Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,570
- 19,449
Nina wasiwasi kama kweli CIA huwa inafanya utafiti wa kutosha na kuwafahamu sawasawa viongozi wa kiafrika; mara nyingi huwa wanakosea. Kwa mfano walisema Mkapa alikuwa Kiongozi mzuri sana aliyekuwa akipendwa sanana na watu wake. Ukweli ni kuwa Mkapa aliondoka madarakani akiwa anachukiwa hata na watoto wadogo. In fact, wakati wa mwisho wa utawala wake, Mkapa alifanya jitihada sana za kushawishi watu wakubali kuwa ameleta maendelea sana Tanzania. Mara baada ya Kikwete kuingia madarakani, amekuwa akimwagiwa sifa nyingi sana kuwa ni kiongozi shupavu sana na mwenye nia kubwa ya kuwaondoa watu wake kutoka kwenye umaskini. Ukweli ni kuwa Kikwete hana mpando wowote wa kuwaondoa watu wake kwenye umaskini, ndiyo maana anela ufisadi kama vile haupo.
Zaidi zadi, kilichonifanya nijiulize swali hili ni jinsi walivyokuwa wanam-characterize Nyerere eti ni mtu asiyekuwa shupavu kiuongozi kiasi kuwa anasukumwa na wafuasi wake tu; yeye mwenyewe hawezi kujiamulia. Je ni kweli kuwa Nyerere alikuwa "Weak" leader? Hebu angalia ripoti hii ya CIA ya mwaka 1965.
Zaidi zadi, kilichonifanya nijiulize swali hili ni jinsi walivyokuwa wanam-characterize Nyerere eti ni mtu asiyekuwa shupavu kiuongozi kiasi kuwa anasukumwa na wafuasi wake tu; yeye mwenyewe hawezi kujiamulia. Je ni kweli kuwa Nyerere alikuwa "Weak" leader? Hebu angalia ripoti hii ya CIA ya mwaka 1965.