CHADEMA 'Lowassa siyo fisadi', CCM 'Lowassa ni fisadi'

Kama lengo pekee la Upinzani ni kwenda Ikulu kwa walichofanya ni sawa kabisa. Ikulu ndo target hata Taifa zima wafe, waingie Ikulu kilichofanyika ni sahihi kabisa. Ila kama upinzani ni kuwasaidia wananchi, kupigania haki zao, kuonyesha madhaifu ya chama Tawala hapo watakuwa wamecheza mchezo mbaya sana. Jingine kubwa wajue wanaweza kushika Dola na kwa kawaida alieko nje ya dola huona makosa mengi sana mabaya yalioko kwenye dola. Tusubiri na tuone. Mungu ibariki Tanzania.
 
Ukweli si huu hebu wenye ujasiri waende hatua moja mbele '' ngazi za juu'' ni nani na wapo wapi kwa sasa mbona hamjawakata?
Swali: Mh. Edward Lowassa unazungumiaje kuhusu kashfa ya Richmond?

Majibu Lowassa: Nipende tu kusema mimi kama waziri mkuu kwa kawaida ya sheria huwa ninaletewa mkataba muda wa mwisho kuupitia na kuupitisha huwa sihusiki na kuandaa mikataba,mwenye mamlaka ni waziri husika,hivyo baada ya kuletewa mkataba husika wa Richmond niliupitia na kiukweli niliuwekea shaka kwa sababu nilishawahi kuwa waziri wizara ya maji nina uzoefu na kuandaa mikataba,nilishauri mkataba huo uvunjwe lakini waziri wa nishati akawasiliana na "NGAZI YA JUU"na kulazimishwa kuupitisha mkataba huo.

Baada ya kugundulika kuwa mkataba huo ulikuwa na mapungufu mengi, "NILICHUKUA MAAMUZI MAGUMU KWA AJILI YA SERIKALI,na kubeba mzigo wote ndio maana hadi leo wanasema mimi ni FISADI WA RICHMOND.

Ametaja sasa na bado mnao.




 
Wasio weledi wa idara ile wamevamia jukwaa! Tu welevu you simply can't easily change our mindset! Andikeenii, jifanyeni wajuajiii, hamtampata MTU.

All we need is a system change
 
Wasio weledi wa idara ile wamevamia jukwaa! Tu welevu you simply can't easily change our mindset! Andikeenii, jifanyeni wajuajiii, hamtampata MTU.

All we need is a system change

Waondoke tuu maana hii system ishaota makucha mazito hatuwaitaji wanaifanya nchi ya familia zao.
 
Ni vigumu kwa tajiri kupenya na kuingia kwenye ufalme wa mbinguni, ni afadhali ngamia kupenya kwenye tundu la sindano. Kama uraisi ni wa kutafuta kwa kila namna, ni hatari sana. watanzania tufikiri kwa kina sana.
 
Ndugu Tetty,

Una hoja kabisa. Lakini pia naamini kwamba huwezi kuiba mitihani ili upate A zote kama unaongozwa na maadili. Njia hii ndio questionable. Uwezo ilioujenga Chadema miaka nenda miaka rudi ni mkubwa sana. Si hivyo tu, wamejiongeza na kuunda UKAWA. Bado UKAWA haujawa tested tunasikia Lowassa. This is where the problem starts about our opposition leaders credibility. Kwa sababu msingi mzima wa kupinga ufisadi umeyeyuka kwa maslahi ya muda mfupi.

Uamuzi walioufanya ni wa haraka mno.Nina uhakika Dr.Slaa angeweza kufanikiwa kupata nafasi na pia uwezo wa CDM kupata wabunge wengi,sijui ni kwanini hawakujiamini.

Pili wangeweza kumchukua Lowassa lakini akawa mwanachama wa kawaida..ili kuisaidia team ya CDM kuweza kuongoza...Kwa kweli I will vote for JJMnyika lakini Rais sitapiga.Na hii itakuja kama JJMnyika atagombea maana hata yeye hajulikani msimamo wake.
 
Kila zama na nabii wake na kila awamu na rais wake. Huenda wakati mwalimu Nyerere ana mtuhumu Edward Lowasa kipenzi cha wananchi hakuwahi kumpa nafasi ya kujitetea ndo maana watu wanadhani kuwa mwalimu kila alicho kisema kilikuwa sawa kiasi cha kumfananisha na nabii au mitume wa Mungu.

Kuna mambo mengi ambayo Mwalimu aliongoza kwa utashi wake kama binadamu ama yalipendwa au kuchukiwa na wengi,lakini Mwalimu ataendelea kuwa binadamu na zama zake zilikwisha pita kilicho baki tunajifunza kutokana na mazuri na mabaya yake.

Leo nchi imegubikwa na gumzo la mtia nia ya urais kupitia CHADEMA kuwakilisha kundi la umoja wa katiba ya wananchi(UKAWA),kundi kubwa la wananchi hususani wanyonge lina imani naye,lakini na wafanyabiashara wa kada zote wana imani naye pia. Dalili ya kukubalika kwake ni tabia yake ya kukunjika na kkukubali kuwajibika pale panapobidi ili kutekeleza misingi ya utawala bora. Serikali yake ilituhumiwa kutokana na ufisadi mkubwa wa mkataba tata wa Richmond,alistukia ukiukwaji wa taratibu za mkataba alishauri kwa mamlaka ya juu lakini ilishindikana.

Serikali yake ilibanwa bungeni na alikubali kuwajibika kisiasa kuinusuru serikali na chama alichokitumikia karibu nusu ya maisha yake yote. Alijiuzuru,lakini licha ya kujiuzuru pamoja na tuhuma hizo serikali ilishindwa kabisa kumshitaki kwenye vyombo vya sheria kutokana na kadhia hiyo ima kwa kujua nini kilicho nyuma ya pazia na kuogopa kuumbuka au ikijua nini hatima ya kashfa hiyo.

Alizungumza kwenye CC ya chama wakati wa kuvuana gamba, Lowasa aliweza kuwabana waliokuwa wana eneza ufisadi wake na hatimaye maazimisho ya kuzaliwa CCM yaliyofanyika huko Mwanza,mwenyekiti wa CCM taifa alitoa ufafanuzi wa kauli ya kuwavua gamba wanachama wake akiwemo mh. Lowasa kuwa mapokeo yalipokelewa vibaya na mwisho wa slogan ya kuvuana gamba ilipozikwa rasmi.

Si hapo tu,rais aliweza pia kumnadi kuwa ni kiongozi msafi na kuwataka wananchi wa Monduli wasimpoteze kiongozi wao kwa kumpa kura za heshima. Aliweza pia kuelezea wasifu wa utendaji kazi wake kwenye mkutano wa kuvunja bunge kwa kumsifia aliyekuwa waziri mkuu wake ,lakini leo yamegeuka na kuwa kashfa iliyokuwa ikipingwa na wana CCM na wapenzi wake. Kosa lake nini,kuhama chama,tumeona watu wanahama dini lakini hakuna anaye kashifu sembuse huyo aliyehama chama kutokana na chama kugeuzwa kampuni ya familia

Watanzania wana imani naye,ndiyo maana kila alipojitokeza watu walimlaki na kumshawishi kutokana na uzoefu wake wa uwaziri mkuu kwa kipindi cha miaka miwili. Tulitegemea chama kikubwa kama CCM kuwa kioo cha kujenga na kudumisha demokrasia kwa kujikita kwenye miongozo ya katiba yao katika mchakato wa kuwachuja wagombea wake. Kilichofanyika kilipingwa na wanachama watatu walionyesha hisia zao kwa kupinga kamati ya maadili kukiuka maadili na kupoka mamlaka ya kamati kuu katika kuwachuja wagombea. Lakini ikumbukwe siku za nyuma vijana wa CCM mkoa wa Pwani walitoa tamko ambalo laiti kama si uvumilivu wa Watanzania lingeweza kuzua mgogoro wa kikatiba kwa kuwabagua wananchi kwa misingi ya ukanda,eti rais ajaye hawezi toka kaskazini.

Kumshambulia Lowasa kwa wanachama hawa wa chama chake cha zamani kinatafsiriwa kuwa ni mgagaa na upwa..........ikiwa wao walimuona wa kazi gani wengi wameona ana faida kwao. Kelele na matamko mbalimbali toka chama cha Mapinduzi ni matokeo ya kauli ya hayati Horace Kolimba kuwa chama kimekosa dira na mwelekeo. Ni ukweli usiopingika kuwa unapo ianza safari wana kutia moyo,unapo onyesha mafanikio hao hao wanainua vikwazo kama si uhuni nini!

