Elections 2010 Chadema watumie rangi nyeupe pe kwenye mikutano yao!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Nimeangalia kwa muda sasa picha za Chadema kwenye mikutano yao ya kampeni. Jambo moja lililo dhahiri ni kuwa hawajajua namna ya kutumia rangi kujenga acceptance, ushirikiano, kukubalika, kupendwa na cohesion ya aina fulani. Naamini tatizo moja ni hilo la magwanda kwa sababu viongozi hawawezi kujiona wanapendeza au wanavutia nje ya makombati na tatizo la pili ni kuwa bendera ya Chadema ina rangi nyingi kidogo (nyekundu, nyeupe, bluu na nyeusi). Hili la pili linafanya ni vigumu sana kuwa na rangi ya kuunganisha wanachama wote.

Hivyo utaona kule Moshi kwenye mikutano wamevaa nyekundu, Dar kwaenye mikutano wamejivalia rangi mbalimbali au hata bila rangi na hivyo ukiangalia mkutano wa Chadema na wa CCM unaona kuwa CCM inakubalika zaidi, ina watu wengi zaidi na inapendwa zaidi.

Ni katika kufikiria hivyo nimeona kuwa ni lazima kucounter hiyo perception kwa Chadema kutumia rangi nyeupe pe (pure white). Siyo nyeupe na bluu kama NCCR au Bluu bahari kama CUF bali rangi nyeupe kabisa hata inayong'ara.

Rangi nyeupe inaendana na ujumbe wa Chadem:

a. Ni usafi - Chadema inasema kuna uchafu na wanataka kuleta usafi
b. Ni Uadilifu - Kinyume cha sifa ya ufisadi na ubadhirifu.
c. Ni Amani - kwamba mabadiliko wanayoyataka kuleta siyo ya vurugu, au shari bali ni mapinduzi ya amani.


So, ningekuwa nina uwezo wa kutoa ushauri mdogo tu ningetumia saikolojia ya rangi kuweza kuonesha jinsi Chadema inakubalika, kupendwa na kuwa na mwonekano (perception) kuwa ni ya umoja wake. Hata makamanda katika makombati yao wanaweza kujiadorn na white lesos!

Just a thought.. you can continue to dismiss it.
 
Mkuu I second this.

Ukweli ni kuwa rangi inleta mvuto sana katika kusanyiko la watu. I suggest CHADEMA to take thins into consideration; rangi nyekundu huwa ni nzuri san pia kwenye makusanyiko; ubaya wake, CCM wanaweza kubadili maana na kusema wanataka kumwaga damu hawa!!

I think pure white is ideal!!:becky:
 
Pure white or the party's coulor but white to dominate and if possible dicard red altogether. CCM wameshaanza kuhubiri mambo ya vurugu kwenye nchi za jirani so any reddish in their colours could jeopardize their position especially in the rural areas where the level of reasoning is low.

I also agree that yale magwanda do not present CHADEMA very well, they do not look nice!
 
You are right Mwanakijiji! Kuna wakati pia wazo hili la rangi lilinijia. Nakubaliana nawe kwamba rangi nyeupe ni muafaka kwa CHADEMA kutokana na ujumbe wake kwa Watanzania. Rangi nyeupe inaashiria amani.
 
Lakini itakuwaje kama wataona hawataki kubadili rangi na ni usumbufu wakati wao wanataka kuonekana ni wapiganaji zaidi? na hivyo kutaka magwanda zaidi ambayo nadhani yanawagawa anyway.. kwa sababu ukiondoa viongozi tu sijaona wanachama wakiwa wamevaa magwanda hayo; hata jeshini mavazi ya wanajeshi na maafisa wao yanafanana ukiondoa vyeo.. ndio maana njano na kijani ya CCM inafanana hata na mama mtu ambaye hana nafasi yoyote ndani ya CCM. Hii inaitwa political connection..

kwa wao kupenda kuvaa magwanda wanajigawa na wananchi wanaotaka kuwaongoza.
 
Yes but it's like it is too late!

Not really mkuu!!
Ni suala la kujipanga tu... I expect CHADEMA have a tactical team in place which can absorbs operational changes!! Hii ni vita mkuu! Believe me color can make a difference!
 
rangi inahusiana na kukubalika; kupatanisha n.k

Mwanakijiji;

Umenifikisha hata kwenye rangi za Bendera.

Sister wangu moja baada ya kusikiliza ufunguzi wa Kampeni wa CCM na CHADEMA hatimaye nilimwuliza unasimama upande gani?

Alinijibu yeye kura yake ni kwa CCM tu. (Hata hivyo yeye si mpenzi wa chama chochote na analaani sana ufisadi wa CCM)

Nilipomdodosa zaidi kwa nini sasa awape CCM, akadai CHADEMA ni watu wa vurugu. Tazama na bendera zao zina RED kuashiria kuwa ni watu wa kumwaga damu. Akadai bora amani kuliko ufisadi.

Nimejiuliza pia mantiki ya CHADEMA kutumia nyekundu, sikuipata. Lakini hata kama ina maana yoyote, walau isingechukuwa sehemu kubwa ya Bendera.

Huenda na hili la sare za mikutano nalo likawa na mantiki kama ulivyoeleza.
 
kubadili sare katikati ya mapambano si vema, HOWEVER
-Chadema wachukue ushauri wa kupamba kwa rangi nyeupe kwenye majukwaa,
-wanachama wavae tishts nyeupe na mashati meupe yaliyo cheap
-Makamanda waendelee na magwanda na skafu nyeupe
 
....Daaah mkuu hili huwa linakuja kichwani mwangu kila nionapo jezi za Chadema.....! Sasa mkuu unaweza kuwapenyezea huo ujumbe, mi nafikiri ni mapema wanaweza kubadilika na kuwa na majukwaa yanayopendeza na kukubalika kwa mtazamo wa nje (bila hata ya kuzungumza kitu)
 
Mwanakijiji;

Umenifikisha hata kwenye rangi za Bendera.

Sister wangu moja baada ya kusikiliza ufunguzi wa Kampeni wa CCM na CHADEMA hatimaye nilimwuliza unasimama upande gani?

Alinijibu yeye kura yake ni kwa CCM tu. (Hata hivyo yeye si mpenzi wa chama chochote na analaani sana ufisadi wa CCM)

Nilipomdodosa zaidi kwa nini sasa awape CCM, akadai CHADEMA ni watu wa vurugu. Tazama na bendera zao zina RED kuashiria kuwa ni watu wa kumwaga damu. Akadai bora amani kuliko ufisadi.

Nimejiuliza pia mantiki ya CHADEMA kutumia nyekundu, sikuipata. Lakini hata kama ina maana yoyote, walau isingechukuwa sehemu kubwa ya Bendera.

Huenda na hili la sare za mikutano nalo likawa na mantiki kama ulivyoeleza.

It is all about perception..! hilo la magwanda siligusi tena maana kama wangekuwa wanajua mambo ya saikolojia ya siasa wangebadilisha zamani kweli.. jamani hata John Garang alivaa suti! Nadhani hawataki kujua jinsi wanakuwa perceived which is the hidden pyschological profile ambayo wananchi wanatengeneza.
 
Nimeangalia kwa muda sasa picha za Chadema kwenye mikutano yao ya kampeni. Jambo moja lililo dhahiri ni kuwa hawajajua namna ya kutumia rangi kujenga acceptance, ushirikiano, kukubalika, kupendwa na cohesion ya aina fulani. Naamini tatizo moja ni hilo la magwanda kwa sababu viongozi hawawezi kujiona wanapendeza au wanavutia nje ya makombati na tatizo la pili ni kuwa bendera ya Chadema ina rangi nyingi kidogo (nyekundu, nyeupe, bluu na nyeusi). Hili la pili linafanya ni vigumu sana kuwa na rangi ya kuunganisha wanachama wote.

Hivyo utaona kule Moshi kwenye mikutano wamevaa nyekundu, Dar kwaenye mikutano wamejivalia rangi mbalimbali au hata bila rangi na hivyo ukiangalia mkutano wa Chadema na wa CCM unaona kuwa CCM inakubalika zaidi, ina watu wengi zaidi na inapendwa zaidi.

Ni katika kufikiria hivyo nimeona kuwa ni lazima kucounter hiyo perception kwa Chadema kutumia rangi nyeupe pe (pure white). Siyo nyeupe na bluu kama NCCR au Bluu bahari kama CUF bali rangi nyeupe kabisa hata inayong'ara.

Rangi nyeupe inaendana na ujumbe wa Chadem:

a. Ni usafi - Chadema inasema kuna uchafu na wanataka kuleta usafi
b. Ni Uadilifu - Kinyume cha sifa ya ufisadi na ubadhirifu.
c. Ni Amani - kwamba mabadiliko wanayoyataka kuleta siyo ya vurugu, au shari bali ni mapinduzi ya amani.


So, ningekuwa nina uwezo wa kutoa ushauri mdogo tu ningetumia saikolojia ya rangi kuweza kuonesha jinsi Chadema inakubalika, kupendwa na kuwa na mwonekano (perception) kuwa ni ya umoja wake. Hata makamanda katika makombati yao wanaweza kujiadorn na white lesos!

Just a thought.. you can continue to dismiss it.
Samahani mkuu,ati umehama CCJ?
 
kubadili sare katikati ya mapambano si vema, HOWEVER
-Chadema wachukue ushauri wa kupamba kwa rangi nyeupe kwenye majukwaa,
-wanachama wavae tishts nyeupe na mashati meupe yaliyo cheap
-Makamanda waendelee na magwanda na skafu nyeupe

nimependa hii.. shukrani.
 
Not really mkuu!!
Ni suala la kujipanga tu... I expect CHADEMA have a tactical team in place which can absorbs operational changes!! Hii ni vita mkuu! Believe me color can make a difference!

Nakubali sana mkuu na naipenda sana hii ila naogopa wapinzani wa chadema wasijesema kuwa hana msimamo ukizingatia watz wengi walivyorahisi kudanganyika wanaweza amini!
 
I don't think so.. kila kampeni ni lazima ijifunze kuadjust, adapt na kubadilika .. you need to have some kind of fluidity..

Nakubali sana mkuu na naipenda sana hii ila naogopa wapinzani wa chadema wasijesema kuwa hana msimamo ukizingatia watz wengi walivyorahisi kudanganyika wanaweza amini!
 
Kama hizi Tshirt ni nzuri saaana.

attachment.php


Au hii hapa chini: Ni ile yenye rangi nyeupe pekeee........ Zaidi angalia hapa uone za Kike na Kofia za Mbayuwayu :
https://www.jamiiforums.com/uchaguzi-tanzania-2010/70548-mbayuwayu-t-shirt-and-caps.html

attachment.php
 

Attachments

  • Mbayuwayu design Men 1.jpg
    Mbayuwayu design Men 1.jpg
    25.3 KB · Views: 138
Back
Top Bottom