Elections 2010 CHADEMA: Tatizo la KUHARIBU KURA Elimu inahitajika Sasa!

mozze

Senior Member
Aug 27, 2010
185
28
kwa viongozi, wanachama na wapenzi na mashabiki kazi kubwa ni kuhakikisha wapiga kura wanaelewa UPIGAJI KURA ili Kupata Kura zote zinazoelekea Chadema otherwise mambo yanaweza yasiwe kama inavyotarajiwa!

Ili kuhakikisha Chadema haipotezi ushindi ni muhimu kuhakikisha Wananchi wanapiga kura kwa umakini ili KURA ZISIHARIBIKE. Waelezwe kuwa wanatakiwa KUWEKA ALAMA YA VYEMA TU, na wasiandike zaidi kwenye ile karatasi ya Kura.

Miaka ya nyuma CUF walipoteza kura nyingi sana, hasa Temeke, kwa sababu wafuasi wao waliweka VYEMA kwa mtu wa CUF halafu wakachorachora picha za CCM. Ukifanya hivyo Kura inakuwa imeharibika.

Hili Linatokea sana hasa ushabiki unapozidi kuliko upenzi!NI MUHIMU SANA kuhakikisha hili swala linajulishwa kwa wapiga kura katika hizi 2weeks zilizobaki.

Wagombea Ubunge, Udiwani na urais wote wapewe maelekezo ya kuwaelimisha wapiga kura wakati wa kura zao!
 
Back
Top Bottom