mediaman
JF-Expert Member
- Mar 20, 2011
- 451
- 687
Habari zilizoandikwa katika gazeti la Mwananchi zinasema kwamba "barabara inayokwenda kwa babu Loliondo inazidi kuharibika na kusababisha mamia ya wagonjwa na jamaa zao kukwama porini. Zaidi ya abiria 600 waliokuwa wanatoka Arusha kwenda huko wamekwama umbali wa kilometa 306 kutokana na ubovu huo. Hadi kufikia juzi, idadi ya magari yanayopeleka wagonjwa kwa Mchungaji Mwasapile yanakadiriwa kufikia 40,000."
Habari hizo zinaonyesha jinsi Tanzania ilivyo na maelfu ya watu wenye magonjwa mabaya(sugu). Kwanini watu waugue namna hii? Tatizo ni nini? Chanzo ni nini? Katika kutafuta jibu la swali hilo nimekutana na Maandiko katika Biblia, kitabu cha Kutoka, yanayosema kwamba Mungu aliwatia(aliwapa) Wamisri, maradhi(magonjwa) mabaya kama vile tauni nzito sana na majipu yenye kufura na kutumbuka kwa sababu ya dhambi zao. Nilipoendelea kusoma kitabu hicho nikaona maandiko mengine ambapo Mungu aliwaambia Wana wa Israeli kwamba hatatia maradhi juu yao kama alivyofanya kwa Wamisri. Hata hivyo aliwaamuru waisikize kwa bidii sauti ya BWANA Mungu, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio wasikie maagizo yake, na kuzishika amri zake. Kinyume cha hapo na wao wangetiwa maradhi mabaya kama Wamisri.
Yamkini Watanzania hatutaki kuisikiliza sauti ya BWANA Mungu ndio maana tunapatwa na maradhi mabaya. Yawezekana hatutaki kutenda mambo mema na yaliyo ya haki. Hatutaki kutii amri zake. Na hapo pana ukweli. Angalieni vitendo vya rushwa vilivyokithiri. Watu wanachakachua kura. Watu wanawaua Albino na kuchuna ngozi za binadamu wenzao eti wapate utajiri. Ubadhirifu wa mali ya umma, wanyonge hawapewi haki zao, majambazi wanaiba fedha benki, biashara ya ukahaba/uzinzi imeshamiri mpaka kwenye tovuti, mishahara inatolewa kwa wafanyakazi "hewa", wanafunzi wanaiba mitihani, waandishi wa magazeti nao wanadiriki hata kuandika habari za uongo ili kuvuna bila jasho! Matusi hata kwenye jamvi la JF. Madawa ya kulevya, pombe, kashfa, dharau… Hayo ni machache tu katika maovu mengi tunayoyaona hapa Tanzania.
Jamani wana JF, Mungu yupo. Ni kweli ana huruma, lakini upande mwingine anaghadhibika sana tunapomkosea kwa kufanya maovu kama hayo, na anaweza kutuangamiza ghafla hata tukifanya mazoezi ya kujikinga na hatari kama walivyokuwa wakifanya Wajapan kila mwezi. Sikia Mungu anavyosema katika Yeremia 30:12-15 "maumivu yako hayaponyekani, na jeraha yako ni kubwa…kwa jeraha yako huna dawa ziponyazo…maana nimekujeruhi…kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako…Mbona unalilia maumivu yako? Hayaponyeki…kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako, kwa sababu dhambi zako zimeongezeka, nimekutenda haya." Kumbe dhambi zinaweza kumfanya Mungu atutende mabaya.
Sisi tumewazidi nini Wamisri waliopata mapigo kwa sababu ya kiburi na ugumu wa mioyo yao? Je, tu watakatifu kuliko wao? Kama sivyo, tusishangae basi tunapoyaona magonjwa sugu(kisukari, kansa, pumu, ukimwi) katika miili yetu. Na wala tusimlaumu Mungu. Mungu hapendezwi na matendo ya dhambi kabisa. Miriam alipomsema vibaya mtumishi wa Mungu, Musa, alipata ukoma. Mungu aliiangamiza miji ya Sodoma na Gomora kwa sababu ya uzinzi na maovu mengi yaliyokuwa yakifanyika katika miji ile. Wakati wa Nuhu, watu wote(isipokuwa Nuhu na jamaa yake) waliangamizwa kwa gharika kwa sababu ya kutotaka kuyashika maagizo ya Mungu. Wakati wa Matendo ya Mitume Anania na Safira walipata adhabu ya kifo kwa kuficha sadaka/fungu la kumi na kusema uongo!
