Mshume Kiyate
JF-Expert Member
- Feb 27, 2011
- 6,766
- 894
KATIBU wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) mkoani Tanga, Benson Mramba. amemweleza Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Professor Ibrahim Lipumba kuwa ni mwanasiasa aliyefirisika kisiasa na kisera.
Mramba pia amemtaka Profesa Lipumba, asome alama za nyakati ili kujua umuhimu wa mabadiliko kwa Watanzania, badala ya kuwa wakala wa CCM. Alikuwa akijibu madai ya Profesa Lipumba, kuwa yoyote anayeamini kuwa Chadem itatawala nchi, ni mgonjwa na anapaswa kwenda kwa Mchungaji Ambikile Masapila, kupata kikombe cha dawa.
Mramba alisema Profesa Lipumba, anajidanganya na kwamba Chadema ni taasisi na si chama kinachotegemea umaarufu wa mtu mmoja, kama ilivyo CUF. Alisema kwa msingi huo, chama hicho kitashika dola bila wasiwasi. Alimataka Mwenyekiti huyo kupumzika katika duru za kisiasa kwa kuwa hana jipya la kuwaambia wananchi.
Chadema inajiamini na ipo kwa ajili ya kuwakomboa wananchi wa Tanzania.
SOURCE: Mwananchi Machi 31, 2011
Mramba pia amemtaka Profesa Lipumba, asome alama za nyakati ili kujua umuhimu wa mabadiliko kwa Watanzania, badala ya kuwa wakala wa CCM. Alikuwa akijibu madai ya Profesa Lipumba, kuwa yoyote anayeamini kuwa Chadem itatawala nchi, ni mgonjwa na anapaswa kwenda kwa Mchungaji Ambikile Masapila, kupata kikombe cha dawa.
Mramba alisema Profesa Lipumba, anajidanganya na kwamba Chadema ni taasisi na si chama kinachotegemea umaarufu wa mtu mmoja, kama ilivyo CUF. Alisema kwa msingi huo, chama hicho kitashika dola bila wasiwasi. Alimataka Mwenyekiti huyo kupumzika katika duru za kisiasa kwa kuwa hana jipya la kuwaambia wananchi.
Chadema inajiamini na ipo kwa ajili ya kuwakomboa wananchi wa Tanzania.
SOURCE: Mwananchi Machi 31, 2011