Chondechonde chadema undeni kambi yenye nguvu bungeni

elimukwanza

Senior Member
Dec 27, 2010
168
23
Nawasihi chadema waunde kambi yenye nguvu kushirikiana na vyama vingine vya upinzani bungeni.wasahau yote yaliyopita wawe wakomavu wa kisiasa.kamawameliweza hili la kuamsha umma katika mijadala ya kitaifa kitu ambacho kilikuwa akiwezekani naomba na ile walivunje kwani ni mtaji wa ccm.
kunaweza kuwa na wasiwasi na cuf lakini ndani ya muungano watajulikana kama kuna agenda za siri,sina shida na akina kafulila kwani ni hasira tu na kutofautiana na Mbowe lakini lengo ni moja.naomba wana jf tuwashi chadema walikubali bora tutoe mapendekezo namna gani ya muundo utakavyo kuwa kuliko kuendelea na kambi mbili za upinzani.
 
Naunga mkono hoja! Cdm kubalini kuungana halafu mbaya tutamfahamu tuu!
 
Nawasihi chadema waunde kambi yenye nguvu kushirikiana na vyama vingine vya upinzani bungeni.wasahau yote yaliyopita wawe wakomavu wa kisiasa.kamawameliweza hili la kuamsha umma katika mijadala ya kitaifa kitu ambacho kilikuwa akiwezekani naomba na ile walivunje kwani ni mtaji wa ccm.
kunaweza kuwa na wasiwasi na cuf lakini ndani ya muungano watajulikana kama kuna agenda za siri,sina shida na akina kafulila kwani ni hasira tu na kutofautiana na Mbowe lakini lengo ni moja.naomba wana jf tuwashi chadema walikubali bora tutoe mapendekezo namna gani ya muundo utakavyo kuwa kuliko kuendelea na kambi mbili za upinzani.

Mmh! Credibility ya hivyo vyama vya kuungana scares me to death! Let me wait and see, may be am wrong.
 
Natamani wangekuwa na masikio ya binaadamu wakakusikieni, siku zote chama chenye nia ya mageuzi ya kweli hakifanyia maamuzi ya kukurupuka kurupuka.Leo baadhi ya viongozi wa chadema wameonyesha rangi yao halisi, wameweka wazi nini wanachokitaka katika siasa, ile dhana ya kua ni chama cha kimageuzi imekufilia mbali.

Awali nidhani wamekataa kuunganisha nguvu na CUF, chama ambacho kimewabeba katka kambi ya upinzani kwa miaka kumi, kwa kile mwenye kiti wao alichokiita kuwa " ...hajuwi kama CUF ni ndege au mnyama", lakini nilichokiona ndani ya Mwenyekiti wa chadema si siasa za kimageuzi bali his lust needy-greedy to boss others(mifano ipo mingi) maana hata NCCR-Mageuzi hawakuwa na hitilafu aliyoiyona mwenyekiti wa chadema kwa CUF bali kwake kilikuwa " ..chama kidogo chenye sera tofauti na chadema...". Nabaki najiuliza je ni kweli chama kinachojiona kuwa mbadala wa kushika dola kinaweza kuwabaguwa wanamageuzi wenzake katika serikali kivuli ya upinzani bungeni, hali itakuwaje chama hiki kikabidhiwa kuongoza nchi?
 
Ni dhahiri Chadema they dont trust CUF et al....., Since they know more than we do.... Ninaheshimu maamuzi yao..., Probably they think others are traitors and who knows maybe they are..., and Chadema have reasons to believe so.., so if they think they can achieve alone all the best.
 
Muungano na vyama vingine vya upinzani bungeni is OK, Lakini kuungana na CUF kwa mawazo yangu ni big NO, tayari hali halisi tuliiiona siku ya mdahalo, CUF na CCM wana joint venture Zanzibar, CUF hawakumpigia kura mgombea wa kiti cha spika wa CDM, CUF walifirahia na kuchekelea walk out ya CDM na kukalia viti vya CDM bungeni
 
Siungi mkono kabisa hivi utashirikiana na cuf ,NCCR,TLP NA UDIPI Hawo wote mamrukitu kama wanajua umoja ninguvu kwanini walikataa kumuunga mkono Dr slaa kny uchaguzi mkuu? Bora ufe mwenyewe kuriko kuishi na masnichi kibao. hao wote mi ccm tu wanatuzuga tu.Hawana maana kabisa.cdm hatudanganyiki.
 
Naomba nieleweshwe na yeyote mwenye ujuzi wa shughuli za bunge. CDM kama chama kikuu cha upinzani chenye wabunge wengi bungeni, je, kitapoteza nini katika mijadala ya kitaifa wakiungana na vyama vingine vya upinzani bungeni ikiwa:
1. CUF, NCCR na TLP waingiapo bungeni kazi yao iwe kulala usingizi tu?
2. CUF, NCCR na TLP wakiwapo bungeni kazi yao iwe ni kuipinga CDM?
3. CUF,NCCR na TLP wakiwapo bungeni kazi yao iwe ni kuiunga mkono CCM?

Vilevile, CUF, NCCR na TLP wakiruhusiwa kuanzisha kambi ndogo ya upinzani bungeni, je kambi kuu ya upinzani itaathirika kwa lolote?
 
Back
Top Bottom