CDM na uteuzi wa CJ

KAUMZA

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
699
237
CHADEMA yampongeza Jaji Chande


Na Mwandishi wetu

SIKU moja baada ya uteuzi wa Jaji Mkuu mpya wa Tanzania, Mohamed Chande, kisha kuapishwa jana, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa pongezi, kikimuahidi ushirikiano, lakini kikitoa tahadhari pia.Akizungumza
na Majira jana, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, Bw. Erasto Tumbo, alisema kuwa chama hicho kinapongeza uteuzi huo na kumtakia heri Jaji Mkuu Chande katika majukumu yake mapya ya kuongoza moja ya mihimili ya dola, mahakama.

"CHADEMA tunatoa pongezi za dhati kwa Jaji Chande kwa kuteuliwa kuwa Jaji Mkuu...lakini tunaomba uteuzi wake usije ukawa kikwazo na kuturudisha nyuma hasa katika vuguvugu la sasa la katiba mpya...aige mfano wa aliyemtangulia, ambaye aliweka bayana msimamo wake.

"Jaji Mkuu Chande ni mtu mkubwa, atambue kuwa sauti yake ina nguvu na inasikilizwa na watu wengi, tunatarajia atakuwa jaji mkuu makini...lakini pia asiwe tatizo kama aliyepita ambaye alishindwa na kuacha kiporo suala la mgombea binafsi," alisema Bw. Tumbo.

Alisema kuwa suala la mgombea binafsi liliwashangaza Watanzansia wengi baada ya mahakama kushindwa kutoa ufafanuzi wa kikatiba na kisheria ambayo ni majukumu ya mhimili huo, badala yake likarusha mpira kwa bunge kwa kusema kuwa katiba ni suala la kisiasa.

"Kwa kweli hakikuwa kitu cha kawaida, wananchi wamekuwa wakitegemea kuwa mahakamani ni mahali ambako ufafanuzi wa kisheria na katiba wa masuala kama hayo unapatikana.

"Lakini mahakama chini ya jaji mkuu aliyepita ikashindwa na kuacha kiporo suala la mgombea binafsi...tunatumaini Jaji Chande atatuongoza vizuri hasa katika kuelekea kupata katiba mpya," alisema Bw. Tumbo.
 
Back
Top Bottom