Nafikiri huu ni wakati mwafaka wa kubadili tabia zetu na kuanza kumcha Mungu Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Labda sasa unasema, "Ah hata tukiugua, babu yupo Loliondo tutapata kikombe!" Unaweza kufia njiani kabla hujafika kwa babu, si umesikia foleni ilivyo ndefu? Hata kama hakuna foleni, unaweza kufa njiani kwa ajali. Na hata baada ya kufika huko unaweza usipone kama ndugu zake Rostam na majirani zangu walioenda huko! Na hata ukipona, kesho utaugua tena maana chanzo cha magonjwa hujakiondoa. Ukinywa dawa ya kutibu malaria, utapona; lakini usipoondoa vyanzo vya mbu wanaoleta malaria nyumbani kwako, utaugua tena malaria baada ya muda mfupi.
Vipo vyanzo vingi vya magonjwa, lakini kama tulivyoona katika maandiko yale, inaonekana wazi kuwa dhambi ni chanzo kimojawapo cha magonjwa sugu yasiyoponyeka. Katika Yohana 5:14 Yesu alimwambia yule mtu aliyeponywa(na Yesu) "...Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi."
Sio rahisi kukiondoa chanzo hicho kwa nguvu na jitihada zetu. Lakini tukitubu dhambi zote na kuziacha na kumpokea Yesu kwa imani katika mioyo yetu, awe Bwana na Mwokozi wetu tutapewa(na Yesu mwenyewe) uwezo wa kushinda dhambi(Yohana 1:12; Warumi 8:37). Hapa na pale, tutaugua, maana bado tupo duniani, lakini kama Mungu alivyoahidi, hatatia maradhi mabaya juu yetu kama yale aliyowatia Wamisri, maana Yeye ni BWANA Mungu atuponyaye. Tukitubu dhambi na kuziacha na kumwamini Yesu, tutakuwa pia na uhakika wa kuingia mbinguni baada ya kufa. Huwezi kukwepa kifo kwa kupata kikombe cha babu. Babu mwenyewe ana miaka michache iliyosalia ya kuishi, maana miaka yetu ni 70 au 80 tukiwa na nguvu(Zaburi 90:10). Tusisahau, watakaoingia mbinguni ni watakatifu tu(Ufunuo 21:27). Tukiingia mbinguni tutastarehe milele na milele maana huko hakuna magonjwa wala kifo.
Habari hizo zinaonyesha jinsi Tanzania ilivyo na maelfu ya watu wenye magonjwa mabaya(sugu). Kwanini watu waugue namna hii? Tatizo ni nini? Chanzo ni nini? Katika kutafuta jibu la swali hilo nimekutana na Maandiko katika Biblia, kitabu cha Kutoka, yanayosema kwamba Mungu aliwatia(aliwapa) Wamisri, maradhi(magonjwa) mabaya kama vile tauni nzito sana na majipu yenye kufura na kutumbuka kwa sababu ya dhambi zao. Nilipoendelea kusoma kitabu hicho nikaona maandiko mengine ambapo Mungu aliwaambia Wana wa Israeli kwamba hatatia maradhi juu yao kama alivyofanya kwa Wamisri. Hata hivyo aliwaamuru waisikize kwa bidii sauti ya BWANA Mungu, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio wasikie maagizo yake, na kuzishika amri zake. Kinyume cha hapo na wao wangetiwa maradhi mabaya kama Wamisri.
Yamkini Watanzania hatutaki kuisikiliza sauti ya BWANA Mungu ndio maana tunapatwa na maradhi mabaya. Yawezekana hatutaki kutenda mambo mema na yaliyo ya haki. Hatutaki kutii amri zake. Na hapo pana ukweli. Angalieni vitendo vya rushwa vilivyokithiri. Watu wanachakachua kura. Watu wanawaua Albino na kuchuna ngozi za binadamu wenzao eti wapate utajiri. Ubadhirifu wa mali ya umma, wanyonge hawapewi haki zao, majambazi wanaiba fedha benki, biashara ya ukahaba/uzinzi imeshamiri mpaka kwenye tovuti, mishahara inatolewa kwa wafanyakazi "hewa", wanafunzi wanaiba mitihani, waandishi wa magazeti nao wanadiriki hata kuandika habari za uongo ili kuvuna bila jasho! Matusi hata kwenye jamvi la JF. Madawa ya kulevya, pombe, kashfa, dharau… Hayo ni machache tu katika maovu mengi tunayoyaona hapa Tanzania.
