CHADEMA, Wanaharakati waalikeni waungwana mpatanishwe

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,997
35,988
Huu ni ushauri wa bure kwa CHADEMA na Wanaharakati (wote ndani na nje), ikiwapendeza, waungwana kabisa.

Kutoka kwa mwananchi, mdau.

Kwenu waheshimiwa, niwasalimu kwa jina la solidarity: "Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu."

Tulikuwa tuko vizuri. Tulikuwa wamoja. Tulikuwa tukitembea vifua mbele kuelekea kwenye nchi ya ahadi. Nchi yenye asali na maziwa. Shetani gani katupitia, ghafla tushindwe kuelewana?

Wanasema waswahili, ndugu wawili wakigombana, chukua jembe ukalime. Siku wakipatana, chukua kapu ukavune. Misahafu inasema, heri wapatanishi kwa maana hao wataitwa wana wa Mungu.

Tusikubali kufarakanishwa kirahisi. Tusikubali kufarakana kirahisi. Tunajenga nyumba moja. Pamoja, tuko vizuri zaidi.

Kulikoni kutowafikiria viongozi wa dini au hata na waungwana wengine, wa ndani na nje ya vyama au hata ndani na nje ya nchi, ili kuwezesha kusaka mapatano?

Kulikoni kutowafikiria waungwana kama TEC, KKKT, Waislam, madhehebu zingine nk au hata na wasomi, wakiwamo nguli? Hawawezi kutuangusha watu hawa. Wengi wao wamekuwa nasi katika dhiki hizi za mapambano.

Fikiria akina Sheikh Ponda, Askofu Bagonza, Askofu Niwemugizi, Prof. Shivji, Askofu Mwamakula (pole zake kwa msiba) nk, nk, kwenye jopo kama hilo?

Kwamba wengine tumelazimika kupiga kelele hivi, tukisisitiza kutafuta mapatano bila kujali changamoto zote zilizotukabili, ni kwa sababu tukiamini Tanzania ya namna hii:

IMG_20231011_141544.jpg


Ilikuwa karibu zaidi katika umoja wetu kuliko wakati mwIngine wowote. Fikiria Tanzania hiyo. Kizuizi gani Ya-Rabi kiwepo njiani hapo, kitushinde kukiondoa kwa ajili ya ushindi huu ulio karibuni na dhahiri hivyo?

Kulikoni tusiweke yoyote binafsi pembeni, tukajaribu kutafuta mapatano? Ikishindikana, basi ikawe imekuwa bahati mbaya. Kwamba haikuwa riziki, ila kwa dhati yetu kabisa, tulijaribu?

Wakulima wanasema majembe yaliyopo pamoja kukwaana, hutokea. Tutafute mapatano nafasi hii ya dhahabu tulipo, isituponyoke kirahisi.

Kutengana kwa makundi mawili haya ni hasara kubwa kwa yote. Hali ni faida kubwa mno kwa mahasimu wetu wasiopenda katu, tuelewane.

Wanasema waswahili, "Wagombanao, ndiyo wapatanao." Tumtangulize Mola mbele. Palipo yeye hakuna lisilowezekana. Penye nia, pana njia.
 
Huu ni ushauri wa bure kwa CHADEMA na Wanaharakati (wote ndani na nje) ikiwapendeza waungwana kabisa.

Kutoka kwa mwananchi, mdau.

Kwenu waheshimiwa, niwasalimu kwa jina la solidarity: "Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu."

Tulikuwa tuko vizuri. Tulikuwa wamoja. Tulikuwa tukitembea vifua mbele kuelekea kwenye nchi ya ahadi. Nchi yenye asali na maziwa. Shetani gani katupitia, ghafla tushindwe kuelewana?

Wanasema waswahili, ndugu wawili wakigombana, chukua jembe ukalime. Siku wakipatana, chukua kapu ukavune. Misahafu inasema, heri wapatanishi kwa maana hao wataitwa wana wa Mungu.

Tusikubali kufarakanishwa kirahisi. Tusikubali kufarakana kirahisi. Tunajenga nyumba moja. Pamoja, tuko vizuri zaidi.

Kulikoni kutowafikiria viongozi wa dini au hata na waungwana wengine, wa ndani na nje ya vyama au hata ndani na nje ya nchi, ili kuwezesha kusaka mapatano?

