi isiyokuwa huru.

Kilichonifurahisha zaidi ni kitendo hicho kuweka mpaka vichwani na mawazoni mwa wananchi kuwa ni chama gani kipo kwa maslahi mapana zaidi ya taifa na watanzania na vyama gani vipo kwa ajili ya kutumiwa na ccm kujinda katiba na tume huru isiyokuwa huru; na kwa maana hiyo ufukara na umaskini na kukua kwa matabaka miongoni mwa watanzania.

Kwa kumsusia rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania aliye zao la katiba na tume ya uchaguzi mbovu, chadema imeungana na 51.2% ya watanzania waliojiandikisha kupiga kura lakini wakasusa kujitokeza kupinga mambo mbali mbali ikiwemo katiba na tume mbovu. Ukichanganya na 26% aliyopata dr slaa baada ya kuchakachuliwa utagundua kuwa wabunge wa chadema walikuwa wanawawakilisha takribani 77% ya watanzania waliojiandikisha kupiga kura ikilinganishwa na ccm na mhe jakaya kikwete amabye alikuwa akiwawakilisha 27% tu ya waliojiandikisha kupiga kura.

Big up chadema!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

CUF hawawezi kuipinga serikali yao wenyewe, na hadi sasa hatuna chama cha upinzani kinachoitwa CUF maana ni sehemu ya CCM, maana tumeona wana CUF wakiacha kugombea nafasi bungeni kwa madai ya kuimarisha mshikamano wao na CCM
 
Mimi sioni sababu ya kuhanagaika na CUF, sisi nyumbani kwetu CUF ni chama kinachodharaulika mpaka basi. Ukionekana unatembea kwa mguu kwa muda mrefu watakutania kuwa unaenda mwendo wa CUF maanake kwa mguu. Nilikuwa na waona wazee wa CUF kijijini kwetu hata wale ambao walikuwa wakristo walilazimika kuvaa vibandiko vyeupe ili wafanane na CUF . Kumbukeni hawa wote ni waswahili,.... bwana mambo ya kwenye gahawa ndo yanaendesha nchi.

CUF kamwe haiwezi kuungana na Chadema maana hawafanani na IQ zinatofautiana kwa mabli mno, za CUF zinaweza kufanana na za CCM ndiyo maana wanaweza kuelewana. Inashangaza Sharif kasahau yote aliyofanyiwa na CCM wakati ule amewasaliti wanawake walioba...... kwa kupata cheo kisichokuwa na kichwa wala miguu.
Hawa ndo waswahili bwana wanaridhika kwa chai na chapati tuuuuuuuuuuu.
 
. Mauaji ya Wete 2001

Katika chaguzi za vyama vingi tangu mwaka 1995 wakazi wengi wa Wete jinsi wakazi wa Pemba kwa jumla walipendelea chama cha CUF. Kiongozi wa CUF Seif Shariff Hamad ni mwenyeji wa Wete. Baada ya uchaguzi wa mwaka 2000 wafuasi wa CUF waliona ya kwamba kura haikuwa ya kweli na tar. 27 Januari 2001 maelfu ya wananchi walikusanyika Wete kudai uchaguzi urudiwe.
Askari za Polisi walikuwa na amri kuzuia maandamano yalivunjwa na polisi kwa ukali mkubwa. Waandamanaji angalau 13 waliuawa, watu 213 walijeruhiwa na zaidi ya 400 walikamatwa. Polisi pamoja iliendelea kutafuta wapinzani katika siku zilizofuata kuna taarifa ya kwamba watu wengi walipigwa na wanawake kunajisiwa. Zaidi ya watu 2,000 kutoka Pemba walikimbia Kenya kwa maboti madogo walipoishi katika makambi hasa shimoni.[/QUOTE]

...Kwa kweli CUF wamesononesha wengi.....nani asiyejuwa namna vyama vyote vya upinzani walivyoiunga mkono CUF wakati wanadai haki yao.........,nani asiyejuwa namna wanachama wa CUF bara ...wakiiongozwa na James mapalaa ,Mugeni musobi na sasa Lipumba walivyojitoa kukijenga chama.....leo hii CUF wamepewa umakamu wa rais [pamoja na kuwa walishinda ].....na kati ya mawaziri takribani 20 [wakiwemo wasiokuwa na wizara maalum]...CUF wamepewa wizara 6 ..... lakini matokeo yake wameridhika na kusahau wanachama wake walio upande wa pili......huu ni uchahidi wa wazi kuwa CUF hawawezi kutetea lolote la Tanganyika .....