Jamani wana JF, Mungu yupo. Ni kweli ana huruma, lakini upande mwingine anaghadhibika sana tunapomkosea kwa kufanya maovu kama hayo, na anaweza kutuangamiza ghafla hata tukifanya mazoezi ya kujikinga na hatari kama walivyokuwa wakifanya Wajapan kila mwezi. Sikia Mungu anavyosema katika Yeremia 30:12-15 "maumivu yako hayaponyekani, na jeraha yako ni kubwa…kwa jeraha yako huna dawa ziponyazo…maana nimekujeruhi…kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako…Mbona unalilia maumivu yako? Hayaponyeki…kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako, kwa sababu dhambi zako zimeongezeka, nimekutenda haya." Kumbe dhambi zinaweza kumfanya Mungu atutende mabaya.
Sisi tumewazidi nini Wamisri waliopata mapigo kwa sababu ya kiburi na ugumu wa mioyo yao? Je, tu watakatifu kuliko wao? Kama sivyo, tusishangae basi tunapoyaona magonjwa sugu(kisukari, kansa, pumu, ukimwi) katika miili yetu. Na wala tusimlaumu Mungu. Mungu hapendezwi na matendo ya dhambi kabisa. Miriam alipomsema vibaya mtumishi wa Mungu, Musa, alipata ukoma. Mungu aliiangamiza miji ya Sodoma na Gomora kwa sababu ya uzinzi na maovu mengi yaliyokuwa yakifanyika katika miji ile. Wakati wa Nuhu, watu wote(isipokuwa Nuhu na jamaa yake) waliangamizwa kwa gharika kwa sababu ya kutotaka kuyashika maagizo ya Mungu. Wakati wa Matendo ya Mitume Anania na Safira walipata adhabu ya kifo kwa kuficha sadaka/fungu la kumi na kusema uongo!
Nafikiri huu ni wakati mwafaka wa kubadili tabia zetu na kuanza kumcha Mungu Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Labda sasa unasema, "Ah hata tukiugua, babu yupo Loliondo tutapata kikombe!" Unaweza kufia njiani kabla hujafika kwa babu, si umesikia foleni ilivyo ndefu? Hata kama hakuna foleni, unaweza kufa njiani kwa ajali. Na hata baada ya kufika huko unaweza usipone kama ndugu zake Rostam na majirani zangu walioenda huko! Na hata ukipona, kesho utaugua tena maana chanzo cha magonjwa hujakiondoa. Ukinywa dawa ya kutibu malaria, utapona; lakini usipoondoa vyanzo vya mbu wanaoleta malaria nyumbani kwako, utaugua tena malaria baada ya muda mfupi.
Vipo vyanzo vingi vya magonjwa, lakini kama tulivyoona katika maandiko yale, inaonekana wazi kuwa dhambi ni chanzo kimojawapo cha magonjwa sugu yasiyoponyeka. Katika Yohana 5:14 Yesu alimwambia yule mtu aliyeponywa(na Yesu) "...Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi."
Sio rahisi kukiondoa chanzo hicho kwa nguvu na jitihada zetu. Lakini tukitubu dhambi zote na kuziacha na kumpokea Yesu kwa imani katika mioyo yetu, awe Bwana na Mwokozi wetu tutapewa(na Yesu mwenyewe) uwezo wa kushinda dhambi(Yohana 1:12; Warumi 8:37). Hapa na pale, tutaugua, maana bado tupo duniani, lakini kama Mungu alivyoahidi, hatatia maradhi mabaya juu yetu kama yale aliyowatia Wamisri, maana Yeye ni BWANA Mungu atuponyaye. Tukitubu dhambi na kuziacha na kumwamini Yesu, tutakuwa pia na uhakika wa kuingia mbinguni baada ya kufa. Huwezi kukwepa kifo kwa kupata kikombe cha babu. Babu mwenyewe ana miaka michache iliyosalia ya kuishi, maana miaka yetu ni 70 au 80 tukiwa na nguvu(Zaburi 90:10). Tusisahau, watakaoingia mbinguni ni watakatifu tu(Ufunuo 21:27). Tukiingia mbinguni tutastarehe milele na milele maana huko hakuna magonjwa wala kifo.