CHADEMA kumbukeni hata Mrema aliwahi kununuliwa nyumba Sinza na Wananchi

Ndugu zangu,

"Kuishi kwingi kuona mengi" huenda haya ninayoyasema sasa ni asilimia ndogo sana walikuwa na ufahamu na wanakumbuka. Kipindi cha muongo wa kwanza wa siasa za vyama vingi kambi ya upinzani ilitawaliwa na Augustine Mrema na vyama vyake kwanza akiwa NCCR-Mageuzi na baadaye TLP.

Mrema akiwa na kauli yake ya "kulipua mabomu" bungeni na nje ya Bunge alisababisha mawaziri kadha wa kadha kung'atuka na hatimaye kuondoka katika siasa.Sera ya "kulipua mabomu" ilisababisha Mrema kuletewa zengwe na kutimuliwa kwenye nyumba ya serikali ambamo aliishi kama mpangaji.

Baada ya watu kusikia kuwa Mrema anaondolowa kwenye nyumba aliyopanga walikusanyika eneo la Manzese Argentina na kutangaza kununua nyumba mara moja na kumpa hati milki ili aendelee "kulipua mabomu".Nyumba ikapatikana Sinza mbapo Mrema na mkewe Rose walihamia na kuishi bila bugdha.

Tabia ya watanzania kusaidia ipo pale pale lakini haimaanishi kuwa watakuchagua uwe Rais wao.Nakumbuka pamoja na wananchi kumnunulia nyumba ilipofika mwaka 2000 kuelekea uchaguzi mkuu Mrema alikataa gari lake kusukumwa baada ya kugundua kuwa linapokuja suala la kura hawampi.


Tutaendelea kuwapa historia vijana wetu na kuwakumbusha waliosahau.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siasa zimebadilika sana na nyakati hizi nawaona wananchi ni kama wanamaanisha sana kutokana na hali halisi …. ukiangalia Maisha ya miaka ya 1990 kuelekea 2000 huwezi kulinganisha na sasa ...bado ajila zilikuwepo kwa kiasi chake … sasa acha tuone , huko tuendako napaona pakiwa na shughuli kubwa sana kutoka mikononi mwa watanzania hawa
 
Ndugu zangu,

"Kuishi kwingi kuona mengi" huenda haya ninayoyasema sasa ni asilimia ndogo sana walikuwa na ufahamu na wanakumbuka. Kipindi cha muongo wa kwanza wa siasa za vyama vingi kambi ya upinzani ilitawaliwa na Augustine Mrema na vyama vyake kwanza akiwa NCCR-Mageuzi na baadaye TLP.

Mrema akiwa na kauli yake ya "kulipua mabomu" bungeni na nje ya Bunge alisababisha mawaziri kadha wa kadha kung'atuka na hatimaye kuondoka katika siasa.Sera ya "kulipua mabomu" ilisababisha Mrema kuletewa zengwe na kutimuliwa kwenye nyumba ya serikali ambamo aliishi kama mpangaji.

Baada ya watu kusikia kuwa Mrema anaondolowa kwenye nyumba aliyopanga walikusanyika eneo la Manzese Argentina na kutangaza kununua nyumba mara moja na kumpa hati milki ili aendelee "kulipua mabomu".Nyumba ikapatikana Sinza mbapo Mrema na mkewe Rose walihamia na kuishi bila bugdha.

Tabia ya watanzania kusaidia ipo pale pale lakini haimaanishi kuwa watakuchagua uwe Rais wao.Nakumbuka pamoja na wananchi kumnunulia nyumba ilipofika mwaka 2000 kuelekea uchaguzi mkuu Mrema alikataa gari lake kusukumwa baada ya kugundua kuwa linapokuja suala la kura hawampi.


Tutaendelea kuwapa historia vijana wetu na kuwakumbusha waliosahau.

Sent using Jamii Forums mobile app
Na ndo maana tunaogopa tume huru ya uchaguzi, otherwise itabidi tufute uchaguzi Kama tulivyofanya Zanzibar vinginevyo ccm itatupwa makumbusho ya Taifa
 
Siasa zimebadilika sana na nyakati hizi nawaona wananchi ni kama wanamaanisha sana kutokana na hali halisi …. ukiangalia Maisha ya miaka ya 1990 kuelekea 2000 huwezi kulinganisha na sasa ...bado ajila zilikuwepo kwa kiasi chake … sasa acha tuone , huko tuendako napaona pakiwa na shughuli kubwa sana kutoka mikononi mwa watanzania hawa
Ndugu Isaya ngoja tusubiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila ninacho kijua ni kwamba wananchi wapo tayari kabisa kuyakubali mabadiliko na kujaribu uongozi wa vyama vingine kuongoza nchi ila CCM hatupo tayari kwa hilo ingawa tuna jua fika hayo ni matakwa ya watanzania tena walio wengi, hivyo kwa hali hiyo lazima itumike nguvu kupingana hilo kwa lazima na si hiyari tena.
Mimi nipo tayari kuungana na mtu yeyote mwenye nia ya kuiondoka ccm madarakani kwa nguvu
 
Mimi nipo tayari kuungana na mtu yeyote mwenye nia ya kuiondoka ccm madarakani kwa nguvu
Huna jeuri hiyo hata ukipata wakuungana nao bado hamna jeuri hiyo.
Ccm kutoka madarakani hadi iamue yenyewe kutoka na si kwa kwa kutolewa na aina ya upinzani zilizopo hapa
 
Huna jeuri hiyo hata ukipata wakuungana nao bado hamna jeuri hiyo.
Ccm kutoka madarakani hadi iamue yenyewe kutoka na si kwa kwa kutolewa na aina ya upinzani zilizopo hapa
Nakubaliana na wewe mkuu mkuu wakati ninafanya kazi Malawi ,nilikuwa nawaona wamalawi mazuzu kuliko hivyo wewe unavyowachukulia watanzania,umefuatilia yanayoendelea huko sasa? APM akitoboa atakuwa mwanaume,so hii la watanzania kuendelea kujari maslahi yetu ya muda mfupi na kusahau kabisa maslahi mapana ya Taifa letu na watoto wetu au
kusubiria au kuomba ccm na serikali ndo waamue kila Jambo linalohusu nchi yetu,maisha yetu naya watoto wetu ni tatizo lingine,but Kama wamalawi wameamka na wanadai nchi yao toka chama tawala sisi tumemkosea nini Mungu hadi tulale usingizi mzito milele?acha tuone
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom