Oloronyo
Member
- Mar 29, 2009
- 80
- 9
Habari za uhakika nilizozipata ni kuwa yule aliyekuwa Mkurugenzi mtendaji wa HITS-TANZANIA Bw.Gerhard May (Pichani)ame-resign siku ya Alhamisi,Wakati huo kukiwa na tetesi kampuni ya Huawei Technologies iliyopewa tenda ya kujenga miundo mbinu ya Hits kusimamishwa kazi hiyo huku kukiwa kuna kila dalili ya kampuni hiyo ya simu kuchukuliwa na Orange ambayo imeshachukua mtandao wa Hits wa nchini Uganda.
Chanzo hicho cha habari kilidai kuwa kuna kila dalili ya yale yaliyotokea enzi za TRITEL kujirudia, kwani kabla ya ya kampuni ya TRITEL kutangaza kufilisika uongozi wa juu wa TRITEL ulihama nyumba walizokuwa wanapanga na kuhamia hotelini kabla ya kutokomea! Kwa sasa Bw.Chris Keeping Mkuu wa kitengo cha biashara cha kampuni hiyo ndiye anayekaimu nafasi yake kiliongezea chanzo hicho.
Chanzo hicho cha habari kilidai kuwa kuna kila dalili ya yale yaliyotokea enzi za TRITEL kujirudia, kwani kabla ya ya kampuni ya TRITEL kutangaza kufilisika uongozi wa juu wa TRITEL ulihama nyumba walizokuwa wanapanga na kuhamia hotelini kabla ya kutokomea! Kwa sasa Bw.Chris Keeping Mkuu wa kitengo cha biashara cha kampuni hiyo ndiye anayekaimu nafasi yake kiliongezea chanzo hicho.