CRDB ni Moja ya Benki zenye huduma mbovu sana

baadhi matawi mameneja wanakaa sana wengine hawana elimu ya umeneja kwa mfano tawi la dodoma meneja huyo huyo toka ilipoanzishwa bank hiyo
 
Hii benki mwanzoni nilikuwa nikisiakia watu wanailaumu naona kama ni majungu ila nimekuja kuprove kwamba CRDB huduma zao sio nzuri kabisa, Nimefuatilia ishu ya simu benking wiki nzima sasa na wakati najaza fomu niliambiwa ni masaa 48 na kibaya zaidi ni uongo wa wafanya kazi wao kila kitu wanasingizia systeam ilikuwa mbovu, hata kalamu ikiisha wao ni systeam ilikuwa mbovu.

Unajaza fomu wanapoteza inabidi tena ujaze upya fomu, kwa kweli wajirekebishe.
Hapo kwenye RED ngoja nimpigie simu Charles Kimei kama ni kweli!
 
Sikumbuki kama nilijaza form ya kuomba kuunganishwa na simbanking, nakumbuka niliomba tu kwa simu na nikawapigia simu wakanipa maelezo kidogo hadi leo natumia simbanking na mwisho wa mwezi natumiwa statement kwa mail kuonyesha jinsi mpunga ulivyoteketea. Mtoa mada nakuomba ujaribu kuwasumbua kwa simu, achana na mambo ya kwenda kuonana nao face to face, naamini utafanikiwa ndani ya muda mfupi.

Mkuu hata mm niliuna e statement na Sim banking siku hio hio bila kujaza form,ila ilikua zamani sahivii ndo kamawasemavyo wadau uzembe mwingi na steps nyingi pia...ishu mfano ya ATM card unaambiwa urudi kwa branch ulofungulia sasa si ujinga huuu??
 
Kaka huu ni mwaka wa sita napokea pesa kwa njia hii... wire transfer haihitaji chochote zaidi ya jina la account, account namba jina la mtu mwenye account, adress yake, jina la bank na branch yake, swift code ambayo kwa CRDB ni CORUTZTZ...wanachelewesha sana hela hawa ni uzembe wa kitengo kinachopokea hizo transfers...hivi kwa miaka sita yote details za account yangu zimekosewa????

Kwenye Bank yangu, kama natumiwa pesa kutoka USA correspondence bank ni Citi bank USA, nikitumiwa hela kutoka Europe correspondence ni HSBC. Haichukui 12 hrs, amount imeshaingia kwenye account yangu. Waambie wakupe full details.
 
Dah! Nilidhani hawa wana nafuu kumbe ndo wale wale tu.

Oh well...we're screwed, I guess.
 
Kwangu mimi wanachoniboa ni kutokuwepo hela kwenye ATM siku za weekends. Yaani siku ambazo watu tunakwenda shambani tunahitaji hela, wenyewe utakuta ATM zao hazina hela. Huwa nakereka sana.
Ila kwa huduma nyingine naona wanajitahidi, though NBC kwa sasa imeanza kufanya vizuri in terms of huduma hasa baada ya kukimbiwa kwa kasi na wateja.
Wanapitia wakati mgumu sana sasa ivi kifedha (nikimaanisha liquidity) sio wanaishiwa ktk ATM ni wanamanage liquidity yao kihuni hawana maana. Haiwezekani ATM nyingi kiasi hicho zinakosa hela kila j2 haijalishi mwanzo wa mwezi au lini.
 
binafsi card yangu ilisha muda wake nilitakiwa nipige picha upya....nijaze fomu upya......kwa gharama zangu.....folen ndefu ya kusubiri huyo mpiga picha wao.....tangu siku hiyo.....si mteja wao tena....pesa yako usumbufu wa nin?mbona bank nyingine id ikiisha muda wako unaenda kwenye tawi lako unapewa id mpya bila usumbufu!mim si mteja wa hiyo bank.....wanaboa!
 
Mkuu hata mm niliuna e statement na Sim banking siku hio hio bila kujaza form,ila ilikua zamani sahivii ndo kamawasemavyo wadau uzembe mwingi na steps nyingi pia...ishu mfano ya ATM card unaambiwa urudi kwa branch ulofungulia sasa si ujinga huuu??

Kama ni hivyo basi kumbe mabo yamebadilika, sasa inakuwaje labda ulifungulia Mtwara na sasa uko Bukoba au umefungulia Arusha na sasa uko Sumbawanga si kutafutana ubaya tu hapo.
 
Huenda hujajaribu NBC ukaona ubovu wa huduma uliokithiri zaidi mno.

As to me, CRDB ni benki yenye huduma bora na nzuri pengine kuliko benki nyingine zozote hapa nchini...

Kuwa na huduma bora kuliko nyingine haimaanishi kuwa ina huduma nzuri, utajilinganishaje afya yako na mgonjwa?
Wote mmeongea point ila nimependa hii ya wooden flag, kwa jumla CRDB kiaina wanajitahidi kwa viwango vyetu vya kibongobongo kwa kufanya comparison na wengine hasa kwa sie wananchi wa kawaida tusioweza kufungua a/c Bank M. Hiyo issue ya simbanking mbona wengine ilikuwa faster mno na information tunapewa kupitia kwenye email na huduma kama balance
 
mkuu kiukweli sijakuelew kwa upande wangu banki inayoongoza kwa huduma nzuri Tanzaniaf Crdb na hili halina ubishi yaani ni kama vile kujiuliza umevaa nini wakati. upo bafuni unaoga
 
mkuu kiukweli sijakuelew kwa upande wangu banki inayoongoza kwa huduma nzuri Tanzaniaf Crdb na hili halina ubishi yaani ni kama vile kujiuliza umevaa nini wakati. upo bafuni unaoga

