Changia kwa hekima, kosoa kwa heshima

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,640
697,994
Jamii forums imetoa uhuru wa kutumia utambulisho bandia kwa akili ya kulinda maslahi binafsi ya mwanachama.. Lakini kupewa huo uhuru haina maana uwatweze wengine kwa vile tu hujulikani utambulisho wako halisi

Ndani ya huu mtandao kuna mwanachama wa aina mbili au tatu
1. Wanaotumia utambulisho halisi
2. Wanaotumia utambulisho bandia
3. Wanaotumia utambulisho halisi na bandia
Watu wanakutana hapa hawafahamiani lakini kutokana na mahitaji ya kimaisha na maslahi ya kila mmoja ama ya upande mmoja watu hufikia hatua ya kufahamiana zaidi nje ya huu mtandao

Kuna wajinga wachache wenye uono kimo cha mbilikimo wanaodhani kwa kutumia utambulisho bandia basi wanaweza kufanya lolote na wasijulikane popote bila kujua ya kwamba maandishi hayafitiki.. Ni kupitia maandishi yako ya jana ama hitaji lako la mbeleni unaweza kujifunua na kubaki uchi kabisa

Heshimu sana maandiko ya wengine hasa wale ambao unaishia kuwaona jukwaani lakini hamjawahi hata kuonana.. Hata kama maandiko yake hukubaliani nayo kosoa kwa adabu kosoa kwa heshima..Kosoa kwa hoja jadilifu na si vioja, kashfa, dharau au kejeli!

Heshima muda wake aliotumia kuandika hiyo mada, kifurushi chake, ujumbe na maudhui yake..! Si lazima ukubaliane naye.. Hivyo mpinge kwa hoja zenye mantiki ama mpotezee.. Sometimes kuna kipengele cha kukubaliana kutokubaliana na kinyume chake!

Ukiona mada imeruhusiwa kuwa hewani na kupata wachangiaji... Iheshimu sana kwa maana ina kibali cha kanuni na sheria za jukwaa! Kwa maana ya kwamba imekidhi vigezo vyote vya kuruhusiwa kuwepo hai.. Watu wanaweka mada na hazichukui round zinaliwa kichwa na kutupwa jalalani..

Mada inayoachwa hewani iheshimu sana kulingana na jukwaa lake husika..kitendo cha kuiita ya kipuuzi ama ya kipumbavu si kwamba umemtusi na kumkejeli mtoa mada tu, bali hata wachangiaji wengine na hata walioiruhusu iwepo hewani

Unapokuwa mwanachama mgeni (sio multiple ID) Unakuwa mkweli sana.. Unaongea maisha yako unajitambulisha uhalisia wako na kuomba ushauri hapa na pale. Unapokuwa mzoefu unaanza kuvimba kichwa na kujisahau wewe ni nani uko wapi na unafanya nini.. Unasahau hata background yako na kudhani hujulikani..

Usiwe ndezi kiasi Hicho una background that can be traced to the maximum... Maandishi yako mwenyewe ya awali yanaweza kuwaongoza watu mpaka ulipo na wakakufikia bila shida na wakakufanya chochote watakacho hasa kama hawana hofu na Mungu aliye hai

Kikubwa unapotumia utambulisho bandia usidhani ndio umeyawezea maisha.. Kumbuka bado unaishi na shida hazikomi.. Lakini pia kumbuka una background ambayo kwa namna iwayo yote huwezi kuifuta na watu wanayo mkononi..

Ni hayo tuu
 
Ukisemacho ni kweli. Lakini pia,kumbuka, watu wameumbwa tofauti. Sikatai kuwa kuna watu ukiangalia majibu,yao,unaona kweli mamemaanisha. Lakink,wengine wanapenda na utani utani. Labda kama utani ndo marufuku. Wengine wanakwazika,ukiwaeleza kwa nini umejibu ovyo wanaelewa.
Japo wakati mwingine,pia comments hutokana na mada yenyewe. Zipo zinazokaa kiheshima,na nyimgine zaimekaa kihuni huni
 
Ukisemacho ni kweli. Lakini pia,kumbuka, watu wameumbwa tofauti. Sikatai kuwa kuna watu ukiangalia majibu,yao,unaona kweli mamemaanisha. Lakink,wengine wanapenda na utani utani. Labda kama utani ndo marufuku. Wengine wanakwazika,ukiwaeleza kwa nini umejibu ovyo wanaelewa.
Japo wakati mwingine,pia comments hutokana na mada yenyewe. Zipo zinazokaa kiheshima,na nyimgine zaimekaa kihuni huni
Kuna utani mwingi sana kwa waliozea kutaniana lakini huwa ni utani wenye mipaka na staha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wajinga wachache wenye uono kimo cha mbilikimo wanaodhani kwa kutumia utambulisho bandia basi wanaweza kufanya lolote na wasijulikane popote bila kujua ya kwamba maandishi hayafitiki.. Ni kupitia maandishi yako ya jana ama hitaji lako la mbeleni unaweza kujifunua na kubaki uchi kabisa


