GeniusBrain
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 4,315
- 306
Jana yalifanyika maadhimisho ya miaka 48 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambapo viongozi mbali mbali wa vyama vyote vya siasa walihudhuria isipokuwa CDM peke yao. Hii ni ishara mbaya kwa chama cha siasa kinacho tafuta ridhaa ya watanzania ya kuongoza nchi kujitenga na sherehe za kitaifa. Ikumbukwe kuwa sherehe hizi za Kitaifa hazipo Tanzania tu, zipo duniani kote na huwa ni za wananchi wote bila kutizama itikadi za vyama vyao. Kwani hata CDM wakipata ridhaa ya watanzania hizi sherehe watazifanya tu. CDM pevukeni kifikra na kimawazo mnajishusha hadhi yenu kwa vitu km hivi na ndipo watu wanakuja na hoja ya kuwa mna ajenda za kuvuruga nchi pindi mtakapo pewa madaraka