Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Nimeangalia kwa muda sasa picha za Chadema kwenye mikutano yao ya kampeni. Jambo moja lililo dhahiri ni kuwa hawajajua namna ya kutumia rangi kujenga acceptance, ushirikiano, kukubalika, kupendwa na cohesion ya aina fulani. Naamini tatizo moja ni hilo la magwanda kwa sababu viongozi hawawezi kujiona wanapendeza au wanavutia nje ya makombati na tatizo la pili ni kuwa bendera ya Chadema ina rangi nyingi kidogo (nyekundu, nyeupe, bluu na nyeusi). Hili la pili linafanya ni vigumu sana kuwa na rangi ya kuunganisha wanachama wote.
Hivyo utaona kule Moshi kwenye mikutano wamevaa nyekundu, Dar kwaenye mikutano wamejivalia rangi mbalimbali au hata bila rangi na hivyo ukiangalia mkutano wa Chadema na wa CCM unaona kuwa CCM inakubalika zaidi, ina watu wengi zaidi na inapendwa zaidi.
Ni katika kufikiria hivyo nimeona kuwa ni lazima kucounter hiyo perception kwa Chadema kutumia rangi nyeupe pe (pure white). Siyo nyeupe na bluu kama NCCR au Bluu bahari kama CUF bali rangi nyeupe kabisa hata inayong'ara.
Rangi nyeupe inaendana na ujumbe wa Chadem:
a. Ni usafi - Chadema inasema kuna uchafu na wanataka kuleta usafi
b. Ni Uadilifu - Kinyume cha sifa ya ufisadi na ubadhirifu.
c. Ni Amani - kwamba mabadiliko wanayoyataka kuleta siyo ya vurugu, au shari bali ni mapinduzi ya amani.
So, ningekuwa nina uwezo wa kutoa ushauri mdogo tu ningetumia saikolojia ya rangi kuweza kuonesha jinsi Chadema inakubalika, kupendwa na kuwa na mwonekano (perception) kuwa ni ya umoja wake. Hata makamanda katika makombati yao wanaweza kujiadorn na white lesos!
Just a thought.. you can continue to dismiss it.
Hivyo utaona kule Moshi kwenye mikutano wamevaa nyekundu, Dar kwaenye mikutano wamejivalia rangi mbalimbali au hata bila rangi na hivyo ukiangalia mkutano wa Chadema na wa CCM unaona kuwa CCM inakubalika zaidi, ina watu wengi zaidi na inapendwa zaidi.
Ni katika kufikiria hivyo nimeona kuwa ni lazima kucounter hiyo perception kwa Chadema kutumia rangi nyeupe pe (pure white). Siyo nyeupe na bluu kama NCCR au Bluu bahari kama CUF bali rangi nyeupe kabisa hata inayong'ara.
Rangi nyeupe inaendana na ujumbe wa Chadem:
a. Ni usafi - Chadema inasema kuna uchafu na wanataka kuleta usafi
b. Ni Uadilifu - Kinyume cha sifa ya ufisadi na ubadhirifu.
c. Ni Amani - kwamba mabadiliko wanayoyataka kuleta siyo ya vurugu, au shari bali ni mapinduzi ya amani.
So, ningekuwa nina uwezo wa kutoa ushauri mdogo tu ningetumia saikolojia ya rangi kuweza kuonesha jinsi Chadema inakubalika, kupendwa na kuwa na mwonekano (perception) kuwa ni ya umoja wake. Hata makamanda katika makombati yao wanaweza kujiadorn na white lesos!
Just a thought.. you can continue to dismiss it.