Ehhh Mola uitwae Mungu uwakimbiae watu unaobambikiziwa huku inajulikana kweli wewe kujawahi na hutakaa utokee, kuna kiumbe hapa anatutukana watu waliosalia wakati ule unachagua wa kwenda nao
 
Kuna utani mwingi sana kwa waliozea kutaniana lakini huwa ni utani wenye mipaka na staha

Sent using Jamii Forums mobile app
Watu humu wamekulia sehemu tofauti tofauti. JF ni jamii kubwa ambayo ingetumika kistaarabu,wengi wangenufaika. Lakini,ukiangalia mada zinazoandikwa,comments zake,wengi utawajua. Kiutani utani mtu atacomment kuongeza scores,lakini pia mchango wake hupatikana inapobidi. Watu ambao hawajaishi na watu,ndo unakuta wakiguswa tu kiutani, wanakuja juu na milingoti.
Na miaka ya nyuma,majukwaa yote yalikuwa na adabu. Sijui kaingia mdudu gani!
 
Jamii forums imetoa uhuru wa kutumia utambulisho bandia kwa akili ya kulinda maslahi binafsi ya mwanachama.. Lakini kupewa huo uhuru haina maana uwatweze wengine kwa vile tu hujulikani utambulisho wako halisi

Ndani ya huu mtandao kuna mwanachama wa aina mbili au tatu
1. Wanaotumia utambulisho halisi
2. Wanaotumia utambulisho bandia
3. Wanaotumia utambulisho halisi na bandia
Watu wanakutana hapa hawafahamiani lakini kutokana na mahitaji ya kimaisha na maslahi ya kila mmoja ama ya upande mmoja watu hufikia hatua ya kufahamiana zaidi nje ya huu mtandao

Kuna wajinga wachache wenye uono kimo cha mbilikimo wanaodhani kwa kutumia utambulisho bandia basi wanaweza kufanya lolote na wasijulikane popote bila kujua ya kwamba maandishi hayafitiki.. Ni kupitia maandishi yako ya jana ama hitaji lako la mbeleni unaweza kujifunua na kubaki uchi kabisa

Heshima sana maandiko ya wengine hasa wale ambao inaishia kuwaona jukwaani lakini hamjawahi hata kuonana.. Hata kama maandiko yake hukubaliani nayo kosoa kwa adabu kosoa kwa heshima..Kosoa kwa hoja jadilifu na si vioja, kashfa, dharau au kejeli!

Heshima muda wake aliotumia kuandika hiyo mada, kifurushi chake, ujumbe na maudhui yake..! Si lazima ukubaliane naye.. Hivyo mpinge kwa hoja zenye mantiki ama mpotezee.. Sometimes kuna kipengele cha kukubaliana kutokubaliana na kinyume chake!

Ukiona mada imeruhusiwa kuwa hewani na kupata wachangiaji... Iheshimu sana kwa maana ina kibali cha kanuni na sheria za jukwaa! Kwa maana ya kwamba imekidhi vigezo vyote vya kuruhusiwa kuwepo hai.. Watu wanaweka mada na hazichukui round zinaliwa kichwa na kutupwa jalalani..

Mada inayoachwa hewani iheshimu sana kulingana na jukwaa lake husika..kitendo cha kuiita ya kipuuzi ama ya kipumbavu si kwamba umemtusi na kumkejeli mtoa mada tu, bali hata wachangiaji wengine na hata walioiruhusu iwepo hewani

Unapokuwa mwanachama mgeni (sio multiple ID) Unakuwa mkweli sana.. Unaongea maisha yako unajitambulisha uhalisia wako na kuomba ushauri hapa na pale. Unapokuwa mzoefu unaanza kuvimba kichwa na kujisahau wewe ni nani uko wapi na unafanya nini.. Unasahau hata background yako na kudhani hujulikani..

Usiwe ndezi kiasi Hicho una background that can be traced to the maximum... Maandishi yako mwenyewe ya awali yanaweza kuwaongoza watu mpaka ulipo na wakakufikia bila shida na wakakufanya chochote watakacho hasa kama hawana hofu na Mungu aliye hai

Kikubwa unapotumia utambulisho bandia usidhani ndio umeyawezea maisha.. Kumbuka bado unaishi na shida hazikomi.. Lakini pia kumbuka una background ambayo kwa namna iwayo yote huwezi kuifuta na watu wanayo mkononi..

