Kamende
JF-Expert Member
- Mar 1, 2008
- 416
- 45
Baada ya kutoa taarifa za uongo kuhusu CHADEMA kumiliki silaha mbali mbali zikiwepo Magobore, mapanga, visu na tindikali mbele ya vyombo vya habari sasa RPC wa mkoa wa Kagera Salewi anakabiliwa na wakati mgumu baada ya CHADEMA kuamua kumfikisha mahakamani kwa tuhuma ya kukichafua na kuudanganya umma.
Kamanda wa uchaguzi wa CHADEMA mjini hapa alisema kuwa kama Salewi angekuwa mstaarabu angetokeza mbele ya jamii tena kuomba radhi baada ya jeshi lake kufanya upekuzi na kukuta kuwa gari letu halina kitu chochote cha hatari.
"Kutokufanya hivyo kunatudhihirishia sisi na umma mzima wa watanzania kuwa hatua ya kukichafua chama ilikuwa ni kutekeleza agizo la CCM" Tunamfikisha mahakamani ili aijue thamani ya dhamana aliyopewa na nchi yetu". Alisema John Mrema ambaye ndiye kamanda wa uchaguzi Biharamulo kwa CHADEMA.
Kamanda wa uchaguzi wa CHADEMA mjini hapa alisema kuwa kama Salewi angekuwa mstaarabu angetokeza mbele ya jamii tena kuomba radhi baada ya jeshi lake kufanya upekuzi na kukuta kuwa gari letu halina kitu chochote cha hatari.
"Kutokufanya hivyo kunatudhihirishia sisi na umma mzima wa watanzania kuwa hatua ya kukichafua chama ilikuwa ni kutekeleza agizo la CCM" Tunamfikisha mahakamani ili aijue thamani ya dhamana aliyopewa na nchi yetu". Alisema John Mrema ambaye ndiye kamanda wa uchaguzi Biharamulo kwa CHADEMA.