Uwezo Tunao
JF-Expert Member
- Nov 14, 2010
- 6,942
- 1,190
Hapo nyuma wananchi tulionyesha wasiwasi mkubwa na nyinyi kujihusisha na katiba kwa peke yenu, baada ya kutuibia uchaguzi wetu October 2010 ikatuondoa kabisa imani kwenu lakini bado mkajing'ang'aniza kwamba tuwaamini na kazi hii nyeti; ajabu bado tena mmeingiza ule ule mtindo wenu wa usanii hata kwa mambo yasiohitaji mzaha.
Kwa mtaji wa matangazo ya muswada mliogeuza juu chini na kulitoa kwenye gazeti rasmi ya serikali sasa imetuacha bila masuali zaidi kwamba kazi hii kamwe hamuiwezi na wala si wa kuaminika na lolote tena kwa kuchagua kuweka pembeni wadau wengine na kujifanyia tu mambo mpendavyo sirini.
Tunasema kama mnadhani ni mzaha tena na msirudishe matakwa sahihi ya umma badala ya matakwa ya serikali kwenye katiba basi uvumilivu wetu kuwapa muda zaidi ni mpaka hapo April 08, 2011 ambapo baada ya hapo mtakua mmetushinikiza kwenye mfululizo wa maandamano mpaka kieleweke.
Kwa mtaji wa matangazo ya muswada mliogeuza juu chini na kulitoa kwenye gazeti rasmi ya serikali sasa imetuacha bila masuali zaidi kwamba kazi hii kamwe hamuiwezi na wala si wa kuaminika na lolote tena kwa kuchagua kuweka pembeni wadau wengine na kujifanyia tu mambo mpendavyo sirini.
Tunasema kama mnadhani ni mzaha tena na msirudishe matakwa sahihi ya umma badala ya matakwa ya serikali kwenye katiba basi uvumilivu wetu kuwapa muda zaidi ni mpaka hapo April 08, 2011 ambapo baada ya hapo mtakua mmetushinikiza kwenye mfululizo wa maandamano mpaka kieleweke.