MKALIMOTTO
Senior Member
- Apr 7, 2012
- 136
- 9
Wanajamvi, si jambo geni kuwa chadema haiko katika good term na vyombo vya dola. Ni kutokana na madai kuwa dola inakihujumu chama hicho katika harakati zake za kuongoza nchi. Mimi sina uhakika na tuhuma hizo. Kama ni kweli ama la, ni siri ya watuhumiwa pengine na watuhumu. Katika hili niishauri cdm irudi nyuma na kutafakari juu ya tuhuma zake hizo ambayo kiukweli inakera na inakatisha tamaa. Cdm ijue kuwa inajipanga kuchukua nchi na kwamba ni lazima sasa iseme vizuri na wenye nchi, naam wenye nchi ndiyo kwa kuwa ndiyo wenye jukumu namba moja la kuhakikisha nchi iko shwari. Iseme nao vizuri kwasasbabu kwa vyovyote vile ili itawale kwa mafanikio haitakuwa na budi kufanya kazi na dola hiyo hiyo. Vinginevyo wakifikiri eti kubadili top ranks ndiyo itakuwa suluhisho haitasaidia, kitakachokuwa kinafanyika ni kuwa cdm itahujumiwa mpaka basi. Mimi binafsi naogopa sana, cjui labda kama cdm ina mpango wa kukodi polisi, usalama wa taifa na jwtz kutoka nje ya nchi. Kama si hivyo, kwa vyovyote jamaa watarevenge kwa kutumia technical subotage ambayo itaifanya serikali kushindwa kabisa na hivyo wananchi kupoteza imani nayo. Ninaishauri cdm kuwa isitunishiane msuli na wazee wa kazi, iwe pole na ijenge urafiki kwaajili ya mafanikio ya baaadaye. Karibuni kwa michango yenye hekima na busara kwa lengo la kuwasaidia wakurupukaji na waropokaji kama akina lema (aondolewe ndani ya chama ni mzigo)