Channel 10 na kujisafisha kwa Emmanuel Nchimbi, je ni kumuenzi Daudi Mwangosi?

Mkomamanga

JF-Expert Member
Dec 9, 2011
815
189
Leo baada ya taarifa ya habari ya saa moja channel 10 wameonesha kipindi maalum juu ya Press Conference ya Waziri wa Mambo ya ndani Emmanuel Nchimbi na waandishi wa habari iliyofanyika jana. Mambo kadhaa ameyataja katika hotuba yake lakini machache naona yanahitaji kufikiria kidogo.

1. Hadithi ya kumwokoa naibu waziri aliyetiwa mikononi mwa polisi kwa kuendesha kwa kasi, na pesa ikatumwa kwa M-Pesa je ndo mfumo wa siku hizi wa kukusanya mapato ya TRA?
2. Amedokeza mazungumzano ya IGP na Dr. Slaa na kuwa IGP alimsihi Dr. Slaa kama vile yeye si IGP lakini akasema avumilie kidogo mambo ya Sensa, je kule BUBUBU Zanzibar hakukuwa na sensa? Akina Kigwangala na Bashe wamefanya mikusanyiko ya wafuasi wao na kutishiana kupigana risasa sensa ilikuwa inaendelea na uchaguzi wa nazi za mikoa na wilaya kwa upande wa jumuiya za CCM pia umefanyika wakati wa Sensa wao wako juu ya amri ya serikali?
3. Amesema kipindi cha kupigania uhuru Baba wa taifa katika mikutano yake hakuna wafuasi waliowahi kuuawa! Je haoni kama anaashiria polisi wa kikoloni kuwa wastaarabu kuliko polisi wetu wa sasa nchi huru?
4. Na channel 10 kurusha taarifa yake kwa staili hii na mambo aliyoyazungumza yenye propaganda nyingi za kichama zaidi kuliko serikali hawaoni kama ni kumsaliti mwajiriwa wao marehemu Daudi Mwangosi?

Wakuu karibu jamvini tutoe mawazo yetu
 
Channel Ten hawajali hata siku ya kuanza walionyesha tukio kwa kurusha rusha ,ITV ndio waliipa coverage kubwa ndipo channel ten kwenye kipindi cha Baragumu dachi akavalia bango taarifa ,
Dina chahali kiongozi wa channel ten alisema Mwangosi hakuwa mwajiri wao kwa hiyo alimkana
Hii propaganda ya Nchimbi imebuma shughuli za mikusanyiko ziliendelea katika nyanja zote hakukuwa na sababu ya kuzuia chadema
Hakuna soko lilifungwa ,Kanisa ,Msikiti,Shule, Stand za mabasi,fiesta,arusi,send off,kipaimara,ubatizo,CCM na mikutano yao,ADC,CUF kwa hiyo hata wasemeje wao wameset precidency ya kupambana na chadema, kitu ambacho najiuliza jee wanaweza kupambana na nguvu ya umma
 
Mtoa roho siku zote hajiulizi mara mbili sababu za kukutoa roho yako! Ni kama vile wasemavyo kwamba mtu akianza kula nyama ya mtu hataacha ataendelea tu. Maana yake ni kwamba hawa mabwepande hawakuanza kuua leo, ndiyo maana ukiangalia sababu wanazotoa kuanzia nchimbi mwenyewe hazina mashiko wajameni. Au niwakumbushe, mmesikiliza/mmeona kwa makini maelezo ya mwema aliyoyatoa akiwa Iringa juzi alipoongozana na yule mfukia watu kule Bulyanhulu?
 
Inasikitisha kwamba Tanzania tangu tupate huru wa bendera hatujawahi kuwa na waziri wa mambo ya ndani wa kiwango cha chini cha busara kama Nchimbi, hata kutumia prefix ya Dr. naona hastahili labda kama ni Dr. magumashi! wanajikanyaga tu; ukweli uko wazi na wataumbuka siku si nyingi

Hata hivyo watahangaika sana patupu, tunaelewa kwamba mti unaorushiwa mawe mengi ni ule wenye matunda mengi! no wonder wanahangaika sana na CDM maana huko kwingine ni patupu.
 
nasikia rostam ana hisa kwenye hiyo channel...what do you expect from that?
 
Leo baada ya taarifa ya habari ya saa moja channel 10 wameonesha kipindi maalum juu ya Press Conference ya Waziri wa Mambo ya ndani Emmanuel Nchimbi na waandishi wa habari iliyofanyika jana. Mambo kadhaa ameyataja katika hotuba yake lakini machache naona yanahitaji kufikiria kidogo.

