Chenge: Muongozo wa rasimu tuliyotunga ulitoka kamati kuu ya CCM

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Hatimaye yale madai kuwa rasimu ya katiba iliyokuwa ikijadiliwa bungeni ilitoka CCM yameanza kubainika ukweli wake.

Leo saa saba mchana mwenyekiti wa kamati ya uandishi wa rasimu ya katiba mpya Andrew Chenge amebainisha kuwa rasimu mpya ya katiba ilitungwa na CCM kipindi cha uchaguzi wa mabaraza ya katiba.

Aidha Chenge amethibitisha kuwa rasimu hiyo ilisambazwa kwenye mabaraza yote nchini na walitakiwa kutoa maoni yao kwa kufuata muongozo waliopewa, jambo ambalo tume ya Warioba ililibaini na kuyatupilia mbali maoni ya mabaraza hayo ambapo Chenge amesema kuwa taswira ya rasimu ya pili ya Warioba ingekuwa sawa kabisa na taswira ya rasimu ilyopelekwa bungeni na kamati yake kama wangezingatia maoni ya mabaraza hayo ambapo kimsingi yalitoka kamati kuu ya CCM kupitia ndugu Asharoze Migiro na ndugu Evodi Mmanda ambao waliyaratibu.

"Hata hii sisi tuliyotunga muongozo wake tuliupata kutoka CC ya CCM" alisema bwana Chenge.

Chenge aliyasema hayo wakati alipobanwa na baadhi ya waumini waliotoka kwenye ibada ili kujua ukweli wa mambo.

Aidha katika utafiti nilioufanya nimebaini kuwa vigogo wengi wa bunge maalum la katiba ambao waliingia kupitia taasisi mbalimbali ni makada waandamizi na wajumbe wa kamati kuu ya CCM ambao waliiandaa rasimu hii mapema sana na kwa kutumia sayansi ya hali ya juu kisha kuipenyeza kwenye mabaraza ya katiba jambo ambalo liligundulika na Chadema na tume ya Warioba.Pia makada hao wameongoza kamati zote zenye maamuzi juu ya rasimu hiyo.

Aidha Chenge alibaini kuwa kuzomewa kwa Warioba alipowasilisha rasimu bungeni ulikuwa mkakati wa mwanzo wa CCM kuikataa rasimu ya tume yake.

Cha kushangaza ni kuwa Chenge alisema CCM imefanya hivyo kwa nia njema ya kuliokoa taifa!
 
kuliokoa Taifa kwa kuondoa mambo tuliyotaka yawabane Viongozi wazembe na mafisa kama ya kuzuia viongozi kuwa na akaunti nje ya nchi, kuweka uwazi na uwajibikaji katika Serikali , pia kutochanganya mambo ya Tanganyika na Muungano. Na kwa taarifa yenu katiba hii imeua kabisa katiba ya zanziba kwa kuiondolea meno.
 
Hii ni nchi ya maajabu Mwizi, Fisadi ambae alitakiwa awe ameshitakiwa na kuhukumiwa miaka kadhaa jela hadi sasa kwa kashfa ya kulitia hasara Taifa katika sakata la Rada feki na utiaji saini wa mikataba kadhaa inayoliangamiza Taifa hadi sasa akiwa mwanasheria Mkuu leo hii ndio kiongozi wa uandishi wa Katiba ya Watanzania je tutarajie nini hapo?
 
UKAWA tumewazoea na Hekaya zenu za kijinga....

Tunasubiria Maandamano.
 
Kama ana nia ya kuliokoa taifa ajipeleke mwenyewe Segerea kujifunga kwa kosa la kuiba vijisenti vya RADA maana CCM yake imegoma kumchunguza na kumshtaki. Au naye aliiba hela za rada kwa maslahi ya Taifa?

Hii CCM tukiitoa madarakani 2015 tuombe msajiri aifute kabisa, imetesa Sana watanzania
 
leo mzee wa vijisenti amekuwa msafi wa kutuandikia katiba ccm wanaona warioba sio msafi wa kuandika katiba ama kweli watanzania tunasafari ndefu
 
Tanzania na watanzania kwa ujumla wao wanapaswa kuingizwa kwenye kitabu cha Guinness kwa maajabu yao. Mindset zetu zimelala sana ndio maana CCM wanatufanyia kadri wanavyotaka. Sisi ni sawa na kondoo hata akikamatwa na chui hapigi kelele hadi anauawa na kuliwa!
!
 
UKAWA tumewazoea na Hekaya zenu za kijinga....

Tunasubiria Maandamano.

Mijitu mingine bhana!nyinyi ndiyo wale meya mmoja alisema mnafikiria kwakutumia ------!hebu tuwe tunaacha upuuzi katika mambo ya maana,mnashangilia hata mtu akijamba!pumbavu sana.mtu akatoa hoja na ana ushahidi,wewe unaleta ushabiki!Mungu akusaidie.
 
Andrew Chenge amebaini kuwa rasimu mpya ya katiba ilitungwa na CCM kipindi cha uchaguzi wa mabaraza ya katiba.

Mkuu nisaidie kuelewa:

Andrew Chenge amebaini au amebainisha...?

-Kama amebaini (kuelewa) leo, ina maana siku zote akiwa kama mwenyekiti wa kamati ya kuandika rasimu alikuwa hajui hayo aliyoyasimamia kuandikwa?

-Kama amebainisha maanake ametoka nje ya sanduku na kudhihirisha undumila kuwili wake.

Kwanini aendelee kuaminiwa kwamba wana nia ya dhati ya kuandaa katiba mpya yenye kujali maslahi mapana ya wananchi bila kujali itikadi za vyama vyao?
 
Mkuu nisaidie kuelewa:

Andrew Chenge amebaini au amebainisha...?

-Kama amebaini (kuelewa) leo, ina maana siku zote akiwa kama mwenyekiti wa kamati ya kuandika rasimu alikuwa hajui hayo aliyoyasimamia kuandikwa?

-Kama amebainisha maanake ametoka nje ya sanduku na kudhihirisha undumila kuwili wake.

Kwanini aendelee kuaminiwa kwamba wana nia ya dhati ya kuandaa katiba mpya yenye kujali maslahi mapana ya wananchi bila kujali itikadi za vyama vyao?

Mkuu mimi nimechukulia neno 'baini' kama kutoa jambo sirini mwa kundi fulani na kulitoa kwa watu wachache ambao sio wahusika wa kundi ambapo kimsingi sio taarifa rasmi ya kundi.Ila kuweka mambo sawa nimebadilisha ili kuondoa mkanganyiko!
 
Hii nchi yaani hadi aibu watanzania
Wameharibiwa na moto wa mwenge
Ghafla tunakuwa wapole Kama mbwa
Anavyomuona chatu hakimbii wala kupambana
Badala yake hulialia na kujiandaa kukaa mkao wa kumezwa
Uchafu unaofanyika bmk watanzania
Tumepumbazwa na nini?
 
Mkuu mimi nimechukulia neno 'baini' kama kutoa jambo sirini mwa kundi fulani na kulitoa kwa watu wachache ambao sio wahusika wa kundi ambapo kimsingi sio taarifa rasmi ya kundi.Ila kuweka mambo sawa nimebadilisha ili kuondoa mkanganyiko!

Pamoja sana mkuu...
 
Back
Top Bottom