Wewe hujapata shida that is why, ila kwa CRDB nisha pata matatizo kibao, na hili la juzi kati ndo limenifanya niandike na hapa ni katika kuwafanya wajirekebishe,
 
Mkuu Eddy,
Changamoto zote hizo ni kwa kila Bank, ninachojua kuna idara tofauti tofauti na kila moja ina majukumu yake. Kuna idara inahusika na ufunguaji na account tu. Kuna idara ya Credit, inajishughulisha na mambo ya mikopo na kuna idara ya customer service, wanahusika na kuwaelekeza wateja wapi waende kujipatia huduma kutegemeana na hitaji lake. Hilo la Tellers kujihusisha na whatsup sina uhakika sana, ila ninachojua kuna miamala ya Mpesa, tigopesa nk. Kama kweli lipo inabidi management wawazuie haraka sana.

Ni kweli kuna idara tofauti ila wote wapo katika banking hall moja, mteja anavamia yeyote kwani hajui yupi anahusika na nini, wakati wa nbc ya zamani ilikuwepo forex house wateja wa pale walikuwa vibopa tu.

unayosema kuhusu bankM ni kweli wao wameamua kuwa na wateja wachache wanaoweza kuwahudumia vizuri ndio traditional business yao, citi group na absa usitizame tawi moja tazama kutokea global HQ, ukiitizama huku utaona kama bank ndogo kumbe ni one of the giant bank.

kwa sasa ilivyo ikipata mtikisiko kidogo kilio chake kitakuwa kikubwa kwani mayai yote yapo katika kapu moja, mwanzoni nilishauri ijitanue nje ya Tanzania nadhani kimei alinisoma, sasa hivi tawi lake la Burundi linafanya vizuri sana.

Pia ikiweza kubadilika na kuwa "group of companies" inaweza anzisha "merger and acquisition" kwa kuzinunua bank ndogondogo zinazofanya vizuri katika soko na kuhamishia kule baadhi ya service badala ya zote kuwa katika banking hall moja.
 
Hapo sikuuingi mkono. Corporate wa Bank M ni wa kuhesabu. Ukienda Citibank ndiyo kabisa RM mmoja anaweza kuwahudimia. Hata staff wenyewe hawaruhusiwi kuwa na account wanapofanyia kazi. Bora ulinganishe corporate customers wa NBC,NMB na CRDB.

huu utaratibu wa kuzuia wafanyakazi wasiwe na account wasiingie na simu kazini unasaidia kuleta nidhamu na concentration kazini badala ya kubadili counter kuwa sehemu za kupigia dili.
 
Hii benki mwanzoni nilikuwa nikisiakia watu wanailaumu naona kama ni majungu ila nimekuja kuprove kwamba CRDB huduma zao sio nzuri kabisa, Nimefuatilia ishu ya simu benking wiki nzima sasa na wakati najaza fomu niliambiwa ni masaa 48 na kibaya zaidi ni uongo wa wafanya kazi wao kila kitu wanasingizia systeam ilikuwa mbovu, hata kalamu ikiisha wao ni systeam ilikuwa mbovu.

Unajaza fomu wanapoteza inabidi tena ujaze upya fomu, kwa kweli wajirekebishe.

And vice versa is true@ChashaPoultryFarm hakuna bank inayotoa huduma nzuri kama Crdb trust me jaribu kuingia Nmb au Nbc uone mziki utajuta
 
And vice versa is true@ChashaPoultryFarm hakuna bank inayotoa huduma nzuri kama Crdb trust me jaribu kuingia Nmb au Nbc uone mziki utajuta


Kwani Tanzania kuna Benki hizo pekee? Ninavyo jua kuna Benki zaidia ya 20 kwa sasa but mbona NMB na NBC? huzungumzii wakina Kenya Comercial Benk, wakina Exim na kazalika.
 
And vice versa is true@ChashaPoultryFarm hakuna bank inayotoa huduma nzuri kama Crdb trust me jaribu kuingia Nmb au Nbc uone mziki utajuta
NMB mimi sina acaunt kule nazungumzia enki ambapo ninaingia mara kwa mara, But runk benk zote Tanzania na si CRDB, NMB na NBC
 
kitengo cha FOREIGN TRANSFERS, au wanaopoke international money transfers ni wababaishaji sana....kawaida Telegraphic Money Transfer, kama umetumiwa kutoka nchi nyingine let's say Uingereza inapaswa pesa kuonekana kwenye account yako baada ya masaa 24 lakini hawa CRDB kwa sababu nisizozifahamu wanashikilia sana pesa za watu kabla ya kuwawekea kwenye account husika... Mimi nashangaa wanashikilia pesa za wateja kwa sababu gani? Ukienda mapokezi wanakwambia eti Value date bado.....huu ni wizi kabisa. Bank inanufaika kutokana na fees itakayokatwa kweny pesa zilizopokelewa hawana uhalali kabisa kushikilia pesa za mteja kabla ya kuzi release kwenye account yake. Sisi tunaolipwa kutoka nje tunapata shida sana unakuta pesa zimetumwa zaidi ya wiki hujazipata wakati ni kitendo cha masaa tu...
Aisee, nilifikiri ni mimi tu walinifanyia hii kitu, kumbe ni kawaida yao. Sijui kwa nini wanafanya haya madudu au ndo mwendelezo uleule wa wabongo kubweteka baada ya kupata mafanikio kidogo
 
Back
Top Bottom