Kulikoni kutowafikiria waungwana kama TEC, KKKT, Waislam, madhebu zingine nk au hata na wasomi, wakiwamo nguli? Hawawezi kutuangusha watu hawa. Wengi wao wamekuwa nasi katika dhiki hizi za mapambano.

Fikiria akina Sheikh Ponda, Askofu Bagonza, Askofu Niwemugizi, Prof. Shivji, Askofu Mwamakula (pole zake kwa msiba) nk, nk, kwenye jopo kama hilo?

Kwamba wengine tumelazimika kupiga kelele hivi, tukisisitiza kutafuta mapatano bila kujali changamoto zote zilizotukabili, ni kwa sababu tukiamini Tanzania ya namna hii:

View attachment 2779321

Ilikuwa karibu zaidi katika umoja wetu kuliko wakati wowote. Fikiria Tanzania hiyo. Kizuizi gani Ya-Rabi kiwepo njiani hapo, kitushinde kukiondoa kwa ajili ya ushindi huu ulio karibuni na dhahiri hivyo?

Kulikoni tusiweke yoyote binafsi pembeni, tukajaribu kutafuta mapatano? Ikishindikana, basi ikawe imekuwa bahati mbaya. Kwamba haikuwa riziki, ila kwa dhati yetu kabisa, tulijaribu?

Wakulima wanasema majembe yaliyopo pamoja kukwaana, hutokea. Tutafute mapatano nafasi hii ya dhahabu tulipo, isituponyoke kirahisi.

Kutengana kwa makundi mawili haya ni hasara kubwa kwa yote. Hali ni faida kubwa mno kwa mahasimu wetu wasiopenda katu, tuelewane.

Wanasema waswahili, "Wagombanao, ndiyo wapatanao." Tumtangulize Mola mbele. Palipo yeye hakuna lisilowezekana. Penye nia, pana njia.
Kila la heri!
 
Mwabukusi, na mdude wakaribishwe chadema maana kule NCCR serikali imesha pora chama na Mwabukusi pale hachomoi. Mahala pekee anaweza kufikisha ujumbe wake ni akiwa chadema, lakini akikubali Dr.Slaa ammiliki hatofika popote.
Aachane na Dr.Slaa ajiunge Chadema.
Mwabukusi Alihama CHADEMA baada ya kushindwa uchaguzi wa mwenyekiti wa kanda ya Nyasa,Alihama kwa kuahidiwa ubunge wa Busokelo na Mbatia kwa msaada wa Magufuli.
Leo anataka kuitumia CDM kujibebea umaarufu,abaki huko huko NCCR asitake CHADEMA ionekane mbaya kwa tamaa zake
 
Wakati ni huu ni vizuri kutambua umefuatana na akina nani ili ujue namna nzuri ya kujizoesha kukaa nao ili nao wakzoee na baadae muendelee katika safari yenu ndefu. Nasema safari ndefu nikimaanisha hivyo.
 
Kila la heri!

Wanasema waungwana: "well said."

Fikiria wakiwamo wenye mawazo haya:

Screenshot_20231012-070427~2.jpg


(Juu ni case ya Lissu kurudi Loliondo)

Screenshot_20231012-070530.jpg


(Hapa juu ni kwenye kadhia ya wamasai kuondolewa Loliondo)

Kwamba hata wawili hao, leo ni katika walio mstari wa mbele kushabikia mafarakano.

Kwamba wanalia kuliko wafiwa?

Tangu lini watu kama hao waitakie mema CHADEMA au wana HARAKATI?

Suluhu haiwezi kuwa hadharani, mitandaoni aghalabu hata kupatikania humu JF.

"Suluhu ni ana kwa ana, faragha. Labda mbele ya mediators wenye kheshimika au kuaminika."

Kutofautiana mawazo si dhambi. Kukubali kutofautiana kimawazo ni jambo la afya.

"Ni mawazo yangu kuwa tuwe wastahamilivu kweli kweli hapa. Kusulihisha mambo hadharani machoni pa watesi wetu inataka kipaji na hekima ya kimbingu."

Screenshot_20231012-065829.jpg


Mungu ibariki CHADEMA, Mungu wabariki Wana HARAKATI.
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Chadema wanasumbuliwa na hofu na wivu wakidhani wanaharakati wanaweza kuingilia ulaji wao. Kama kweli mnapigania kitu kimoja, kuna haja gani ya kuanza kuvuana nguo? Au Chadema ni kama TLP na Mremavu?

