Katika uchaguzi mdogo unao endelea hivi sasa Tarime kuna mengi ya kujifunza.La msingi hata hivyo ni hili la CCM kutumia nguvu nyingi kupita kiasi.Tumeshuhudia bwana Steven Wasira akitumia hata gari la serikali kufanyia kampeini na hatimaye kuonywa.Tumeshuhudia pia viongozi mbalimbali wa ngazi za juu kabisa wa CCM wakiongeza nguvu katika suala zima la kampeini.Na katika hali isiyo ya kawaida kabisa, hata Mtikila amekuwa 'drafted' kuongeza nguvu na hati za kupigia kura za CCM zinauzwa hovyo mitaani,ushahidi wa kijana yule aliyekamatwa mtaani ni dhahiri.Kwangu mimi hii ni ishara tosha kwamba CCM hawakubaliki tena na wako tayari kutumia mbinu zozote, hata chafu, kufanikisha adhma yao ya kupata kiti cha Tarime.Kama wangekuwa wanakubakika nguvu hizi zisingekuwa za lazima.Lakini ninalojiuliza mimi ni kwamba wanataka kumuongoza nani hasa,na wanachong'ang'nia ni nini?CCM wameshapoteza 'credibility'
kwa wananchi na hawaaminiki tena kabisa.Ni vema wakalitambua hilo na wakapisha wengine ambao wana nia ya kweli ya kuwasaidia wananchi wa Tanzania.CCM wanakotupeleka siko,tunawaomba kwa nia njema kabisa waondoke.
kwa wananchi na hawaaminiki tena kabisa.Ni vema wakalitambua hilo na wakapisha wengine ambao wana nia ya kweli ya kuwasaidia wananchi wa Tanzania.CCM wanakotupeleka siko,tunawaomba kwa nia njema kabisa waondoke.