1. Hadithi ya kumwokoa naibu waziri aliyetiwa mikononi mwa polisi kwa kuendesha kwa kasi, na pesa ikatumwa kwa M-Pesa je ndo mfumo wa siku hizi wa kukusanya mapato ya TRA?
2. Amedokeza mazungumzano ya IGP na Dr. Slaa na kuwa IGP alimsihi Dr. Slaa kama vile yeye si IGP lakini akasema avumilie kidogo mambo ya Sensa, je kule BUBUBU Zanzibar hakukuwa na sensa? Akina Kigwangala na Bashe wamefanya mikusanyiko ya wafuasi wao na kutishiana kupigana risasa sensa ilikuwa inaendelea na uchaguzi wa nazi za mikoa na wilaya kwa upande wa jumuiya za CCM pia umefanyika wakati wa Sensa wao wako juu ya amri ya serikali?
3. Amesema kipindi cha kupigania uhuru Baba wa taifa katika mikutano yake hakuna wafuasi waliowahi kuuawa! Je haoni kama anaashiria polisi wa kikoloni kuwa wastaarabu kuliko polisi wetu wa sasa nchi huru?
4. Na channel 10 kurusha taarifa yake kwa staili hii na mambo aliyoyazungumza yenye propaganda nyingi za kichama zaidi kuliko serikali hawaoni kama ni kumsaliti mwajiriwa wao marehemu Daudi Mwangosi?

Wakuu karibu jamvini tutoe mawazo yetu


Mkuu, mi hawa Chanel 10 wananishangaza sana. wanakuwa wanabadilikabadilika kwenye mambo yao mpaka nashindwa kuwaelewa. ukiangalia kile kipindi cha Hamza Kassongo Hour, kilichohudhuriwa na wale waandishi wawili wa habari, kwa kweli kilikuwa kizuri mno, yaani ni sawa na kupata mwalimu mtaalamu wa hesabu, halafu akakufundisha 5+5 huku akitumia vidole vyako vya mikono (hasa ukiwa navyo vyote vitano kila mkono). yaani utaelewa na kamwe hautasahau mpaka unaingia kaburini. cha ajabu hicho kipindi maalum cha hiyo press conference ya nchimbi, ni uharo mtupu.
WANANG'ANG'ANIA KUFUATA SHERIA, POLISI KUMUUA MTU BILA KUMFIKISHA MAHAKAMANI HALI YA KUWA YUPO MIKONONI MWENU NA HANA UWEZO WA KUWATOROKA, NI SHERIA GANI??? HAKYANANI NINGEKUWA KARIBU NA HUYU ZUZU mwema, NINGEMKATA BONGE LA KOFI. HANA AKILI KABISA HUYU MJINGA. POLISI WAMEKIUKA SHERIA, HUWAAMBII LOLOTE, HALAFU ANA WATAKA WENGINE WATII SHERIA TENA BILA SHURUTI, HIVI HUYU mwema, ZINAMTOSHA KWELI??? AU NDO KWA SABABU HANA WA KUMUULIZA???
NDO MAANA WAISLAMU TUNALAANIWA KWA UNAFIKI HALI YA KUWA QUR'AN INAKATAZA KUWA MNAFIKI. SHERIA ZA MWENYEZI MUNGU ZIMEWASHINDA, HATA HIZI ZA KUCHAKACHULIWA NA BINADAMU NAZO HAMZIWEZI??? DUDE ZIMA LI mwema LINAONGEA PUMBA MBELE ZA KAMERA KUSITIRI TUMBO LAKE NA FAMILIA YAKE. NDO MAANA MWENYEZI MUNGU ALITUTAHADHARISHA MAPEMA KWENYE QUR'AN KUWA MAKINI NA FITINA YA MALI NA WATOTO. TUANAENDEKEZA MNO NJAA MPAKA TUNADHALILIKA



Tuendeleeni kuwaelimisha watanzania, waelimike ili waliondoe madarakani hili li serikali la ccm MAONGO/MAFISADI/MAJAMBAZI/WAUAJI.
 
Nilishangaa Kipindi ambacho kilipaswa Kirushwe na TBC kinarushwa na Channel 10 ambayo ilipaswa kuwa mstari wa Mbele kususia habari zinazohusu police na wizara ya Nchimbi, wamemsaliti mwangosi mapema sana!
 
tutaendelea kumlilia mwangosi.Waliomua ni mapolisi wa serikali katili kama ya makaburu, Hawana ubinadamu kabisa. N ukiwaangalia sana unaona heri polisi wa kikoloni walikuwa na utu kuliko polisi wa serikali ya JK.
 