Mada inaongelea suluhu.

Kulikoni tusiwape wa aina ya:

"Sheikh Ponda, Askofu Bagonza, Askofu Niwemugizi, Prof. Shivji, Askofu Mwamakula, nk," nafasi?

Busara zao zikiwaleta pamoja nini tatizo gani?

Kwamba:

Dkt. Rugemeleza Nshala: Nimetishiwa maisha baada ya kutoa maoni kuhusu mkataba wa Bandari na DP World

Kwa kauli hizi:

Screenshot_20231012-084514.jpg


Miluzi mingi humpoteza mbwa.
 
CHADEMA imegombana na wanaharakati gani? Au kuna wanaharakati uchwara wanalazimisha ugomvi na CHADEMA Ili wapate mileage?

Nadhani mada hujaisoma au hukuielewa:

"Hakuna popote panaposema nani kagombana na nani?" Au hata "nani kafanya nini."

Zingatia:

"Huu ni ushauri wa bure kwa CHADEMA na Wanaharakati (wote ndani na nje) ikiwapendeza waungwana kabisa hawa."

"Kutoka kwa mwananchi, mdau."


Kumbuka:

1. Kupatanishwa si lazima uwepo ugomvi.
2. Mada haina cha kufanya na ugomvi hata kama upo.
3. Malalamiko ya upande wowote kama yapo, ni huko kwenye usuluhishi.
4. Yote kheri, na ni kama itawapendeza.
 
Mwabukusi, na mdude wakaribishwe chadema maana kule NCCR serikali imesha pora chama na Mwabukusi pale hachomoi. Mahala pekee anaweza kufikisha ujumbe wake ni akiwa chadema, lakini akikubali Dr.Slaa ammiliki hatofika popote.
Aachane na Dr.Slaa ajiunge Chadema.

Uko nje ya mada mkuu. Yumkini hujaisoma au hukuielewa:

Hakuna popote panapo mtaja awaye yote. Wanaharakati ni zaidi ya hawa uliowataja wewe. Hata wanasiasa (wakiwamo CHADEMA) ni wanaharakati."

Harakati ni jitihada za kuleta mabadiliko. Anayeshiriki au kujihusisha humo ni mwanaharakati.

Humo wamo wote, isipokuwa CCM (asiyetaka mabadiliko). Kinacho tofautiana ni mbinu tu ila ni uanaharakati ule ule.

Zingatia kuhusiana na mada, iko wazi:

"Huu ni ushauri wa bure kwa CHADEMA na Wanaharakati (wote ndani na nje) ikiwapendeza waungwana kabisa hawa.

Kutoka kwa mwananchi, mdau."


Imewekwa wazi:

"Yote kheri, na ni kama itawapendeza."

Rejea uliyoandika, kujiridhisha.
.
 
Wakati ni huu ni vizuri kutambua umefuatana na akina nani ili ujue namna nzuri ya kujizoesha kukaa nao ili nao wakzoee na baadae muendelee katika safari yenu ndefu. Nasema safari ndefu nikimaanisha hivyo.

Ninakusoma vyema na kutambua kuwa "safari ni ndefu na una maanisha."

Ninatambua uwepo wa mawazo tofauti ya dhati kabisa. Nafasi tofauti si nadra kutofautiana.

Hata hivyo na wachawi nao (ma CCM) hawachezi mbali. Ninatambua hao kama walivyokuwa kenge kwenye msafara wa mamba nao wamo.

Hao watafanya kila kitu kutufarakanisha. Ninasema kila kitu nikiwa ninamaanisha hivyo.

Au nasema uongo Moisemusajiografii na ndugu wadau?
 
Ninakusoma vyema na kutambua kuwa "safari ni ndefu na una maanisha."

Ninatambua uwepo wa mawazo tofauti ya dhati kabisa. Nafasi tofauti si nadra kutofautiana.

Hata hivyo na wachawi nao (ma CCM) hawachezi mbali. Ninatambua hao kama walivyokuwa kenge kwenye msafara wa mamba nao wamo.

Hao watafanya kila kitu kutufarakanisha. Ninasema kila kitu nikiwa ninamaanisha hivyo.

Au nasema uongo Moisemusajiografii na ndugu wadau?
Huna baya tajiri bilionea.
 
Back
Top Bottom