CUF imewatumia wanachama wake bara kama wasukuma gari ....limewaka wamewaachia vumbi tu...ni wazi kuwa ni vigumu chama hiki kuaminika tena tanganyika ...wamekubali kuuliwa na CCM....wanachama wake walio bara wajuwe wameachwa kwenye mataa ....watafute chama kipya wakijenge iwapo wataona CHADEMA haiwafai kuna vyama kama NRA na UMD na vingine vingi tu ambavyo vipo dormant.....pateni picha juzi maalim ameingia ofisi kuu za CUF buguruni ......hata kuingia ndani ilikuwa taabu..amesahau haraka mazilla aliyoyapita.....akila miogo na wapambanaji wake pale buguruni na kulala star light hotel......

NCCR MAGEUZI ...wanao vijana wazuri sana kina Kfulila na Mtakamali etc ....hawa vijana siwalaumu sana najuwa wajo under pressure ya watu kama kina Mbatia......lakini bila hivyo naamini kuwa wanaamini kwa kile kinachopiganiwa ...TLP na UDP pale ni maslahi tu!!!
 
Ndoa ya mkeka inawasumbua, ngoja wapewe talaka

Hawa watakaposhindwa hii ndoa sijui watafanyaje.....ningekuwa mimi maalum ...ningekuwa kimya bila kutoa comment...au ningetumia nafasi hii kupromote CUF bara.....nadhani watu walio makaburini wanazunguka hawaamini hasa wale waliouwawa Pemba ,,..wale waliokimbilia shimoni mombasa,waliopinduliwa kwa mamia na boti [hii siri inajulikana waliokufa walikuwa wengi]
 
kk Jk mwenyewe mzinifu sasa unafikilia mzinifu uwa anongeaga point
sasa uo udini ukwapi mbona atuuoni yeye na sheikh wa hukle masjidi ndio waliuanzisha
 
Kwa jinsi nilivyowadharau CUF, hakuna kipimo cha kupima, wameonyesha uozo wao mbele ya uma wa watanzania, wamejiua wenyewe
 
Mkuu nami jana nilitaja kama wewe,ivi inaingia akilini kwamba watz waliodanganywa kukesha wakilinda kura na wakatiwa nguvuni na kukaa kolokoloni alaf leo Seif na hamad wanaungana na wakoloni weusi kuendelea kutunyanyasa kwa kuodhi mali za umma,kupora viwanja na kujimilikisha maliasili,kukaa na katiba mbovu,leo hii wanakaa kuchekelea si tukingali matatani. Jeikeie anasema wapinzani wataenda watarudi tu,hawana wa kumlilia matatizo yetu isipokuwa mimi,jkei na serikali ya sism,huu si udikteta?anakemea udini bungeni,ivi udini uko kwa nani mbona mtaana shwari tu tuko pamoja? Jamaa ana matatizo makubwa,anazidi kuonesha IQ yake ilivo.

JK aposema wataenda lakini mwisho watarudi, anajua watarudije?????
 
kk Jk mwenyewe mzinifu sasa unafikilia mzinifu uwa anongeaga point
sasa uo udini ukwapi mbona atuuoni yeye na sheikh wa hukle masjidi ndio waliuanzisha

Udini nchi hii ulianza pale waliposema "huyu kijana kama hali ni hii atatupeleka pabaya...!" kijana akajibu "...huyu shehe ni mtakadini" huo ndio ulikuwa mwanzo wa udini! kwa maana mzee yule alifanya hesabu za kutoa kwa kujumlisha huku akizisoma alama za nyakati!:teeth:
 
Back
Top Bottom