Nyota ya UKAWA inang'aa toka mashariki ya mbali ni kazi kwetu kuhakikisha mamajusi hawarudi kukutana na mfalme Herode ili safari yetu ya ukombozi iweze timia. Ukombozi wa taifa hili uko mikononi mwetu ndo maana wajengao mnara wa Babel wameanza kutofautiana lugha. Ni kipindi cha historia mpya kuandikwa nchini mwetu,kama ni mabadiliko hata walio ndani ya nyumba hiyo hiyo nao wanalia kilio kimoja na sisi tulio nje ya nyumba hiyo je wewe una ngoja nini!
 
Imchafue mara ngapi? Hukusikia El alivyosema wamemchafua katika op magamba?
 
Alilopanga Mungu haliwezi kubatilishwa na mwanadamu. Hata waongee maneno yote wanajisumbua tu lakini Mungu amjua mtu wake alimuandaa kuwakomboa watanzania kutoka katika ukandamizaji wa haki na lindi la kutisha la umaskini. Kama viongozi wa juu hawatendeani haki itakuwaje kwa watanzania wakawaida? Ndio maana Bwana Yesu alisema kama wanaweza kutendea mtu mbichi namna hii itakuwaje kwa mti mkavu? Watanzania amkeni tuikomboe nchi na tuachane na ushabiki usiokuwa na maana yoyote.
 
Kama Unaushaidi peleka mahakamani,Kama Hauna "shut-up"



Hiyo ni sentence fupi aliyoitoa kamanda Lowassa kwa wale mavuvuzela wa kisiasa wakiongozwa na Nape na Makonda.
Na baada ya sentence hiyo Lowassa kawa huru na roho nyeupe kama nywele zake.
Bila kusahau alitakata zaidi na kugeuka nuru pale aliposema"Mimi niliambiwa ni maagizo kutoka juu"
"lowassa"Umeanza na mungu na Utamaliza na mungu,UKAWA ni mpango wa mungu.
 
Sikumpenda kabisa kwanza kutokana na wana CCM kumkubali sana kuwa ndiye Raisi ajaye nakila mtu niliyekuwa nikimuuliza kwa rika tofauti alimtaja kama ndiye Rais.

Rakini lapili ni yeye kuwa MwanaCCM chama ambacho sina imani nacho,na kila mwana CCM niliyekuwa nikimuuliza kwanini Fisadi ashinde alimsafisha kuwa tuhuma zile hazikuwa zake.

Lakini la tatu ni namna nilivyo muamini Kikwete 1995 na hatimaye 2010 kwa kazi alizowahi kufanya kama kufunga akaunti ya Kigoma Malima aliyekuwa ameficha pesa nje ya nchi.Wengi tuliamini kuwa walafi Wa pesa zetu wamekwisha atawamaliza wote.

Kinyume chake ni kuwa Kigoma alifilisiwa kwa sababu alikuwa anahama chama .Kwa utaratibu Wa CCM ni kulindana.

CCM imejilimbikizia Mali ilizochuma kwa WATZ kwa manufaa ya chama kama viwanja vya Mpira Shule nk.
Huyu Lowasa alikuwa ndiye mpanga mipango ya kudhurumu wapinzani sasa mbinu nyigi anazifahamu kura nitampa hata kama mgonjwa kama nilivyompa mgonjwa aliyekuwa anadondoka majukwaan 2005.

Mfumo Wa CCM No kulindana na kuwatoa kafara usiowapenda.

Sasa Niko naye katika safar ya matumaini.Lowassa umewajua marafiki Wa kweli engine jina lilipokatwa tu walikukimbia,lakini engine Wapo CCM kimwili kiroho wako nawe waache wafanye kazi huko.
 
Katika kile kinachoendelea kwenye siasa za Tanzania watu hasa CCM wameshikilia bango kuwa waziri mkuu mstaafu ndg Edward Lowasa eti ni fisadi ndio maana hawakumteua kupeperusha bendera ya CCM ktk kinyang'anyiro cha urais wa JMT.
Wengi wao waki-recall tukio la Mwembe Yanga " LIST OF SHAME" hivyo hiyo ndio imekuwa kete yao pamoja na mambo mengine kumfanya akose sifa ya kuteuliwa ktk nafasi hiyo.
Lakini inapaswa tujiulize List of Shame haijamtaja Edo peke yake hata mkuu wa kaya alitajwa na wengine kibao wakiwemo mawaziri na wanachama wengine wa CCM.
Mbona hao hawataji kama wanavyotaja sasa hivi ndg Edo?
 
Huo wimbo wa ufisadi ni wenu, mwambieni Mzee SLAA na wenzake waendelee kuuimba.MSIHANGAIKE tushajua rangi zenu.
 
Back
Top Bottom