Ni hayo tuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Ha ha!

...tracked to the maximum.

Tisha tisha hii. ati utatafutwa na watu wasiojulikana?

Kumbe mnawajua hao wasiojulikana, wasio na hofu
watakao kufikia bila shida na wakakufanya chochote watakacho hasa kama hawana hofu na Mungu aliye hai
halafu mnakaa humu kuwasingizia wengine!
 
Haya ni mawazo yako, lakini yanaweza kukosolewa. Kumbuka sio kila siku ni Jumapili au ijumaa. Wewe ulikuwa hutambuliki mwanzo lakini baadaye uliamua kwa mapenzi yako kujitambulisha. Hatufahamu sababu zako kujitambulisha, na hiziwezi kuwafanya watu wote wajitambulishe humu.

Kumbuka Serikali yetu ni moja ya sababu ya watu kutokujitambulisha. Jamii FORUM kwa miaka nenda rudi imekuwa ikiwahakikishia members wake kuwa identities zao zinalindwa hilo limewapa wengi nguvu kukosoa au kusema yale ambayo wengi tusingeyafahamu. Na hiyo ni kwasababu wengi hufungua Account kwa taarifa za uongo ili kuweza kufikisha ujumbe mahususi na kisha kupotelea huko waliko. Wengi wafanyao hivyo ni wafanyakazi wa serikali wenye taariafa nyeti.

Unaposema wanaweza kufuatiliwa na kupatikana, siwezi kukubishia, lakini kwa mtu makini aliyetoa taarifa nyeti huwezi kumpata. Achana na sisi tunao andika hovyo hovyo humu.

Lakini bado naamini siwezi kuwa verified member, eti kwasababu tu kwamba taarifa za maandiko yangu zinaweza kufichuliwa na identity yangu kufahamika. Kuficha identity yangu na kuandika nitakacho ni hakikisho kutoka JAMIIFORUMS. Ila kama Mshana unasema hakuna hilo hakikisho basi JF itakuwa na matatizo na isipo aminika na members wake basi humu tutakosa taarifa muhimu nyingi na mtandao huu utafubaa na kukosa ladha kabisa.

Hatuwezi wote kufanana, wacha kila mtu afurahi kivyake, kuna mnaofurahi hadharani tupo siye tunaofurahia huku sirini.

Napenda hivi ilivyo to each is different, reveal yourself if you want ,but I won't. I will stay in the shadow.
 
Kwa wachangiaji kutoa lugha za matusi na kejeli, hata JamiiForums imepoteza 'image' iliyokuwanayo hapo mwanzo na kuonekana kama mtandao wa kihuni.

Nakumbuka hapo nyuma watu wengi walikuwa wanakimbilia huku kupata habari na mambo mbalimbali ikiwemo mijadala ya uchumi, mahusiano, afya na mengine. Hii iliwafanya watu wengi kujiunga na mtandao huu.

Mada/hoja zilizokuwa zinaletwa hapa zilifanya watu wengi kujifunza na kwa namna flani kubadilisha mitizamo pia. Lakini leo hii mtu anakuja na hoja flani kama moja ya changamoto inayomtatiza, ila ataonekana kama mkoswa akili na kwanini ameshindwa kujipania kulekule.

Hii pia inaonyesha uhalisia wetu nje ya mtandao huu vile tunavyoishi na ukisasa unavyotuendesha. Je ni ukosefu wa maadili ama 'id fake' ndo tatizo?
 
Watu humu wamekulia sehemu tofauti tofauti. JF ni jamii kubwa ambayo ingetumika kistaarabu,wengi wangenufaika. Lakini,ukiangalia mada zinazoandikwa,comments zake,wengi utawajua. Kiutani utani mtu atacomment kuongeza scores,lakini pia mchango wake hupatikana inapobidi. Watu ambao hawajaishi na watu,ndo unakuta wakiguswa tu kiutani, wanakuja juu na milingoti.
Na miaka ya nyuma,majukwaa yote yalikuwa na adabu. Sijui kaingia mdudu gani!
Na miaka ya nyuma,majukwaa yote yalikuwa na adabu. Sijui kaingia mdudu gani!,
Forum imekua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na miaka ya nyuma,majukwaa yote yalikuwa na adabu. Sijui kaingia mdudu gani!,
Forum imekua

Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini,inatoa picha halisi ya wanachama. Wengi vijana wadogo,ndo maana hata matunda ya kimasihara ndo mengi siku hizi. Sasa, dogo plans ni kugegeda mtu lika la mama yake,mara mshaulini aanzeje! Hata anaeuliza swali la maana,anapewa majibu ya ovyo kabisa
 
Back
Top Bottom