Huyo Dina Chahali kwa kweli alitia fora. Alimkana kinamna flani Mwangosi kwa kudownplay role yake kwa Channel 10. Haisaidii kitu hili polisi wanalo wamemess up kweupeee

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Channel Ten hawajali hata siku ya kuanza walionyesha tukio kwa kurusha rusha ,ITV ndio waliipa coverage kubwa ndipo channel ten kwenye kipindi cha Baragumu dachi akavalia bango taarifa ,
Dina chahali kiongozi wa channel ten alisema Mwangosi hakuwa mwajiri wao kwa hiyo alimkana
Hii propaganda ya Nchimbi imebuma shughuli za mikusanyiko ziliendelea katika nyanja zote hakukuwa na sababu ya kuzuia chadema
Hakuna soko lilifungwa ,Kanisa ,Msikiti,Shule, Stand za mabasi,fiesta,arusi,send off,kipaimara,ubatizo,CCM na mikutano yao,ADC,CUF kwa hiyo hata wasemeje wao wameset precidency ya kupambana na chadema, kitu ambacho najiuliza jee wanaweza kupambana na nguvu ya umma

lakini kama ulimsikiliza lipumba aliongea kwa busara sana na aliongea mambo ya msingi na pia alihoji uhalalili wa ccm kuendelea na mikutano wakati cdm wanazuiwa!

Pia alihoji kwa nini sensa iingilie mikutano ya siasa!

Pia alihoji nguvu kubwa iliyo tumiwa na polisi kuzuia cdm!
 
Huyo Dina Chahali kwa kweli alitia fora. Alimkana kinamna flani Mwangosi kwa kudownplay role yake kwa Channel 10. Haisaidii kitu hili polisi wanalo wamemess up kweupeee

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

kweli mwenyewe sikupendezwa sana japo alikuwa anasema ukweli ila sikuona haja ya kutumia muda mrefu kulizungumzia hilo la kuajiliwa au kutoajiliwa kwa marehemu
 
Inasikitisha kwamba Tanzania tangu tupate huru wa bendera hatujawahi kuwa na waziri wa mambo ya ndani wa kiwango cha chini cha busara kama Nchimbi, hata kutumia prefix ya Dr. naona hastahili labda kama ni Dr. magumashi! wanajikanyaga tu; ukweli uko wazi na wataumbuka siku si nyingi

Hata hivyo watahangaika sana patupu, tunaelewa kwamba mti unaorushiwa mawe mengi ni ule wenye matunda mengi! no wonder wanahangaika sana na CDM maana huko kwingine ni patupu.
Yule siyo Dr basi tu, ulishaona desertation yake? Eti ni mtaalamu wa uchumi, wapi na wapi ndugu yangu!! Nchimbi ni kati ya viongozi ambao ni bogus kabisa. Amekalili tu kuwa ukiua adui basi ndiyo njia nyeupe ya kuwin!! I know there is a list of shame on the Iringa saga!
 
Correction: Mwangosi hakuwa mwajiriwa wa Channel ten.

Ni kweli lakini hakukuwa na haja ya taarifa ya aina hiyo wakati huu. Channel 10 lazima wazingatie kuwa alikuwa mtu muhimu kwao awe wamemuajiri ama wamempa mkataba wa habari. Alikuwa akiwafanyia kazi muhimu.
 
Inasikitisha kwamba Tanzania tangu tupate huru wa bendera hatujawahi kuwa na waziri wa mambo ya ndani wa kiwango cha chini cha busara kama Nchimbi, hata kutumia prefix ya Dr. naona hastahili labda kama ni Dr. magumashi! wanajikanyaga tu; ukweli uko wazi na wataumbuka siku si nyingi

Hata hivyo watahangaika sana patupu, tunaelewa kwamba mti unaorushiwa mawe mengi ni ule wenye matunda mengi! no wonder wanahangaika sana na CDM maana huko kwingine ni patupu.

Mti unaorushiwa mawe unaweza ukawa na nyoka, usikariri...
 
Nilishangaa Kipindi ambacho kilipaswa Kirushwe na TBC kinarushwa na Channel 10 ambayo ilipaswa kuwa mstari wa Mbele kususia habari zinazohusu police na wizara ya Nchimbi, wamemsaliti mwangosi mapema sana!

Usaliti ni kususia habari ambazo Daudi amekufa akizitafuta.
Ili kumuenzi nilitegemea wanahabari wazing'ang'anie habari za polisi mpaka waseme bhaaas!!
Wanishangaza sana hawa wataalamu kwa kweli...
 
Back
Top Bottom